< Ordsprogene 9 >

1 Visdommen bygged sig Hus, rejste sig støtter syv,
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
2 slagted sit Kvæg og blanded sin Vin, hun har også dækket sit Bord;
Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
3 hun har sendt sine Terner ud, byder ind på Byens højeste Steder:
Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
4 Hvo som er tankeløs, han komme hid, jeg taler til dem, som er uden Vid:
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
5 Kom og smag mit Brød og drik den Vin, jeg har blandet!
Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
6 Lad Tankeløshed fare, så skal I leve, skrid frem ad Forstandens Vej!
Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 Tugter man en Spotter, henter man sig Hån; revser man en gudløs, høster man Skam;
“Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
8 revs ikke en Spotter, at han ikke skal hade dig, revs den vise, så elsker han dig;
Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
9 giv til den vise, så bliver han visere, lær den retfærdige, så øges hans Viden.
Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
10 HERRENs Frygt er Visdoms Grundlag, at kende den HELLIGE, det er Forstand.
“Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
11 Thi mange bliver ved mig dine Dage, dine Livsårs Tal skal øges.
Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
12 Er du viis, er det til Gavn for dig selv; spotter du, bærer du ene Følgen!
Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
13 Dårskaben, hun slår sig løs og lokker og kender ikke til Skam;
Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
14 hun sidder ved sit Huses indgang, troner på Byens Høje
Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
15 og byder dem ind, der kommer forbi, vandrende ad deres slagne Vej:
akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
16 Hvo som er tankeløs, han komme hid, jeg taler til dem, som er uden Vid:
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
17 Stjålen Drik er sød, lønligt Brød er lækkert!
“Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
18 Han ved ej, at Skyggerne dvæler der, hendes Gæster er i Dødsrigets Dyb. (Sheol h7585)
Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)

< Ordsprogene 9 >