< Proverbs 9 >

1 Wisdom has built her house. She has carved out her seven pillars.
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo saba kutoka katika miamba.
2 She has prepared her meat. She has mixed her wine. She has also set her table.
Ameandaa wanyama wake kwa chakula cha usiku; ameichanganya divai yake; na kuandaa meza yake.
3 She has sent out her maidens. She cries from the highest places of the city:
Amewatuma watumishi wake kupeleka mialiko na kutoka mahali pa juu sana kwenye mji anaita:
4 “Whoever is simple, let him turn in here!” As for him who is void of understanding, she says to him,
“Wale wasiofunzwa waje hapa!” anawaambia wale wasionaufahamu.
5 “Come, eat some of my bread, Drink some of the wine which I have mixed!
Njoo, ule chakula, na unywe divai nimeshaichanganya.
6 Leave your simple ways, and live. Walk in the way of understanding.”
Acheni njia zenu za kijinga, na mkaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 One who corrects a mocker invites insult. One who reproves a wicked man invites abuse.
Yeyote amrekebishaye mwenye dhihaka hukaribisha matusi na yeyote anayemshutumu mtu mbaya atapata madhara.
8 Do not reprove a scoffer, lest he hate you. Reprove a wise person, and he will love you.
Usimshutumu mwenye dhihaka, ama atakuchukia; mshutumu mtu mwenye busara, naye atakupenda.
9 Instruct a wise person, and he will be still wiser. Teach a righteous person, and he will increase in learning.
Mpe mafundisho mtu mwenye busara, naye atakuwa na busara zaidi; mfundishe mtu mwenye haki, naye ataongeza elimu.
10 The fear of the LORD is the beginning of wisdom. The knowledge of the Holy One is understanding.
Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
11 For by me your days will be multiplied. The years of your life will be increased.
Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
12 If you are wise, you are wise for yourself. If you mock, you alone will bear it.
Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
13 The foolish woman is loud, undisciplined, and knows nothing.
Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
14 She sits at the door of her house, on a seat in the high places of the city,
Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
15 to call to those who pass by, who go straight on their ways,
Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
16 “Whoever is simple, let him turn in here.” As for him who is void of understanding, she says to him,
Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili. “
17 “Stolen water is sweet. Food eaten in secret is pleasant.”
Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
18 But he does not know that the departed spirits are there, that her guests are in the depths of Sheol (Sheol h7585).
Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu. (Sheol h7585)

< Proverbs 9 >