< Psalms 28 >

1 By David. To you, LORD, I call. My rock, do not be deaf to me, lest, if you are silent to me, I would become like those who go down into the pit.
Yahwe, ninalia; mwamba wangu, usinipuuze. Ikiwa haunijibu, nitaungana na wale waendao chini kaburini.
2 Hear the voice of my petitions, when I cry to you, when I lift up my hands toward your Most Holy Place.
Sikia kilio cha kusihi kwangu pale niitapo msaada kutoka kwako, niinuapo mikono yangu mbele ya mahali patakatifu zaidi!
3 Do not draw me away with the wicked, with the workers of iniquity who speak peace with their neighbors, but mischief is in their hearts.
Usiniburute pamoja na waovu, wale wafanyao uovu, waongeao amani na majirani zao lakini mioyoni mwao mna uovu.
4 Give them according to their work, and according to the wickedness of their doings. Give them according to the operation of their hands. Bring back on them what they deserve.
Uwape kulingana na sitahili ya matendo yao na uwalipe kulingana na madai ya maovu yao, uwalipe kwa ajili ya kazi ya mikono yao na uwape kile wanachostahili.
5 Because they do not respect the works of the LORD, nor the operation of his hands, he will break them down and not build them up.
Kwa sababu hawayaelewi matendo ya Yahwe wala kazi ya mikono yake, atawakanyaga kanyaga chini na hata wajenga tena wao.
6 Blessed be the LORD, because he has heard the voice of my petitions.
Abarikiwe Yahwe kwa sababu yeye amesikia sauti ya kusihi kwangu!
7 The LORD is my strength and my shield. My heart has trusted in him, and I am helped. Therefore my heart greatly rejoices. With my song I will thank him.
Yahwe ni nguvu yangu na ngao yangu; moyo wangu wa humwamini yeye, na ninasaidiwa. Kwa hiyo moyo wangu hufurahia sana, nami nitamsifu yeye kwa kuimba.
8 The LORD is their strength. He is a stronghold of salvation to his anointed.
Yahwe ni nguvu ya watu wake, naye ni mkombozi salama wa wapakwa mafuta wake.
9 Save your people, and bless your inheritance. Be their shepherd also, and bear them up forever.
Uwaokoe watu wako na uwabariki warithi wako. Uwe mchungaji wao na uwabebe milele.

< Psalms 28 >