< Psalms 17 >

1 A Prayer by David. Hear, LORD, my righteous plea. Give ear to my prayer that does not go out of deceitful lips.
Maombi ya Daudi. Sikia ombi langu kwa ajili ya haki, Yawhe; uusikilize mwito wangu wa msaada. Uyasikilize maombi yangu yatokayo katika midomo isiyo na udanganyifu.
2 Let my sentence come out of your presence. Let your eyes look on equity.
Uthibitisho wangu na uje kutoka uweponi mwako; macho yako na yaone kile kilicho sahihi!
3 You have proved my heart. You have visited me in the night. You have tried me, and found nothing. I have resolved that my mouth shall not disobey.
Kama utaujaribu moyo wangu, kama utakuja kwangu wakati wa usiku, wewe utanitakasa na hautapata mipango yeyote ya uovu; mdomo wangu hautavunja sheria.
4 As for the deeds of men, by the word of your lips, I have kept myself from the ways of the violent.
Kama kwa matendo ya binadamu, ni katika neno la midomo yako ya kuwa nimejiepusha na njia za wahalifu.
5 My steps have held fast to your paths. My feet have not slipped.
Mwenendo wangu umeshikila kwa umakini mwenendo wako; miguu yangu haija teleza.
6 I have called on you, for you will answer me, God. Turn your ear to me. Hear my speech.
Nakuita wewe, kwa kuwa unanijibu, Mungu; geizia sikio lako kwangu na usikilize ninapo ongea.
7 Show your marvelous loving kindness, you who save those who take refuge by your right hand from their enemies.
Onyesha uaminifu wa agano lako katika namna ya ajabu, wewe uokoaye kwa mkono wa haki yako wale wanao kukimbilia wewe kutoka kwa adui zao.
8 Keep me as the apple of your eye. Hide me under the shadow of your wings,
Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche katika kivuli cha mbawa zako
9 from the wicked who oppress me, my deadly enemies, who surround me.
kutoka katika uwepo wa waovu ambao wananitusi, adui zangu wanizungukao.
10 They close up their callous hearts. With their mouth they speak proudly.
Wao hawana huruma kwa yeyote; midomo yao huongea kwa majivuno.
11 They have now surrounded us in our steps. They set their eyes to cast us down to the earth.
Wao wame zizunguka hatua zangu. Wamekaza macho yao wanishambulie mpaka ardhini.
12 He is like a lion that is greedy of his prey, as it were a young lion lurking in secret places.
Wao ni kama mfano wa hasira ya simba mawindoni. Ni kama simba kijana anapotokea mafichoni.
13 Arise, LORD, confront him. Cast him down. Deliver my soul from the wicked by your sword,
Inuka, Yahwe! Uwashambulie! Uwaangushe chini kwenye nyuso zao! Uyaokoe maisha yangu kutokana na waovu kwa upanga wako!
14 from men by your hand, LORD, from men of the world, whose portion is in this life. You fill the belly of your cherished ones. Your sons have plenty, and they store up wealth for their children.
Uniokoe kutoka kwa watu hawa kwa mkono wako, Yahwe, kutoka kwa watu wa dunia hii ambao utajiri wao ni maisha haya pekee! Wewe utayajaza matumbo ya wale uwathaminio na utajiri; watakuwa na watoto wengi na wataacha utajiri wao kwa watoto wao.
15 As for me, I shall see your face in righteousness. I shall be satisfied, when I awake, with seeing your form.
Bali mimi, nitauona uso wako katika haki; Nitashuhudiwa, pale nitakapo amka, na macho yako.

< Psalms 17 >