< 1 Samuel 26 >

1 And the Ziphites went to Saul at Gibeah, saying: “Behold, David is hidden on the hill of Hachilah, which is opposite the wilderness.”
Wazifi wakamwendea Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi akujificha katika vilima vya Hakila, ambavyo viko mbele ya jangwa?”
2 And Saul rose up, and he descended into the desert of Ziph, and with him three thousand elect men of Israel, so that he might seek David in the desert of Ziph.
Kisha Sauli akaamka na kwenda chini ya jangwa la Zifu, akiwa na watu elfu tatu waliochaguliwa katika Israeli, wamtafute Daudi katika jangwa la Zifu.
3 And Saul encamped at Gibeah on Hachilah, which was opposite the wilderness on the way. But David was living in the desert. Then, seeing that Saul had arrived after him in the wilderness,
Sauli akaweka kambi kwenye kilima cha Hakila, kilicho mbele ya jangwa, kando ya barabara. Lakini Daudi alikuwa akikaa nyikani, na akaona kwamba Sauli alikuwa anamfuatia huko jangwani.
4 he sent explorers, and he learned that he certainly had arrived in that place.
Hivyo Daudi akawatuma wapelelezi na akafahamu kwamba hakika Sauli alikuwa amekuja.
5 And David rose up secretly, and he went to the place where Saul was. And when he had seen the place where Saul was sleeping, and Abner, the son of Ner, the leader of his military, and Saul sleeping in a tent, and the remainder of the common people all around him,
Daudi akaamka na kwenda hadi mahali ambapo Sauli alipiga kambi; akaona mahali alipolala Sauli, na Abneri mwana wa Neri, mkuu wa jeshi lake; Sauli alilala katikati ya kambi, na watu walipiga kambi kumzunguka, na wote wamesinzia.
6 David spoke to Ahimelech, the Hittite, and to Abishai, the son of Zeruiah, the brother of Joab, saying, “Who will descend with me to Saul in the camp?” And Abishai said, “I will descend with you.”
Ndipo Daudi akamwambia Ahimeleki Mhiti, na Abishai mwana wa Seruya, ndugu yake Yoabu, “Ni nani atakwenda nami kambini kwa Sauli? Abishai akasema, “Mimi nitashuka pamoja nawe.”
7 Therefore, David and Abishai went to the people by night, and they found Saul lying down and sleeping in the tent, with his spear fixed in the ground at his head. And Abner and the people were sleeping all around him.
Hivyo Daudi na Abishai wakaliendea jeshi usiku. Na Sauli alikuwapo akisinzia ndani ya kambi, mkuki wake umechomekwa chini pembeni mwa kichwa chake. Abneri na Askari wake wamelala kwa kumzunguka.
8 And Abishai said to David: “God has enclosed your enemy this day in your hands. Now therefore, I will pierce him with my lance, through to the ground, once, and there will not need to be a second.”
Kisha Abishai akamwambia Daudi, “Leo Mungu amemweka adui yako mkononi mwako. Basi tafadhali acha nimchome mkuki nimtoboe hadi chini kwa pigo moja. Sitampiga mara mbili.”
9 And David said to Abishai: “You shall not kill him. For who may extend his hand against the Christ of the Lord, and yet be innocent?”
Daudi akamwambia Abishai, “Usimwangamize; kwa maana nani awezaye kunyoosha mkono wake dhidi ya mtiwa mafuta wa BWANA na asiwe na hatia?”
10 And David said: “As the Lord lives, unless the Lord himself will strike him, or unless his day to die will have arrived, or unless, descending into battle, he will perish,
Daudi akasema, “Kama BWANA aishivyo, BWANA atamuua, au siku ya kufa kwake itakuja, au atakwenda katika vita na ataangamia.
11 may the Lord be gracious to me, so that I may not extend my hand against the Christ of the Lord. Now therefore, take the spear that is at his head, and the cup of water, and let us go.”
BWANA apishe mbali nisinyooshe mkono wangu dhidi ya mtiwa mafuta wake; lakini sasa, nakusihi chukua mkuki uliokichwani pake na jagi la maji, tuondoke.”
12 And so, David took the spear, and the cup of water that was at Saul’s head, and they went away. And there was no one who saw it, or realized it, or awakened, but they were all sleeping. For a deep sleep from the Lord had fallen over them.
Hivyo Daudi akachukua mkuki na jagi la maji kutoka kichwani pa Daudi, wakatoweka. Hakuna mtu aliyewaona au kufahamu habari hii, wala hakuna aliyetoka usingizini, maana wote walisinzia, kwa sababu usingizi mzito kutoka kwa BWANA uliwaangukia.
13 And when David had crossed over to the opposite side, and had stood upon the top of the hill far away, so that there was a great interval between them,
Kisha Daudi akaenda upande mwingine na akasimama juu ya mlima mbali sana; ukiwepo umbali mkubwa katikati yao.
14 David cried out to the people, and to Abner, the son of Ner, saying, “Will you not respond, Abner?” And responding, Abner said, “Who are you, that you would cry out and disquiet the king?”
Daudi akawapigia kelele watu hao na Abneri mwana Neri; akisema, “Hujibu neno, Abneri?” Ndipo Abneri akajibu na kusema, “Wewe ni nani unayempigia mfalme kelele?”
15 And David said to Abner: “Are you not a man? And who else is like you in Israel? Then why have you not guarded your lord the king? For one of the people entered, so that he might kill the king, your lord.
Daudi akamwambia Abneri, “Wewe siye mtu jasiri? Ni nani yuko kama wewe katika Israeli? Kwa nini basi hukukaa macho kumlinda bwana wako mfalme? Kwa maana mtu fulani aliingia kumuua mfalme, bwana wako.
16 This is not good, what you have done. As the Lord lives, you are sons of death, because you have not guarded your lord, the Christ of the Lord. Now therefore, where is the king’s spear, and where is the cup of water that was at his head?”
Jambo hili ulilolifanya siyo zuri. Kama BWANA aishivyo, unapaswa kufa kwa sababu hukumlinda bwana wako, mtiwa mafuta wa BWANA. Na sasa tazama ulipo mkuki wa mfalme, na jagi la maji lililokuwa kichwani pake.”
17 Then Saul recognized the voice of David, and he said, “Is this not your voice, my son David?” And David said, “It is my voice, my lord the king.”
Sauli aliitambua sauti ya Daudi akasema, “Hiyo ni sauti yako, Daudi mwanangu?” Daudi akasema, “Ni sauti yangu, mfalme, bwana wangu.”
18 And he said: “For what reason has my lord pursued his servant? What have I done? Or what evil is there in my hand?
Daudi akasema, “Kwa nini bwana wangu anamwandama mtumishi wake? Nimefanya nini? Mkononi mwangu kuna uovu gani?
19 Now therefore, listen, I beg you, my lord the king, to the words of your servant. If the Lord has stirred you up against me, let him make the sacrifice fragrant. But if the sons of men have done so, they are accursed in the sight of the Lord, who has cast me out this day, so that I would not live within the inheritance of the Lord, saying, ‘Go, serve strange gods.’
Kwa hiyo sasa, nakusihi, bwana wangu mfalme asikilize maneno ya mtumishi wake. Kama ni BWANA ndiye amekuchochea dhidi yangu, na aikubali sadaka; lakini kama ni wanadamu, na walaaniwe mbele za BWANA, maana leo wamenifukuza, nisishikamane na urithi wa BWANA; wameniambia, 'Nenda ukaabudu miungu mingine.'
20 And now, let not my blood be poured out upon the earth before the Lord. For the king of Israel has gone out, so that he might seek a flea, just as the partridge is pursued amid the mountains.”
Kwa hiyo, sasa, usiiachilie damu yangu ianguke ardhini mbali na uwepo wa BWANA; kwa kuwa mfalme wa Israeli ametoka nje kutafuta kiroboto, kama vile mtu awindavyo kware milimani.”
21 And Saul said: “I have sinned. Return, my son David. For I will never again do evil to you, because my life has been precious in your eyes this day. For it is apparent that I have acted senselessly, and have been ignorant of very many things.”
Kisha Sauli akasema, “Nimefanya dhambi. Rudi, Mwanangu, Daudi; maana sitakudhuru tena, kwa sababu leo maisha yangu yalikuwa yenye thamani machoni pako. Tazama, nimetenda upumbavu na nimekosa sana.”
22 And responding, David said: “Behold, the king’s spear. Let one of the servants of the king cross over and take it.
Daudi akajibu na akasema, “Tazama, mkuki wako uko hapa, mfalme! Mruhusu kijana mmojawapo aje auchukue na aulete kwako.
23 And the Lord will repay each one according to his justice and faith. For the Lord has delivered you this day into my hand, but I was not willing to extend my hand against the Christ of the Lord.
Na BWANA amlipe kila mtu kwa ajili ya uadilifu wake na kwa uaminifu wake; kwa sababu leo BWANA alikuweka mkononi mwangu, lakini nisinge mpiga mtiwa mafuta wake.
24 And just as your soul has been magnified this day in my eyes, so let my soul be magnified in the eyes of the Lord, and may he free me from all distress.”
Na tazama, kama maisha yako leo yalivyokuwa ya thamani machoni pangu, vivyo hivyo maisha yangu yathaminiwe sana machoni pa BWANA, na aweze kuniokoa katika shida zote.”
25 Then Saul said to David: “You are blessed, my son David. And whatever you may do, it shall certainly succeed.” And David departed on his way. And Saul returned to his place.
Ndipo Sauli akamwambia Daudi, “Na ubarikiwe, mwanangu Daudi, ili uweze kutenda mambo makuu, na hakika uweze kufanikiwa.” Ndipo Daudi akaenda zake, na Sauli akarudi kwake.

< 1 Samuel 26 >