< 1 Ukorintiyawa 11 >

1 Sun lisosin limang nafo men, nafo na men din su lisosin nafo Kristi.
Igeni mfano wangu, kama ninavyouiga mfano wa Kristo.
2 Nene in di liru mine bara na idin lizunu nin mi nan nya nimon vat tutun inin yisin gangang nan nya nadadu alenge na inani munu.
Ninawasifu kwa kuwa mnanikumbuka katika kila jambo na kwa kushika mafundisho niliyowapa.
3 Nene ndinin su iyinin Kristiari unan nbu nko kame gankilime, a gakilime ubun nwani, a Kutellẹ amere unan bun nKristi.
Napenda mfahamu kwamba kichwa cha kila mwanaume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanaume, nacho kichwa cha Kristo ni Mungu.
4 Gakilime ka na ata nlira sa ayene ubun a litime kirno na ana litime ngongon ba.
Kila mwanaume anayeomba au kutoa unabii akiwa amefunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake.
5 Nani vat uwani ule na ata nlira sa a yene ubun sa ukirrunu litime na nà litime ngongon ba. Bara usosin imon irumere nin woru apele titime.
Naye kila mwanamke anayeomba au kutoa unabii pasipo kufunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake, kwani ni sawa na yeye aliyenyoa nywele.
6 Asa na uwani ma kiru litime ba, na awarin titime cot. Andi imon cingharib uwani werin sa apelu titime, nbara a kiru litime.
Kama mwanamke hatajifunika kichwa chake, basi inampasa kunyoa nywele zake. Lakini kama ni aibu kwa mwanamke kukata au kunyoa nywele zake, basi afunike kichwa chake.
7 Naneri na gankilime wa kiru litime ba, bara na ame kuyeleri nin gongon Kutellẹ. Ame uwani ngogon ngankilimeri.
Haimpasi mwanaume kufunika kichwa chake kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na utukufu wa Mungu, lakini mwanamke ni utukufu wa mwanaume.
8 Bara na iwa ke gankilime unuzu kitin nwani ba, uwaneri iwa keghe unuzu kitin gankilime.
Kwa maana mwanaume hakutoka kwa mwanamke, bali mwanamke alitoka kwa mwanaume.
9 Na iwa ke gankilime bara uwani ba, iwana ke uwani bara gankilimeri.
Wala mwanaume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanaume.
10 Unere nta uwani cau ayita nin litappa tigo litime, bara nono kadura Kutellẹ.
Kwa sababu hii na kwa sababu ya malaika, inampasa mwanamke awe na ishara ya mamlaka juu yake.
11 Vat nin nani, kitin Cikilari, uwani sosin lisosin litime ugan nin gankilime ba, a na gankilime wang sosin lisosin litime ugan nin wani ba.
Lakini katika Bwana, mwanamke hajitegemei pasipo mwanaume na mwanaume hajitegemei pasipo mwanamke.
12 Nafo na uwani na dak unuzu kitin gankilime, nanare gankilime na dak unuzu kitin nwani. A imon vat unuzu kiti Kutellẹ.
Kama vile mwanamke alivyoumbwa kutoka kwa mwanaume, vivyo hivyo mwanaume huzaliwa na mwanamke. Lakini vitu vyote vyatoka kwa Mungu.
13 Sun asarawe ikosu ulire nin natimine, udi dert uwani ti nlira udu kiti Kutellẹ. nin litime fwangha?
Hukumuni ninyi wenyewe: Je, inafaa kwa mwanamke kumwomba Mungu bila kufunika kichwa chake?
14 Ani na makeke litime ndurso minu nenge, asa gankilime di nin titi jakaka imon ncighari kitime,
Je, maumbile ya asili hayatufundishi kuwa ni aibu kwa mwanaume kuwa na nywele ndefu?
15 Ani na makeke ndurso minu nwo asa uwani di nin titi ti jakaka na imon ngogon mere ba?
Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni utukufu kwake? Kwa maana mwanamke amepewa nywele ndefu ili kumfunika.
16 Asa umon di nin mong uliru ugang nin lele, na arik dinin namong al ada ugang ba, sa nan nya niti nlira Kutellẹ wang.
Kama mtu anataka kubishana juu ya jambo hili, sisi wala makanisa ya Mungu hatutambui desturi nyingine.
17 Nan nya nale adue, na ndin liru mine ba, bara asa izuro ligowe, na idin dazu nin nimon icine ba sai inanzan.
Basi katika maagizo yafuatayo, siwezi kuwasifu, kwa sababu mkutanikapo si kwa ajili ya faida bali kwa hasara.
18 Nin cizune, nna lanza au asa izuro ligowe kuti nlira, usali munu nati din nan nya mine, na nyina nin lirumine vat ba.
Kwanza, mnapokutana kama kanisa, nasikia kwamba kuna mgawanyiko miongoni mwenu, nami kwa kiasi fulani nasadiki kuwa ndivyo ilivyo.
19 Uso gwas na ise naissin nan nya mine, bara alenge na iyinna nin liyissin mine inan se useru nan nya mine.
Bila shaka lazima pawe na tofauti miongoni mwenu ili kuonyesha ni nani anayekubaliwa na Mungu.
20 Bara iwa zuro ligowe na idin li ujibin NCikilare ba.
Mkutanikapo pamoja si chakula cha Bwana mnachokula,
21 Asa idin le, kogha mine dirtinu nli ninme imonli, a amon dutu nin kukpon, a umon na yita nin kushiton ntoro.
kwa kuwa mnapokula, kila mmoja wenu anakula bila kuwangoja wengine. Mmoja hukaa njaa na mwingine analewa.
22 Na idi nin nilari na imali iso nan nye ba? din yassu kilari Kutellẹ ini tizza anan likimon ilanza ncingha? Nyaghari nba bellin minu? Meng nrù munua? Na nma zazun minu kitene lile imone ba!
Je, hamna nyumbani kwenu ambako mnaweza kula na kunywa? Au mnalidharau kanisa la Mungu na kuwadhalilisha wale wasio na kitu? Niwaambie nini? Je, niwasifu juu ya jambo hili? La, hasha!
23 Bara nna seru kitin Ncikilari ilenge imon na meng wang nani minu, Cikilari Yisa, nin kitike na iwa nari ame, ayauna ufungule.
Kwa maana mimi nilipokea kutoka kwa Bwana yale niliyowapa ninyi, kwamba Bwana Yesu, usiku ule aliposalitiwa, alitwaa mkate,
24 Kimal ntin lira, apuco uni aworo, “ilele kidowo nigharidi, ka naki di bara anung, man suzun nani ilizizin ninmi”
naye akiisha kushukuru, akaumega, akasema, “Huu ndio mwili wangu, uliotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”
25 Nanere tutung awa yaun kakukke kimal jibe, aworo, “kakkuk kane kan ciu nliru upese ari nannya nmī ning. Suzun nani kubi kongo na idin sonē nin kakukke inan lizino nin me.''
Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu. Fanyeni hivi kila mnywapo, kwa ukumbusho wangu.”
26 Bara vat kubi ko na ileo ufungal ulele nin kakkuk kane, idin girzunu nkul Ncikilarere udu lirin same.
Maana kila mlapo mkate huu na kunywea kikombe hiki, mnatangaza mauti ya Bwana mpaka ajapo.
27 Vat nlege na adin li ufungalle sa adin so kakkuk Ncikilare a ayita likara linanzang ama yitu nin kulapi kiti kidowo nin mī Ncikilare.
Kwa hiyo, mtu yeyote alaye mkate huo au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa na hatia ya dhambi juu ya mwili na damu ya Bwana.
28 Na unit tu adumun litime, ma anin li ufungal ani sono kakukke.
Inampasa mtu ajichunguze mwenyewe, kabla ya kula mkate na kukinywea kikombe.
29 Vat ulenge na adin li aso sa uyenun ngongong kidowo Ncikilare adin li aso usharawari litime.
Kwa maana mtu yeyote alaye na kunywa pasipo kuutambua mwili wa Bwana, hula na kunywa hukumu juu yake mwenyewe.
30 Unnare nta among mine gbardan di nin sali nakara a tikonu, among mine wang nkuzu.
Hii ndiyo sababu wengi miongoni mwenu ni wagonjwa na dhaifu na wengine wenu hata wamekufa.
31 Bara asa ti dumuzuna atibite, iba sunari ushara ba.
Lakini kama tungejichunguza wenyewe tusingehukumiwa.
32 Nani asa idin su nari ushara, ti dinse ugwaru kitin Ncikilare, bara iwa da walin nari ligowe nin yih.
Tunapohukumiwa na Bwana, tunaadibishwa ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.
33 Bara nani nuana ning, asa ida zuro ligowe kiti kileowe son ncà nati.
Kwa hiyo, ndugu zangu, mkutanikapo pamoja ili kula, mngojane.
34 Asa umon din lanzu kukpon, na ali kilari, bara iwa da zuro ligowe nan da so ushara kubi ko nan nda nma bellun minu imn ilenge na idin nbun.
Kama mtu akiwa na njaa, ale nyumbani kwake ili mkutanapo pamoja msije mkahukumiwa. Nami nitakapokuja nitawapa maelekezo zaidi.

< 1 Ukorintiyawa 11 >