< Luke 20 >

1 And it came to pass, on one of the days, as he was teaching the people in the temple, and preaching the gospel, there came upon him the chief priests and the scribes with the elders;
Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
2 and they spake, saying unto him, Tell us: By what authority doest thou these things? or who is he that gave thee this authority?
wakasema, “Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?”
3 And he answered and said unto them, I also will ask you a question; and tell me:
Yesu akawaambia, “Na mimi nitawaulizeni swali:
4 The baptism of John, was it from heaven, or from men?
mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?”
5 And they reasoned with themselves, saying, If we shall say, From heaven; he will say, Why did ye not believe him?
Lakini wao wakajadiliana hivi: “Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
6 But if we shall say, From men; all the people will stone us: for they are persuaded that John was a prophet.
Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii.”
7 And they answered, that they knew not whence [it was].
Basi, wakamwambia, “Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi.”
8 And Jesus said unto them, Neither tell I you by what authority I do these things.
Yesu akawaambia, “Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”
9 And he began to speak unto the people this parable: A man planted a vineyard, and let it out to husbandmen, and went into another country for a long time.
Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
10 And at the season he sent unto the husbandmen a servant, that they should give him of the fruit of the vineyard: but the husbandmen beat him, and sent him away empty.
Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
11 And he sent yet another servant: and him also they beat, and handled him shamefully, and sent him away empty.
Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
12 And he sent yet a third: and him also they wounded, and cast him forth.
Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
13 And the lord of the vineyard said, What shall I do? I will send my beloved son; it may be they will reverence him.
Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
14 But when the husbandmen saw him, they reasoned one with another, saying, This is the heir; let us kill him, that the inheritance may be ours.
Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
15 And they cast him forth out of the vineyard, and killed him. What therefore will the lord of the vineyard do unto them?
Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua.” Yesu akauliza, “Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
16 He will come and destroy these husbandmen, and will give the vineyard unto others. And when they heard it, they said, God forbid.
Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia maneno hayo, walisema: “Hasha! Yasitukie hata kidogo!”
17 But he looked upon them, and said, What then is this that is written, The stone which the builders rejected, The same was made the head of the corner?
Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, “Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
18 Every one that falleth on that stone shall be broken to pieces; but on whomsoever it shall fall, it will scatter him as dust.
Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa.”
19 And the scribes and the chief priests sought to lay hands on him in that very hour; and they feared the people: for they perceived that he spake this parable against them.
Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
20 And they watched him, and sent forth spies, who feigned themselves to be righteous, that they might take hold of his speech, so as to deliver him up to the rule and to the authority of the governor.
Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
21 And they asked him, saying, Teacher, we know that thou sayest and teachest rightly, and acceptest not the person [of any], but of a truth teachest the way of God:
Hao wapelelezi wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
22 Is it lawful for us to give tribute unto Cæsar, or not?
Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!”
23 But he perceived their craftiness, and said unto them,
Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
24 Show me a denarius. Whose image and superscription hath it? And they said, Cæsar’s.
“Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?”
25 And he said unto them, Then render unto Cæsar the things that are Cæsar’s, and unto God the things that are God’s.
Nao wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Yesu akawaambia, “Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu.”
26 And they were not able to take hold of the saying before the people: and they marvelled at his answer, and held their peace.
Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
27 And there came to him certain of the Sadducees, they that say that there is no resurrection;
Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
28 and they asked him, saying, Teacher, Moses wrote unto us, that if a man’s brother die, having a wife, and he be childless, his brother should take the wife, and raise up seed unto his brother.
“Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
29 There were therefore seven brethren: and the first took a wife, and died childless;
Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
30 and the second:
Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
31 and the third took her; and likewise the seven also left no children, and died.
na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba—wote walikufa bila kuacha watoto.
32 Afterward the woman also died.
Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
33 In the resurrection therefore whose wife of them shall she be? for the seven had her to wife.
Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba.”
34 And Jesus said unto them, The sons of this world marry, and are given in marriage: (aiōn g165)
Yesu akawaambia, “Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa; (aiōn g165)
35 but they that are accounted worthy to attain to that world, and the resurrection from the dead, neither marry, nor are given in marriage: (aiōn g165)
lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa. (aiōn g165)
36 for neither can they die any more: for they are equal unto the angels; and are sons of God, being sons of the resurrection.
Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
37 But that the dead are raised, even Moses showed, in [the place concerning] the Bush, when he calleth the Lord the God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Jacob.
Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
38 Now he is not the God of the dead, but of the living: for all live unto him.
Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye.”
39 And certain of the scribes answering said, Teacher, thou hast well said.
Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, “Mwalimu, umejibu vema kabisa.”
40 For they durst not any more ask him any question.
Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
41 And he said unto them, How say they that the Christ is David’s son?
Yesu akawauliza, “Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
42 For David himself saith in the book of Psalms, The Lord said unto my Lord, Sit thou on my right hand,
Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
43 Till I make thine enemies the footstool of thy feet.
mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
44 David therefore calleth him Lord, and how is he his son?
Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?”
45 And in the hearing of all the people he said unto his disciples,
Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
46 Beware of the scribes, who desire to walk in long robes, and love salutations in the marketplaces, and chief seats in the synagogues, and chief places at feasts;
“Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
47 who devour widows’ houses, and for a pretence make long prayers: these shall receive greater condemnation.
Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!”

< Luke 20 >