< John 7 >

1 And after these things Jesus walked in Galilee: for he would not walk in Judæa, because the Jews sought to kill him.
Baada ya hayo, Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea mkoani Yudea kwa sababu viongozi wa Wayahudi walikuwa wanataka kumwua.
2 Now the feast of the Jews, the feast of tabernacles, was at hand.
Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
3 His brethren therefore said unto him, Depart hence, and go into Judæa, that thy disciples also may behold thy works which thou doest.
Basi ndugu zake wakamwambia, “Ondoka hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wazione kazi unazozifanya.
4 For no man doeth anything in secret, and himself seeketh to be known openly. If thou doest these things, manifest thyself to the world.
Mtu hafanyi mambo kwa siri kama anataka kujulikana kwa watu. Maadam unafanya mambo haya, basi, jidhihirishe kwa ulimwengu.”
5 For even his brethren did not believe on him.
(Hata ndugu zake hawakumwamini!)
6 Jesus therefore saith unto them, My time is not yet come; but your time is always ready.
Basi, Yesu akawaambia, “Wakati wangu ufaao haujafika bado. Lakini kwenu ninyi kila wakati unafaa.
7 The world cannot hate you; but me it hateth, because I testify of it, that its works are evil.
Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini mimi wanichukia kwa sababu mimi nauambia wazi kwamba matendo yake ni maovu.
8 Go ye up unto the feast: I go not up unto this feast; because my time is not yet fulfilled.
Ninyi nendeni kwenye sikukuu hiyo. Mimi siendi kwenye sikukuu hiyo, maana saa yangu ifaayo haijafika.”
9 And having said these things unto them, he abode [still] in Galilee.
Alisema hayo kisha akabaki huko Galilaya.
10 But when his brethren were gone up unto the feast, then went he also up, not publicly, but as it were in secret.
Baada ya ndugu zake kwenda kwenye sikukuu, Yesu naye alikwenda, lakini hakuenda kwa hadhara bali kwa siri.
11 The Jews therefore sought him at the feast, and said, Where is he?
Viongozi wa Wayahudi walikuwa wanamtafuta kwenye sikukuu hiyo; Wakauliza: “Yuko wapi?”
12 And there was much murmuring among the multitudes concerning him: some said, He is a good man; others said, Not so, but he leadeth the multitude astray.
Kulikuwa na minong'ono mingi katika umati wa watu. Baadhi yao walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “La! Anawapotosha watu.”
13 Yet no man spake openly of him for fear of the Jews.
Hata hivyo hakuna mtu aliyethubutu kusema, habari zake hadharani kwa kuwaogopa viongozi wa Wayahudi.
14 But when it was now the midst of the feast Jesus went up into the temple, and taught.
Sikukuu hiyo ilipofikia katikati, Yesu naye alikwenda Hekaluni, akaanza kufundisha.
15 The Jews therefore marvelled, saying, How knoweth this man letters, having never learned?
Basi, Wayahudi wakashangaa na kusema “Mtu huyu amepataje elimu naye hakusoma shuleni?”
16 Jesus therefore answered them, and said, My teaching is not mine, but his that sent me.
Hapo Yesu akawajibu, “Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
17 If any man willeth to do his will, he shall know of the teaching, whether it is of God, or [whether] I speak from myself.
Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe.
18 He that speaketh from himself seeketh his own glory: but he that seeketh the glory of him that sent him, the same is true, and no unrighteousness is in him.
Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
19 Did not Moses give you the law, and [yet] none of you doeth the law? Why seek ye to kill me?
Je, Mose hakuwapeni Sheria? Hata hivyo, hakuna hata mmoja wenu anayeishika Sheria. Kwa nini mnataka kuniua?”
20 The multitude answered, Thou hast a demon: who seeketh to kill thee?
Hapo watu wakamjibu, “Una wazimu wewe! Nani anataka kukuua?”
21 Jesus answered and said unto them, I did one work, and ye all marvel because thereof.
Yesu akawajibu, “Kuna jambo moja nililofanya, nanyi mnalistaajabia.
22 Moses hath given you circumcision (not that it is of Moses, but of the fathers); and on the sabbath ye circumcise a man.
Mose aliwapeni ile desturi ya kutahiri. (Si kwamba desturi hiyo ilitoka kwa Mose, bali ilitoka kwa mababu). Sasa ninyi humtahiri mtu hata siku ya Sabato.
23 If a man receiveth circumcision on the sabbath, that the law of Moses may not be broken; are ye wroth with me, because I made a man every whit whole on the sabbath?
Ikiwa basi, mtu hutahiriwa hata siku ya Sabato kusudi Sheria ya Mose isivunjwe, mbona mnanikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya Sabato?
24 Judge not according to appearance, but judge righteous judgment.
Msihukumu mambo kwa nje tu; toeni hukumu ya haki.”
25 Some therefore of them of Jerusalem said, Is not this he whom they seek to kill?
Baadhi ya watu wa Yerusalemu walisema, “Je, yule mtu wanayemtafuta wamuue si huyu?
26 And lo, he speaketh openly, and they say nothing unto him. Can it be that the rulers indeed know that this is the Christ?
Tazameni sasa! Anawaonya hadharani, wala hakuna mtu anayemwambia hata neno. Je, yawezekana kuwa viongozi wametambua kweli kwamba huyu ndiye Kristo?
27 Howbeit we know this man whence he is: but when the Christ cometh, no one knoweth whence he is.
Kristo atakapokuja hakuna mtu atakayejua mahali alikotoka, lakini sisi tunajua alikotoka mtu huyu!”
28 Jesus therefore cried in the temple, teaching and saying, Ye both know me, and know whence I am; and I am not come of myself, but he that sent me is true, whom ye know not.
Basi, Yesu alipokuwa anafundisha Hekaluni alipaaza sauti na kusema, “Ati mnanijua; hata nilikotoka mnakujua! Hata hivyo, sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe; ila yeye aliyenituma mimi ni wa kweli, nanyi hamumjui.
29 I know him; because I am from him, and he sent me.
Lakini mimi namjua kwa sababu nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma.”
30 They sought therefore to take him: and no man laid his hand on him, because his hour was not yet come.
Basi, watu wakataka kumtia nguvuni, lakini hakuna mtu aliyethubutu kumkamata kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
31 But of the multitude many believed on him; and they said, When the Christ shall come, will he do more signs than those which this man hath done?
Wengi katika ule umati wa watu walimwamini, wakasema, “Je, Kristo akija atafanya ishara kubwa zaidi kuliko alizozifanya huyu?”
32 The Pharisees heard the multitude murmuring these things concerning him; and the chief priests and the Pharisees sent officers to take him.
Mafarisayo waliwasikia watu wakinong'ona maneno hayo juu ya Yesu. Basi, wao pamoja na makuhani wakuu wakawatuma walinzi wamtie nguvuni.
33 Jesus therefore said, Yet a little while am I with you, and I go unto him that sent me.
Yesu akasema, “Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma.
34 Ye shall seek me, and shall not find me: and where I am, ye cannot come.
Mtanitafuta lakini hamtaniona, maana pale nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika.”
35 The Jews therefore said among themselves, Whither will this man go that we shall not find him? will he go unto the Dispersion among the Greeks, and teach the Greeks?
Viongozi wa Wayahudi wakasema wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi ambapo hatutaweza kumpata? Atakwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki, na kuwafundisha Wagiriki?
36 What is this word that he said, Ye shall seek me, and shall not find me; and where I am, ye cannot come?
Ana maana gani anaposema: Mtanitafuta lakini hamtanipata, na mahali nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika?”
37 Now on the last day, the great [day] of the feast, Jesus stood and cried, saying, If any man thirst, let him come unto me and drink.
Siku ya mwisho ya sikukuu hiyo ilikuwa siku maalum. Yesu alisimama, akasema kwa sauti kubwa, “Aliye na kiu na aje kwangu anywe.
38 He that believeth on me, as the scripture hath said, from within him shall flow rivers of living water.
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: Anayeniamini mimi, mito ya maji yenye uzima itatiririka kutoka moyoni mwake!”
39 But this spake he of the Spirit, which they that believed on him were to receive: for the Spirit was not yet [given]; because Jesus was not yet glorified.
(Alisema hayo kumhusu Roho ambaye wale waliomwamini yeye watampokea. Wakati huo Roho alikuwa hajafika kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.)
40 [Some] of the multitude therefore, when they heard these words, said, This is of a truth the prophet.
Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, “Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!”
41 Others said, This is the Christ. But some said, What, doth the Christ come out of Galilee?
Wengine wakasema, “Huyu ndiye Kristo!” Lakini wengine walisema, “Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya?
42 Hath not the scripture said that the Christ cometh of the seed of David, and from Bethlehem, the village where David was?
Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!”
43 So there arose a division in the multitude because of him.
Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu.
44 And some of them would have taken him; but no man laid hands on him.
Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata.
45 The officers therefore came to the chief priests and Pharisees; and they said unto them, Why did ye not bring him?
Kisha wale walinzi wakarudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo; nao wakawauliza, “Kwa nini hamkumleta?”
46 The officers answered, Never man so spake.
Walinzi wakawajibu, “Hakuna mtu aliyepata kamwe kusema kama asemavyo mtu huyu!”
47 The Pharisees therefore answered them, Are ye also led astray?
Mafarisayo wakawauliza, “Je, nanyi pia mmedanganyika?
48 Hath any of the rulers believed on him, or of the Pharisees?
Je, mmekwisha mwona hata mmoja wa viongozi wa watu, au mmoja wa Mafarisayo aliyemwamini?
49 But this multitude that knoweth not the law are accursed.
Lakini umati huu haujui Sheria ya Mose; umelaaniwa!”
50 Nicodemus saith unto them (he that came to him before, being one of them),
Mmoja wao alikuwa Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu. Basi, yeye akawaambia,
51 Doth our law judge a man, except it first hear from himself and know what he doeth?
“Je, Sheria yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza na kujua anafanya nini?”
52 They answered and said unto him, Art thou also of Galilee? Search, and see that out of Galilee ariseth no prophet.
Nao wakamjibu, “Je, wewe pia umetoka Galilaya? Haya, kayachunguze Maandiko Matakatifu nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki kamwe nabii!”
53 [And they went every man unto his own house:
Basi, wote wakaondoka, kila mtu akaenda zake;

< John 7 >