< Exodus 26 >

1 “Moreover you shall make the tabernacle with ten curtains of fine twined linen, and blue, and purple, and scarlet, with cherubim. You shall make them with the work of a skillful workman.
Lazima ufanye hiyo maskani iwe na mapazia kumi ifanye ya nguo ya kitani nzuri ya kusokota, pamoja na nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, pamoja na makerubi. Kazi ya fundi stadi.
2 The length of each curtain shall be twenty-eight cubits, and the width of each curtain four cubits: all the curtains shall have one measure.
Urefu wa kila pazia utakuwa dhiraa ishirini na nane, na upana wa kila pazia utakuwa dhiraa nne. Mapazia yote yatakuwa ya kipimo kimoja.
3 Five curtains shall be coupled together to one another, and the other five curtains shall be coupled to one another.
Mapazia matano yataungwa pamoja, na mapazia matano mengine yataungwa pamoja.
4 You shall make loops of blue on the edge of the one curtain from the edge in the coupling, and you shall do likewise on the edge of the curtain that is outermost in the second coupling.
Lazima ufanye tanzi za rangi ya samawati upande wa mwisho wa pazia moja katika ule upindo wa fungu lake. Vivyo hivyo utafanya upande wa mwisho wa ile pazia iliyo, katika fungu la pili.
5 You shall make fifty loops in the one curtain, and you shall make fifty loops in the edge of the curtain that is in the second coupling. The loops shall be opposite one another.
Fanya matanzi hamsini katika pazia moja, na matanzi hamsini katika upande wa mwisho wa ile pazia iliyo katika kuungana kwa pili.
6 You shall make fifty clasps of gold, and couple the curtains to one another with the clasps. The tabernacle shall be a unit.
Fanya hivi ili hizo tanzi zielekeana. Kisha ufanye vifungo hamsini vya dhahabu, na kuunganisha hayo mapazia pamoja kwa vile vifungo na hiyo maskani itakuwa ni moja.
7 “You shall make curtains of goats’ hair for a covering over the tabernacle. You shall make eleven curtains.
Lazima ufanye mapazia ya nywele za mbuzi yawe hema juu ya maskani. Lazima ufanye mapazia kumi na moja.
8 The length of each curtain shall be thirty cubits, and the width of each curtain four cubits: the eleven curtains shall have one measure.
Urefu wa kila pazia utakuwa dhiraa thelathini, na upana wa kila pazia utakuwa dhiraa nne. Hayo mapazia kumi na moja yatakuwa ya kipimo kimoja.
9 You shall couple five curtains by themselves, and six curtains by themselves, and shall double over the sixth curtain in the forefront of the tent.
Lazima utaunganisha mapazia matano mbali, na mapazia sita mbali, na lile pazia la sita utalikunja hapo upande wa mbele wa ile hema.
10 You shall make fifty loops on the edge of the one curtain that is outermost in the coupling, and fifty loops on the edge of the curtain which is outermost in the second coupling.
Ufanye tanzi hamsini upande wa mwisho wa pazia lile lililo la mwisho katika hayo yaliyounganywa pamoja, na tanzi hamsini upande wa mwisho wa lile pazia lililo nje katika hayo ya pili yaliyounganywa pamoja.
11 You shall make fifty clasps of bronze, and put the clasps into the loops, and couple the tent together, that it may be one.
Kisha ufanye vifungo hamsini vya shaba, na kuvitia vile vifungo katika zile tanzi, na kuiunganya ile hema pamoja, ili iwe hema moja.
12 The overhanging part that remains of the curtains of the tent—the half curtain that remains—shall hang over the back of the tabernacle.
Kipande kile kilichosalia, kile kiangukacho, cha yale mapazia ya hema, itaanguka huko upande wa nyuma wa maskani.
13 The cubit on the one side and the cubit on the other side, of that which remains in the length of the curtains of the tent, shall hang over the sides of the tabernacle on this side and on that side, to cover it.
Lazima kuwe na dhiraa moja upande mmoja, na ile dhiraa moja upande wa pili - ya urefu wa mapazia ya hema uliosalia, zitaanguka katika ubavu wa maskani upande huu na upande huu, ili kuifunika.
14 You shall make a covering for the tent of rams’ skins dyed red, and a covering of sea cow hides above.
Nawe fanya kifuniko cha ile hema, cha ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
15 “You shall make the boards for the tabernacle of acacia wood, standing upright.
Nawe lazima ufanye hizo fremu za maskani za mti wa mjohoro.
16 Ten cubits shall be the length of a board, and one and a half cubits the width of each board.
Kila fremu utakuwa na urefu wa dhiraa kumi, na upana wake kila ubao utakuwa dhiraa moja na nusu.
17 There shall be two tenons in each board, joined to one another: thus you shall make for all the boards of the tabernacle.
Kila fremu itakuwa na ndimi mbili, zenye kuunganishwa huu na huu. Ndivyo utakavyozifanya mbao zote za maskani.
18 You shall make twenty boards for the tabernacle, for the south side southward.
Kisha ufanye zile mbao za maskani, mbao ishirini kwa upande wa kusini kuelekea kusini.
19 You shall make forty sockets of silver under the twenty boards; two sockets under one board for its two tenons, and two sockets under another board for its two tenons.
Lazima nawe ufanye vitako arubaini vya fedha chini ya zile fremu ishirini. Vitako viwili chini ya fremu moja, kupokea zile ndimi zake mbili, na vitako viwili chini ya fremu nyingine kupokea zile ndimi zake mbili.
20 For the second side of the tabernacle, on the north side, twenty boards,
Kwa upande wa pili wa maskani, upande wa kaskazini, mbao ishirini
21 and their forty sockets of silver; two sockets under one board, and two sockets under another board.
na vitako vyake vya fedha arubaini. Lazima kuwe na vitako viwili chini ya fremu moja, na vitako viwili chini ya fremu nyingine.
22 For the far side of the tabernacle westward you shall make six boards.
Ufanye fremu sita kwa ajili ya upande wa nyuma wa maskani kuelekea magharibi.
23 You shall make two boards for the corners of the tabernacle in the far side.
Tena ufanye fremu mbili kwa ajili ya hizo pembe za maskani zilizo upande wa nyuma.
24 They shall be double beneath, and in the same way they shall be whole to its top to one ring: thus shall it be for them both; they shall be for the two corners.
Hizi fremu zitakuwa zimetengana upande wa chini, lakini zimeshinkana kwa juu ya duara moja.
25 There shall be eight boards, and their sockets of silver, sixteen sockets; two sockets under one board, and two sockets under another board.
Fremu zitakuwa ni nane, na vitako vyake vya fedha. Vitako kumi na sita, vitako viwili chini ya fremu moja, na vitako viwili chini ya ubao wa pili.
26 “You shall make bars of acacia wood: five for the boards of the one side of the tabernacle,
Lazima ufanye mataruma ya mti wa mshita- mataruma matano kwa ajili ya mbao za upande mmoja wa maskani,
27 and five bars for the boards of the other side of the tabernacle, and five bars for the boards of the side of the tabernacle, for the far side westward.
na mataruma matano kwa ajili ya fremu za upande wa pili wa maskani, na mataruma matano kwa ajili ya fremu za upande wa maskani ulio nyuma kuelekea magharibi.
28 The middle bar in the middle of the boards shall pass through from end to end.
Na hilo taruma la katikati lililo katikati ya zile fremu, litapenya toka mwisho huu hata mwisho huu.
29 You shall overlay the boards with gold, and make their rings of gold for places for the bars. You shall overlay the bars with gold.
lazima uzifunuke hizo fremu kwa dhahabu. Nawe lazima ufanye maduara yake ya za dhahabu, kuwa kama vishikizo, na hayo mataruma utayafunika dhahabu.
30 You shall set up the tabernacle according to the way that it was shown to you on the mountain.
Nawe utaisimamisha hiyo maskani sawasawa na mfano wake uliooneshwa mlimani.
31 “You shall make a veil of blue, and purple, and scarlet, and fine twined linen, with cherubim. It shall be the work of a skillful workman.
Nawe fanya pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na nguo za kitani nzuri zenye kusokotwa, litafumwa na kutiwa makerubi, kazi ya fundi stadi.
32 You shall hang it on four pillars of acacia overlaid with gold; their hooks shall be of gold, on four sockets of silver.
Kisha litungike katika nguzo nne za mti wa mshita zilizofunikwa dhahabu, vifungo vyake vitakuwa vya dhahabu, katika vitako vya fedha vinne.
33 You shall hang up the veil under the clasps, and shall bring the ark of the covenant in there within the veil. The veil shall separate the holy place from the most holy for you.
Nawe tungika lile pazia chini ya vile vifungo, nawe lete lile sanduku la ushuhuda. Lile pazia litawagawanyia kati ya patakatifu, na mahali patakatifu sana.
34 You shall put the mercy seat on the ark of the covenant in the most holy place.
Nawe lazima utaweka kiti cha rehema juu ya lile sanduku la ushuhuda ndani ya mahali pale patakatifu sana. Na ile meza utaiweka nje ya pazia.
35 You shall set the table outside the veil, and the lamp stand opposite the table on the side of the tabernacle toward the south. You shall put the table on the north side.
Lazima uweke kinara cha taa kuikabili ile meza upande wa maskani wa kuelekea kusini. Lile meza utaiweka upande wa kaskazini.
36 “You shall make a screen for the door of the Tent, of blue, and purple, and scarlet, and fine twined linen, the work of the embroiderer.
Kisha utafanya kisitiri kwa mlango wa hema, cha nyuzi za rangi ya buluu, zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa, kazi ya mshonaji wa taraza.
37 You shall make for the screen five pillars of acacia, and overlay them with gold. Their hooks shall be of gold. You shall cast five sockets of bronze for them.
Nawe fanya nguzo tano za mti wa mshita kwa kile kisitiri, na kuzifunika dhahabu; kulabu zake zitakuwa za dhahabu. Nawe utasubu vitako vya shaba vitano kwa ajili yake.

< Exodus 26 >