< Jeremias 37 >

1 Zedekias, Joasiases søn, blev konge Konjas, Jojakims søns sted, idet Kong Nebukadrezar af Babel satte ham til Konge i Judas Land.
Sedekia mwana wa Yosia akafanywa kuwa mfalme wa Yuda na Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye akatawala mahali pa Yehoyakini mwana wa Yehoyakimu.
2 Men han og hans Mænd og Landets Befolkning hørte ikke på de Ord, HERREN talede ved Profeten Jeremias.
Lakini sio Sedekia, wala watumishi wake, wala watu wa nchi walisikiliza maneno ya Bwana aliyonena kupitia kwa nabii Yeremia.
3 Kong Zedekias sendte Jukal. Sjelemjas Søn, og Præsten Zefanja, Maasejas Søn, til Profeten Jeremias og lod sige: "Gå i Forbøn for os hos HERREN vor Gud!"
Hata hivyo, Mfalme Sedekia akamtuma Yehukali mwana wa Shelemia, pamoja na kuhani Sefania mwana wa Maaseya kwa nabii Yeremia na ujumbe huu: “Tafadhali utuombee kwa Bwana, Mungu wetu.”
4 Dengang gik Jeremias frit ud og ind blandt Folket, thi man havde endnu ikke kastet ham i Fængsel.
Wakati huu Yeremia alikuwa huru kuingia na kutoka katikati ya watu, kwa sababu alikuwa bado hajatiwa gerezani.
5 Faraos Hær var rykket ud fra Ægypten; og da kaldæerne, som belejrede Jerusalem, fik Nys herom, var de brudt op fra Jerusalem.
Jeshi la Farao lilikuwa limetoka Misri, nao Wakaldayo waliokuwa wameuzunguka Yerusalemu kwa majeshi waliposikia taarifa kuhusu jeshi hilo walijiondoa Yerusalemu.
6 Da kom HERRENs Ord til Profeten Jeremias således:
Ndipo neno la Bwana likamjia nabii Yeremia kusema:
7 Så siger HERREN, Israels Gud: Således skal du sige til Judas Konge, som har sendt Bud til dig for at rådspørge mig: Se, Faraos Hær, som er rykket ud for at hjælpe eder, skal vende hjem til Ægypten;
“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Mwambie mfalme wa Yuda aliyekutuma uniulize mimi, ‘Jeshi la Farao lililotoka kuja kukusaidia litarudi katika nchi yake yenyewe, yaani Misri.
8 og Kaldæerne skal vende tilbage og angribe denne By, indtage og afbrænde den.
Kisha Wakaldayo watarudi na kushambulia mji huu, watauteka na kuuchoma moto.’
9 Så siger HERREN: Når ikke eder selv ved at sige: "Kaldæerne drager bort fra os for Alvor!" Thi de drager ikke bort.
“Hili ndilo Bwana asemalo: Msijidanganye wenyewe mkifikiri, ‘Hakika Wakaldayo watatuacha na kwenda zao.’ Hakika hawatawaacha!
10 Ja, om, I så slog hele Kaldæernes Hær, der angriber eder, så der kun blev nogle sårede tilbage, hver i sit Telt, så skulde de stå op og afbrænde denne By.
Hata kama mngelishinda jeshi lote la Wakaldayo linalowashambulia ninyi, na wakawa ni watu waliojeruhiwa tu waliobaki kwenye mahema yao, wangetoka na kuuchoma mji huu moto.”
11 Da Kaldæernes Hær var brudt op fra Jerusalem for Faraos Hær,
Baada ya jeshi la Wakaldayo kujiondoa kutoka Yerusalemu kwa sababu ya jeshi la Farao,
12 gik Jeremias ud af Jerusalem for at drage til Benjamins Land og få en Arvelod iblandt Befolkningen.
Yeremia akaanza kuondoka mjini ili kwenda nchi ya Benyamini ili akapate sehemu yake ya milki miongoni mwa watu huko.
13 Men da han kom til Benjaminsporten, var der en Vagthavende ved Navn Jirija, en Søn af Hananjas Søn Sjelemja, og han greb Profeten Jeremias og sagde: "Du vil løbe over til Kaldæerne."
Lakini alipofika kwenye Lango la Benyamini, mkuu wa walinzi, ambaye jina lake lilikuwa Iriya mwana wa Shelemia mwana wa Hanania, akamkamata Yeremia na kusema, “Wewe unakwenda kujiunga na Wakaldayo!”
14 Jeremias svarede: "Det er Løgn; jeg vil ikke løbe over til Kaldæerne." Jirija vilde dog ikke høre ham, men greb ham og bragte ham til Fyrsterne;
Yeremia akasema, “Hiyo si kweli, mimi sijiungi na Wakaldayo.” Lakini Iriya hakumsikiliza; badala yake, akamkamata Yeremia na kumpeleka kwa maafisa.
15 og Fyrsterne vrededes på Jeremias, slog ham og lod ham bringe til Statsskriveren Jonatans Hus; thi det havde de gjort til Fængsel.
Wakamkasirikia Yeremia, wakaamuru apigwe, na akafungwa katika nyumba ya Yonathani mwandishi waliyokuwa wameifanya gereza.
16 Således kom Jeremias i Fangehuset i kælderen; og der sad han en Tid lang.
Yeremia akawekwa kwenye chumba kilichofukuliwa chini, kilichojengwa kwa zege ndani ya gereza chini ya ngome, akakaa huko kwa muda mrefu.
17 Men Kong Zedekias sendte Bud og lod ham hente; og Kongen spurgte ham i al Hemmelighed i sit Palads: "Er der et Ord fra HERREN?" Jeremias svarede: "Ja, der er: Du skal overgives i Babels Konges Hånd."
Kisha Mfalme Sedekia akatumana aletwe katika jumba la kifalme, mahali alipomuuliza kwa siri, “Je, kuna neno lolote kutoka kwa Bwana?” Yeremia akajibu, “Ndiyo, utatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli.”
18 Derpå sagde Jeremias til Kong Zedekias: "Hvad Synd har jeg gjort imod dig, dine Mænd og dette Folk, siden I har kastet mig i Fængsel?
Kisha Yeremia akamwambia Mfalme Sedekia, “Nimefanya kosa gani dhidi yako na maafisa wako au watu hawa, hata ukanitia gerezani?
19 Og hvor er nu eders Profeter, som profeterede for eder, at Babels Konge ikke skulde komme over eder og dette Land?
Wako wapi manabii wako waliokutabiria wakisema, ‘Mfalme wa Babeli hatakushambulia wewe wala nchi hii?’
20 Så hør da, Herre Konge! Lad min Bøn nå dig og lad mig ikke bringe tilbage til Statsskriveren Jonatans Hus, af jeg ikke skal dø der!"
Lakini sasa, bwana wangu mfalme, tafadhali sikiliza. Niruhusu nilete maombi yangu mbele yako, usinirudishe kwenye nyumba ya Yonathani mwandishi, nisije nikafia humo.”
21 Da bød Kong Zedekias, at man skulde holde Jeremias i Varetægt i Vagtforgården; og der gaves ham daglig et Stykke Brød fra Bagerens Gade, indtil Brødet slap op i Byen. Således sad nu Jeremias i Vagtforgården.
Ndipo Mfalme Sedekia akatoa maagizo Yeremia awekwe katika ua wa walinzi, na apewe mkate kutoka mitaa ya waokaji kila siku mpaka mikate yote katika mji itakapokwisha. Kwa hiyo Yeremia akabaki katika ua wa walinzi.

< Jeremias 37 >