< 路加福音 21 >

1 舉目一望,看見富人把他們的獻儀投入銀庫內,
Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
2 又看見一個貧苦的寡婦,把兩文錢投入裡面,
Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
3 遂說:「我實在告訴你們:這個寡婦比別人投入的更多,
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
4 因為眾人都是拿他們多餘的投入,作為給又主的獻儀;而這個寡婦卻是從她的不足中,把她所有的生活費都投入了。
Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
5 有些人正談論聖殿是用美麗的石頭,和還願的獻品裝飾的,耶穌說:
Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
6 「你們所看見的這一切,待那時日一到,沒有一塊石頭留在另一塊石頭上,而不被拆毀的。」
“Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
7 他們遂問說:「師傅,那麼什麼時候要發生這些事﹖這些事要發生的時候,將有什麼先兆﹖」
Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
8 耶穌說:「你們要謹慎,不要受敢騙! 因為將有許多人,假冒我名字來說:我就是(默西亞);又說:時期近了。你們切不可跟隨他們。
Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
9 你們幾時聽見戰爭及叛亂,不要驚惶! 因為這些事必須先要發生,但還不即刻是結局。」
Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
10 耶穌又給他們說:「民族要起來攻擊民族,國家攻擊國家;
Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
11 將有大地震,到處有饑荒及瘟疫;將出現可怖的異象,天上要有巨大的凶兆。
Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
12 但是這一切事以前,為了失名字的緣故,人們要下手把你們拘捕、迫害、解送到會堂,並囚在獄中;且押送到君王及總督之前,
“Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
13 為給你們一個作證的機會。
Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
14 所以,你們心中要鎮定,不要事先考慮申辯,
Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
15 因為我要給你們口才和明智,是你們的一切仇敵所不能抵抗及辯駁的。
Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
16 你們要為父母、兄弟、親戚及朋友所出賣;你們中有一些要被殺死。
Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
17 你們要為了我的名字,受眾人的憎恨;
Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
18 但是,連你們的一根頭髮,也不會失落。
Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
19 你們要憑著堅忍,保全你們的靈魂。」
Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
20 幾時你們看見耶路撒冷被軍隊圍困,那時你們便知道:她的荒涼近了。
“Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
21 那時在猶太的,要逃往山中;在京都的,要離去;在鄉間的,不要茌進京。
Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
22 因為這是報復日子,為要應驗所記載的一切。
Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
23 在那些日子內,懷用孕的及哺的乳的,是禍的,因為要有大難降臨這地方,要有義怒臨於這百姓身上。
Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
24 他們要倒在劍刃之下,要被擄往列國;耶肋米亞要受異民蹂躝,直到異民的時期滿限。
Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
25 在日月星辰上,將有異兆出現;在地上,萬國要因海洋波濤的怒號而驚惶失措。
“Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
26 眾人要因恐懼,等待即將臨於天下的事而昏絕,因為諸天的萬象將要搖動。
Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
27 那時,他們要看見人子,帶著威能及莫大光榮乘雲降來。
Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
28 這些事開始發生時,你們應當挺起身來,抬起你們的頭,因為你們的救援近了。」
Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
29 耶穌又給他們設了一個比喻:「你們看看無花果樹及各種樹木,
Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
30 幾時你們看見它們已經發芽,就知道夏天已經近了。
Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
31 同樣你們看見這些事發生了,也應知道天主的國近了。
Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
32 我實在告訴你們:非等一切事發生了,這一代絕不會過去。
“Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
33 天地要過去,但是,我的話決不會過去。
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
34 你們應當謹慎,免得你們心為宴飲沈醉,及人生的掛慮所累時,那意想不到的日子臨於你們,
“Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
35 因為日子有如羅網,臨於全地面的一切居民。
Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
36 所以你們應當時時醒寤祈禱,為便你們能逃脫即將發生的這一切事,並能立於人子之前。」
Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
37 耶穌白天在聖殿施教,黑夜便出去,到名叫橄欖的山上住宿。
Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
38 眾百姓清早起來,到祂跟前,在聖殿裏聽祂講道。
Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.

< 路加福音 21 >