< 2 Kings 1 >

1 After the death of Ahab, Moab made itself free from the authority of Israel.
Baada ya kifo cha Mfalme Ahabu, nchi ya Moabu iliasi dhidi ya Israeli.
2 Now Ahaziah had a fall from the window of his room in Samaria, and was ill. And he sent men, and said to them, Put a question to Baal-zebub, the god of Ekron, about the outcome of my disease, to see if I will get well or not.
Basi Ahazia alikuwa ameanguka huko Samaria kutoka baraza ya chumba chake cha juu, akaumia. Hivyo akatuma wajumbe, akiwaambia, “Nendeni mkaulize kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni, mkaone kama nitapona kutokana na kuumia huku.”
3 But the angel of the Lord said to Elijah the Tishbite, Go now, and, meeting the men sent by the king of Samaria, say to them, Is it because there is no God in Israel, that you are going to get directions from Baal-zebub, the god of Ekron?
Lakini malaika wa Bwana akamwambia Eliya, Mtishbi, “Panda ukakutane na wajumbe wa mfalme wa Samaria, uwaulize, ‘Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana mnakwenda kumuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni?’
4 Give ear then to the words of the Lord: You will never again get down from the bed on to which you have gone up, but death will certainly come to you. Then Elijah went away.
Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana, ‘Hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!’” Hivyo Eliya akaenda.
5 And the men he had sent came back to the king; and he said to them, Why have you come back?
Wajumbe waliporudi kwa mfalme, akawauliza, “Kwa nini mmerudi?”
6 And they said to him, On our way we had a meeting with a man who said, Go back to the king who sent you and say to him, The Lord says, Is it because there is no God in Israel that you send to put a question to Baal-zebub, the god of Ekron? For this reason, you will not come down from the bed on to which you have gone up, but death will certainly come to you.
Wakamjibu, “Mtu fulani alikuja kukutana nasi, naye akatuambia, ‘Rudini kwa mfalme aliyewatuma na mkamwambie, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana unawatuma watu kwenda kuuliza kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa hiyo hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”’”
7 And he said to them, What sort of a man was it who came and said these words to you?
Mfalme akawauliza, “Alikuwa mtu wa namna gani ambaye mlikutana naye, akawaambia hili?”
8 And they said in answer, He was a man clothed in a coat of hair, with a leather band about his body. Then he said, It is Elijah the Tishbite.
Wakamjibu, “Alikuwa mtu aliyekuwa na vazi la manyoya na mkanda wa ngozi kiunoni mwake.” Mfalme akasema, “Huyo alikuwa ni Eliya, Mtishbi.”
9 Then the king sent to him a captain of fifty with his fifty men; and he went up to him where he was seated on the top of a hill, and said to him, O man of God, the king has said, Come down.
Ndipo mfalme akamtuma mkuu mmoja wa kikosi pamoja na kikosi chake cha askari hamsini kwa nabii Eliya. Yule mkuu wa kikosi akamwendea Eliya, aliyekuwa ameketi juu ya kilima, na kumwambia, “Mtu wa Mungu, mfalme anasema, ‘Shuka chini!’”
10 And Elijah in answer said to the captain of fifty, If I am a man of God, may fire come down from heaven on you and on your fifty men, and put an end to you. Then fire came down from heaven and put an end to him and his fifty men.
Eliya akamjibu yule mkuu wa kikosi, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza yule mkuu wa kikosi pamoja na watu wake.
11 Then the king sent another captain of fifty with his fifty men; and he said to Elijah, O man of God, the king says, Come down quickly.
Aliposikia hili, mfalme akatuma kwa Eliya mkuu wa kikosi mwingine na askari wake hamsini. Yule mkuu wa kikosi akamwambia Eliya, “Mtu wa Mungu, hili ndilo asemalo mfalme, ‘Shuka chini mara moja!’”
12 And Elijah in answer said, If I am a man of God, may fire come down from heaven on you and on your fifty men, and put an end to you. And the fire of God came down from heaven, and put an end to him and his fifty men.
Eliya akajibu, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza yeye na watu wake hamsini.
13 Then he sent a third captain of fifty with his fifty men; and the third captain of fifty went up, and falling on his knees before Elijah, requesting mercy of him, said, O man of God, let my life and the life of these your fifty servants be of value to you.
Hivyo mfalme akatuma mkuu wa kikosi wa tatu na watu wake hamsini. Huyu mkuu wa kikosi wa tatu akapanda na kupiga magoti mbele ya Eliya, akiomba, “Mtu wa Mungu, tafadhali niachie uhai wangu na uhai wa hawa watu hamsini, watumishi wako!
14 For fire came down from heaven and put an end to the first two captains of fifty and their fifties; but now let my life be of value in your eyes.
Tazama, moto umeshuka kutoka mbinguni na kuwateketeza wale wakuu wa vikosi viwili vya kwanza pamoja na watu wao. Lakini sasa niachie uhai wangu!”
15 Then the angel of the Lord said to Elijah, Go down with him; have no fear of him. So he got up and went down with him to the king.
Malaika wa Bwana akamwambia Eliya, “Shuka pamoja naye, usimwogope.” Hivyo Eliya akainuka na kushuka pamoja naye kwa mfalme.
16 And he said to him, This is the word of the Lord: Because you sent men to put a question to Baal-zebub, the god of Ekron, for this reason you will never again get down from the bed on to which you have gone up, but death will certainly come to you.
Akamwambia mfalme, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli wa kumuuliza habari, ndiyo maana ukatuma wajumbe kuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa sababu umefanya hili, kamwe hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”
17 So death came to him, as the Lord had said by the mouth of Elijah. And Jehoram became king in his place in the second year of the rule of Jehoram, son of Jehoshaphat, king of Judah; because he had no son.
Hivyo akafa, sawasawa na lile neno la Bwana ambalo Eliya alikuwa amesema. Kwa kuwa Ahazia hakuwa na mwana, Yoramu akawa mfalme baada yake katika mwaka wa pili wa Yehoramu mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda.
18 Now the rest of the acts of Ahaziah, are they not recorded in the book of the history of the kings of Israel?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahazia na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?

< 2 Kings 1 >