< Genesis 43 >

1 Meanwhile, the famine pressed heavily on all the land.
Njaa ilikuwa kali katika nchi.
2 And having consumed the provisions that they had brought out of Egypt, Jacob said to his sons, “Return and buy us a little food.”
Ikawa walipokuwa wametumia chakula chote walichokitoa Misri, baba yao akawambia, “Nendeni tena; mtununulie chakula.”
3 Judah answered: “The man himself declared to us, under the attestation of an oath, saying: ‘You will not see my face, unless you bring your youngest brother with you.’
Yuda akamwambia, “Yule mtu alituonya kwa ukali, 'Hamtauona uso wangu ndugu yenu asipokuwa nanyi.'
4 If therefore you are willing to send him with us, we will travel together, and we will buy necessities for you.
Ikiwa utamtuma ndugu yetu pamoja nasi, tutashuka na kuwanunulia chakula.
5 But if you are not willing, we will not go. For the man, as we have often said, declared to us, saying: ‘You will not see my face without your youngest brother.’”
Lakini usipompeleka, hatutashuka. Kwa maana yule mtu alitwambia, 'Hamtauona uso wangu ndugu yenu asipokuwa nanyi.”
6 Israel said to them, “You have done this for my misery, in that you revealed to him that you also had another brother.”
Israeli akawambia, “Kwa nini mlinitendea mimi vibaya hivyo kwa kumwambia mtu huyo kwamba mnaye ndugu mwingine?”
7 But they responded: “The man questioned us in order, concerning our family: whether our father lived, if we had a brother. And we answered him respectively, according to what he demanded. How could we know that he would say, ‘Bring your brother with you?’”
Wakasema, “Yule mtu alituuliza habari zetu na familia yetu kwa kina. Akasema, 'Je baba yenu bado yuko hai? Je mnaye ndugu mwingine?'Tukamjibu kulingana na maswali haya. Tungejuaje kwamba angetwambia, 'Mleteni ndugu yenu?”
8 Likewise, Judah said to his father: “Send the boy with me, so that we may set out and be able to live, lest we and our little ones should die.
Yuda akamwambia Israeli baba yake, “Mtume kijana pamoja nami. Tutainuka na kwenda ili kwamba tuishi tusife, wote sisi, wewe, na hata watoto wetu.
9 I accept the boy; require him at my hand. Unless I lead him back and restore him to you, I will be guilty of a sin against you for all time.
Mimi nitakuwa mdhamini wake. Utaniwajibisha mimi. Kama nisipomleta na kumweka mbele yako, basi nibebe lawama daima.
10 If a delay had not intervened, by now we would have returned here a second time.”
Kwani kama tusingekawia, bila shaka hata sasa tungekuwa tumekwisha rudi mara ya pili.”
11 Therefore, their father Israel said to them: “If it is necessary to do so, then do what you will. Take, in your vessels, from the best fruits of the land, and carry down gifts to the man: a little resin, and honey, and storax ointment, oil of myrrh, turpentine, and almonds.
Israeli baba yao akawambia, “Kama ni hivyo, basi fanyeni hivi. Chukueni baadhi ya mazao mazuri ya nchi katika mifuko yenu. Mchukulieni yule mtu zawadi: baadhi ya malhamu, asali, viungo na manemane, jozi na lozi.
12 Also, take with you double the money, and carry back what you found in your sacks, lest perhaps it was done in error.
Chukueni pesa mara mbili mikononi mwenu. Pesa iliyorudishwa katika magunia yenu, muichukue tena katika mikono yenu. Pengine walikosea.
13 But also take your brother, and go to the man.
Mchukueni ndugu yenu pia. Inukeni na mwende tena kwa mtu yule.
14 Then may my Almighty God cause him to be pleased by you. And send your brother, whom he holds, back with you, along with this one, Benjamin. But as for me, without my children, I will be like one who is bereaved.”
Mungu Mwenyezi na awape kuona rehema mbele ya huyo mtu, hivyo kwamba awafungulie ndugu yenu mwingine na Benjamini. Kama nikipotelewa na watoto, nimepotelewa.”
15 Therefore, the men took the gifts, and double the money, and Benjamin. And they went down into Egypt, and they stood in the presence of Joseph.
Watu wale wakachukua zawadi hii, na katika mikono yao wakachukua mara mbili ya kiasi cha pesa, pamoja na Benjamini. Wakaamka na kushuka Misri na kusimama mbele ya Yusufu.
16 And when he had seen them and Benjamin together, he instructed the steward of his house, saying: “Lead the men into the house, and kill victims, and prepare a feast, because they will be eating with me at midday.”
Yusufu alipomwona Benjamini akiwa nao, akamwambia mtunzaji wa nyumba yake, “Walete watu hao ndani ya nyumba, chinja mnyama na umwandae, kwani watu hawa watakula chakula cha mchana pamoja nami.”
17 He did what he had been ordered to do, and he brought the men into the house.
Mtunzaji wa nyumba akafanya kama Yusufu alivyosema. Akawaleta wale watu nyumbani kwa Yusufu.
18 And there, being terrified, they said one to another: “Because of the money, which we carried back the first time in our sacks, we have been brought in, so that he may unleash a false accusation against us, and by violence subjugate both us and our donkeys into servitude.”
Wale ndugu wakaogopa kwa vile walivyoletwa katika nyumba ya Yusufu. Wakasema, “Ni kwa sababu ya pesa iliyorudishwa katika magunia yetu mara ya kwanza tulipoletwa ndani, kwamba atafute nafasi kinyume chetu. Kwamba aweze kutukamata na kutuchukua kama watumwa, na kuchukua punda wetu.” Wakamsogelea mtunzaji wa nyumba ya Yusufu,
19 For this reason, approaching the steward of the house at his door,
nao wakaongea naye mlangoni mwa nyumba,
20 they said: “We beg you, lord, to hear us. We came down once before to buy food.
wakisema, “Bwana wangu, tulikuja mara ya kwanza kununua chakula.
21 And having bought it, when we arrived at the inn, we opened our sacks and found the money in the mouths of the sacks, which we now have carried back in the same amount.
Ikawa, tulipofika katika eneo la kupumzikia, tukafungua magunia yetu, na, tazama, pesa ya kila mtu ilikuwa katika gunia lake, pesa yetu kwa kiasi kamili. Tumeileta katika mikono yetu.
22 But we have also brought other silver, so that we may buy those things that are necessary for us. It is not on our conscience who had placed it in our bags.”
Tumekuja na pesa nyingine pia mikonon mwetu ili kununua chakula. Hatujui aliyeziweka pesa katika magunia yetu.”
23 But he responded: “Peace be with you. Do not be afraid. Your God, and the God of your father, has given you the treasure in your sacks. As for the money that you gave to me, I held it as a test.” And he led Simeon out to them.
Mtunzaji wa nyumba akasema, “Amani iwe kwenu, msiogope. Mungu wenu na Mungu wa baba yenu ndiye aliyeweka pesa katika magunia yenu. Nilipokea pesa yenu.” Kisha mtunzaji wa nyumba akamleta Simoni kwao.
24 And having led them into the house, he brought water, and they washed their feet, and he gave fodder to their donkeys.
Msimamizi wa nyumba akawapeleka watu hao katika nyumba ya Yusufu. Akawapa maji, nao wakaosha miguu yao. Akawalisha punda wao.
25 But they also prepared the gifts, until Joseph entered at midday. For they had heard that they would eat bread there.
Wakaandaa zawadi kwa ajili ya Yusufu aliyekuwa akija mchana, kwani walikuwa wamesikia kwamba watakula pale.
26 And so Joseph entered his house, and they offered him the gifts, holding them in their hands. And they reverenced prone on the ground.
Yusufu alipokuja nyumbani, wakaleta nyumbani zawadi iliyokuwa mikononi mwao, nao wakainama mbele yake hata chini.
27 But he, gently greeting them again, questioned them, saying: “Is your father, the old man about whom you spoke to me, in good health? Is he still alive?”
Akawauliza juu ya hali zao na kusema,”Je baba yenu hajambo, yule mzee mliyemnena? Je bado yu hai?”
28 And they answered: “Your servant, our father, is safe; he is still alive.” And bowing, they reverenced him.
Wakasema, “Mtumishi wako baba yetu hajambo. Na bado yu hai” Wakajinyenyekeza na kuinama chini.
29 Then Joseph, lifting up his eyes, saw Benjamin, his brother of the same womb, and he said, “Is this your little brother, about whom you spoke to me?” And again, he said, “May God be compassionate to you, my son.”
Alipoinua macho yake akamwona Benjamini ndugu yake, mwana wa mamaye, naye akasema, “Je huyu ndiye mdogo wenu mliyemsema?” Na kisha akasema, “Mungu na awe mwenye neema kwako, mwanangu.”
30 And he hurried out, because his heart had been moved over his brother, and tears gushed out. And going into his chamber, he wept.
Yusufu akaharakisha kutoka chumbani, kwani aliguswa sana kuhusu nduguye. Akatafuta mahali pa kulia. Akaingia chumbani mwake na kulia umo.
31 And when he had washed his face, coming out again, he composed himself, and he said, “Set out bread.”
Akaosha uso wake na kutoka nje. Akajizuia mwenyewe, akasema, “karibuni chakula.”
32 And when it was set out, separately for Joseph, and separately for his brothers, likewise separately for the Egyptians, who ate at the same time, (for it is unlawful for Egyptians to eat with Hebrews, and they consider feasting in this way to be profane)
Watumishi wakamhudumia Yusufu peke yake na wale ndugu peke yao. Wamisri pale wakala pamoja naye peke yao kwa sababu Wamisri hawakuweza kula mkate na Waebrania, kwani hilo ni chukizo kwa Wamisri.
33 they sat before him, the firstborn according to his birthright, and the youngest according to his state of life. And they wondered exceedingly,
Wale ndugu wakakaa mbele yake, mzaliwa wa kwanza kwa kulingana na haki yake ya uzaliwa, na mdogo kulingana na ujana wake. Wale watu wakashangaa wote.
34 taking the portions that they received from him. And the greater portion went to Benjamin, so much so that it exceeded five parts. And they drank and became inebriated along with him.
Yusufu akapeleka sehemu kwao kutoka katika chakula kilichokuwa mbele yake. Lakini sehemu ya Benjamini ilikuwa mara tano zaidi ya kila ndugu zake. Wakanywa na wakamfurahia.

< Genesis 43 >