< Job 39 >

1 “Do you know the time when the mountain goats give birth? Do you watch when the doe bears fawns?
Je unajua ni wakati gani mbuzi mwitu huzaa watoto wao katika miamba? Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao?
2 Can you count the months that they fulfill? Or do you know the time when they give birth?
Waweza kuhesabu miezi ya kuchukua mimba? Je unaujua muda ambao huzaa watoto wao?
3 They bow themselves. They bear their young. They end their labor pains.
Wanainama chini na kuzaa watoto wao, na kisha maumivu yao ya uzazi yanaishi.
4 Their young ones become strong. They grow up in the open field. They go out, and do not return again.
Watoto wao huwa na nguvu na kukua katika uwanda wa wazi; hutoka nje na hawarudi tena.
5 “Who has set the wild donkey free? Or who has loosened the bonds of the swift donkey,
Ni nani huwaacha punda mwitu waende huru? Je nani amevilegeza vifungo vya punda wepesi,
6 whose home I have made the wilderness, and the salt land his dwelling place?
ni nyumba ya nani nimeifanya katika Araba, au nyumba yake katika nchi ya chumvi?
7 He scorns the tumult of the city, neither does he hear the shouting of the driver.
Hucheka kwa dharau katika kelele katika mji; hasikilizi kelele za mwongozaji.
8 The range of the mountains is his pasture. He searches after every green thing.
Hutembeatembea juu ya milima kama malisho yake; huko hutafuta kila mmea ulio wa kijani kwa ajili ya kula.
9 “Will the wild ox be content to serve you? Or will he stay by your feeding trough?
Je nyati atakuwa na furaha kukutumikia? Je atakubali kukaa katika zizi lako?
10 Can you hold the wild ox in the furrow with his harness? Or will he till the valleys after you?
Waweza kumwongoza nyati kulima mtaro kwa kamba? Je atachimba bonde kwa ajili yako?
11 Will you trust him, because his strength is great? Or will you leave to him your labor?
Je waweza kumtumaini kwasababu ya nguvu zake nyingi? Je waweza kumwachia kazi yako ili aifanye?
12 Will you confide in him, that he will bring home your seed, and gather the grain of your threshing floor?
Je waweza kumtegemea akuletee nyumbani nafaka, au kukusanya nafaka katika uwanda wako wa kupuria?
13 “The wings of the ostrich wave proudly, but are they the feathers and plumage of love?
Mabawa ya mbuni hupunga kwa majivuno, bali je mabawa na manyoya yana upendo?
14 For she leaves her eggs on the earth, warms them in the dust,
Kwa maana huuacha mayai yake katika nchi, na huyaacha yapate joto katika mavumbi;
15 and forgets that the foot may crush them, or that the wild animal may trample them.
husahau kuwa mguu waweza kuyaharibu au kwamba mnyama mwitu aweza kuyakanyaga.
16 She deals harshly with her young ones, as if they were not hers. Though her labor is in vain, she is without fear,
Huyatendea vibaya makinda yake kana kwamba si yake; haogopi kwamba kazi yake yaweza kupotea bure,
17 because God has deprived her of wisdom, neither has he imparted to her understanding.
kwasababu Mungu amemnyima hekima na hajampa ufahamu wowote.
18 When she lifts up herself on high, she scorns the horse and his rider.
Na wakati anapokimbia kwa haraka, huwacheka kwa dharau farasi na mpanda farasi wake.
19 “Have you given the horse might? Have you clothed his neck with a quivering mane?
Je umempa farasi nguvu zake? Je umeivika shingo yake kwa manyoya?
20 Have you made him to leap as a locust? The glory of his snorting is awesome.
Je umemfanya aruke kama panzi? Enzi ya mlio wake ni wa kutisha.
21 He paws in the valley, and rejoices in his strength. He goes out to meet the armed men.
Hurarua kwa nguvu na kufurahia katika nguvu zake; hukimbia upesi kukutana na silaha.
22 He mocks at fear, and is not dismayed, neither does he turn back from the sword.
Huidharau hofu na hashangazwi; huwa harudi nyuma kutoka katika upanga.
23 The quiver rattles against him, the flashing spear and the javelin.
Podo hugongagonga ubavuni mwake, pamoja na mkuki unaong'aa na fumo.
24 He eats up the ground with fierceness and rage, neither does he stand still at the sound of the trumpet.
Huimeza nchi kwa hasira na ghadhabu; katika sauti ya tarumbeta, hawezi kusimama sehemu moja.
25 As often as the trumpet sounds he snorts, ‘Aha!’ He smells the battle afar off, the thunder of the captains, and the shouting.
Wakati wowote tarumbeta inapolia, husema, 'Ooh! Huisikia harufu ya vita kutoka mbali - vishindo vya radi za makamanda na makelele.
26 “Is it by your wisdom that the hawk soars, and stretches her wings toward the south?
Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa juu, na ya kuwa huyanyosha mabawa yake kwa upande wa kusini?
27 Is it at your command that the eagle mounts up, and makes his nest on high?
Je ni kwa agizo lako kwamba tai huruka juu na kufanya kiota chake katika sehemu za juu?
28 On the cliff he dwells and makes his home, on the point of the cliff and the stronghold.
Huishi katika majabali na hufanya makao yake katika vilele vya majabali, na ngomeni.
29 From there he spies out the prey. His eyes see it afar off.
Kutoka huko hutafuta mawindo; macho yake huyaona mawindo kutoka mbali.
30 His young ones also suck up blood. Where the slain are, there he is.”
Makinda yake hunywa damu pia; na pale walipo watu wafu, ndipo na yeye alipo.

< Job 39 >