< Acts 4 >

1 And as they spoke to the people, the priests and the captain of the temple and the Sadducees approached them,
Wakati Petro na Yohana walipokuwa wakisema na watu, makuhani, mkuu wa walinzi wa Hekalu na Masadukayo wakawajia,
2 being greatly annoyed because of their teaching the people, and proclaiming in Jesus the resurrection of the dead.
huku wakiwa wamekasirika sana kwa sababu mitume walikuwa wanawafundisha watu na kuhubiri kwamba kuna ufufuo wa wafu ndani ya Yesu.
3 And they threw hands on them, and put them in custody for the morrow, for it was now evening.
Wakawakamata Petro na Yohana na kuwatia gerezani mpaka kesho yake kwa kuwa ilikuwa jioni.
4 But many of those who heard the word believed, and the number of the men became about five thousand.
Lakini wengi waliosikia lile neno waliamini, idadi yao ilikuwa yapata wanaume 5,000.
5 And it came to pass on the morrow, to be assembled in Jerusalem, their rulers, and elders, and scholars,
Kesho yake, viongozi wa Kiyahudi, wazee na walimu wa sheria wakakusanyika Yerusalemu.
6 and Annas the high priest, and Caiaphas, and John, and Alexander, and as many as were of the high priestly family.
Walikuwepo kuhani mkuu Anasi, Kayafa, Yohana, Iskanda, na wengi wa jamaa ya kuhani mkuu.
7 And after placing them in the midst, they inquired, By what power, or in what name, have ye done this?
Baada ya kuwasimamisha Petro na Yohana katikati yao, wakawauliza, “Ni kwa uwezo gani au kwa jina la nani mmefanya jambo hili?”
8 Then Peter being filled with the Holy Spirit, said to them, Rulers of the people, and elders of Israel,
Petro, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akajibu, “Enyi watawala na wazee wa watu,
9 if we are examined today about a good deed, of a feeble man, by what this man has been healed,
kama leo tukihojiwa kwa habari ya mambo mema aliyotendewa yule kiwete na kuulizwa jinsi alivyoponywa,
10 be it known to you all, and to all the people of Israel, that in the name of Jesus Christ the Nazarene, whom ye crucified, whom God raised from the dead, by this, this man stands here before you healthy.
ijulikane kwenu nyote na kwa watu wote wa Israeli kwamba: Ni kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulubisha lakini Mungu akamfufua kutoka kwa wafu, kwa jina hilo mtu huyu anasimama mbele yenu akiwa mzima kabisa.
11 This is the stone that was rejected by you who build, which became into the head of the corner.
Huyu ndiye “‘jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilikataa, ambalo limekuwa jiwe kuu la pembeni.’
12 And salvation is not in any other man, for there is no other name under the heaven, that has been given among men, by which we must be saved.
Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hakuna jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.”
13 Now when they saw the boldness of Peter and John, and having perceived that they are illiterate and uneducated men, they marveled. And they recognized them, that they had been with Jesus.
Wale viongozi na wazee walipoona ujasiri wa Petro na Yohana na kujua ya kuwa walikuwa watu wa kawaida, wasio na elimu, walishangaa sana, wakatambua kwamba hawa watu walikuwa na Yesu.
14 And seeing the man who was healed standing with them, they had nothing to contradict.
Lakini kwa kuwa walikuwa wanamwona yule kiwete aliyeponywa amesimama pale pamoja nao, hawakuweza kusema lolote kuwapinga.
15 But after commanding them to go outside of the council, they conferred among each other,
Wakawaamuru watoke nje ya Baraza la Wayahudi wakati wakisemezana jambo hilo wao kwa wao.
16 saying, What will we do to these men? For that indeed a notable sign has happened by them, is apparent to all who dwell in Jerusalem, and we cannot deny it.
Wakaulizana, “Tuwafanyie nini watu hawa? Hatuwezi kukanusha muujiza huu mkubwa walioufanya ambao ni dhahiri kwa kila mtu Yerusalemu.
17 But that it may not spread on further among the people, let us threaten them with threats to speak no longer in this name, to not one man.
Lakini ili kuzuia jambo hili lisiendelee kuenea zaidi kwa watu, ni lazima tuwaonye watu hawa ili wasiseme tena na mtu yeyote kwa jina la Yesu.”
18 And having called them, they commanded them entirely, not to utter nor to teach in the name of Jesus.
Kisha wakawaita tena ndani na kuwaamuru wasiseme wala kufundisha kamwe kwa hili jina la Yesu.
19 But Peter and John having replied to them, they said, Whether it is right in the sight of God to hearken to you rather than God, judge ye.
Lakini Petro na Yohana wakajibu, “Amueni ninyi wenyewe iwapo ni haki mbele za Mungu kuwatii ninyi kuliko kumtii Mungu.
20 For we are not able not to speak what we saw and heard.
Lakini sisi hatuwezi kuacha kusema yale tuliyoyaona na kuyasikia.”
21 And they, having further threatened, released them, finding nothing how they might punish them, because of the people. Since all glorified God for that which happened.
Baada ya vitisho vingi, wakawaacha waende zao. Hawakuona njia yoyote ya kuwaadhibu, kwa sababu ya watu, kwa kuwa watu wote walikuwa wakimsifu Mungu kwa kile kilichokuwa kimetukia.
22 For the man was more than forty years old on whom this sign of healing had occurred.
Kwa kuwa umri wa yule mtu aliyekuwa ameponywa kwa muujiza ulikuwa zaidi ya miaka arobaini.
23 And after being released, they went to their own men, and reported as many things as the chief priests and the elders said to them.
Punde Petro na Yohana walipoachiliwa, walirudi kwa waumini wenzao wakawaeleza waliyoambiwa na viongozi wa makuhani na wazee.
24 And those who heard lifted up a voice to God with one accord, and said, Thou Master, the God who made the heaven and the earth and the sea, and all things in them.
Watu waliposikia hayo, wakainua sauti zao, wakamwomba Mungu kwa pamoja, wakisema, “Bwana Mwenyezi, uliyeziumba mbingu na nchi na bahari, na vitu vyote vilivyomo.
25 He who said through the mouth of thy boy David, Why do the nations rage, and the peoples meditate vain things?
Wewe ulisema kwa Roho Mtakatifu kupitia kwa kinywa cha baba yetu Daudi, mtumishi wako, ukasema: “‘Mbona mataifa wanaghadhibika, na kabila za watu zinawaza ubatili?
26 The kings of the earth stood up, and the rulers were gathered together, against the Lord, and against his Christ.
Wafalme wa dunia wamejipanga, na watawala wanakusanyika pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.’
27 For in truth, against thy holy Boy Jesus, whom thou anointed, both Herod and Pontius Pilate, with the Gentiles and the peoples of Israel, were gathered together,
Ni kweli Herode na Pontio Pilato pamoja na watu wa Mataifa na Waisraeli, walikusanyika katika mji huu dhidi ya mwanao mtakatifu Yesu uliyemtia mafuta.
28 to do as many things as thy hand and thy purpose predetermined to happen.
Wao wakafanya yale ambayo uweza wako na mapenzi yako yalikuwa yamekusudia yatokee tangu zamani.
29 And now, Lord, look upon their threats, and grant to thy bondmen with all boldness to speak thy word,
Sasa, Bwana angalia vitisho vyao na utuwezeshe sisi watumishi wako kulinena neno lako kwa ujasiri mkuu.
30 by thy stretching forth thy hand for healing, and signs and wonders to happen through the name of thy holy Boy Jesus.
Nyoosha mkono wako ili kuponya wagonjwa na kutenda ishara na miujiza kwa jina la Mwanao mtakatifu Yesu.”
31 And when they prayed, the place in which they were assembled was shaken, and they were all filled with the Holy Spirit, and they spoke the word of God with boldness.
Walipokwisha kuomba, mahali walipokuwa wamekutanika pakatikiswa, wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.
32 And the multitude of those who believed were of one heart and soul. And not even one man said that anything of the things that was possessed by him was his own, but all things were common to them.
Wale walioamini wote walikuwa na moyo mmoja na nia moja. Wala hakuna hata mmoja aliyesema chochote alichokuwa nacho ni mali yake mwenyewe, lakini walishirikiana kila kitu walichokuwa nacho.
33 And with great power the apostles gave back the testimony of the resurrection of the Lord Jesus, and great grace was upon them all.
Mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwa Bwana Yesu kwa nguvu nyingi na neema ya Mungu ilikuwa juu yao wote.
34 For not even any needy was among them, for as many as were owners of lands or houses, selling, they brought the proceeds of the things that were sold,
Wala hapakuwepo mtu yeyote miongoni mwao aliyekuwa mhitaji, kwa sababu mara kwa mara wale waliokuwa na mashamba na nyumba waliviuza, wakaleta thamani ya vitu vilivyouzwa,
35 and placed them at the apostles' feet. And it was distributed to each, according as any man had need.
wakaiweka miguuni pa mitume, kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake.
36 And Joses, who was surnamed by the apostles, Barnabas (which is, being translated, son of encouragement), a Levite, a Cypriot by nationality,
Yosefu, Mlawi kutoka Kipro, ambaye mitume walimwita Barnaba (maana yake Mwana wa Faraja),
37 having sold a field that was possessed by him, brought the money and placed it at the apostles' feet.
aliuza shamba alilokuwa nalo, akaleta hizo fedha alizopata na kuziweka miguuni pa mitume.

< Acts 4 >