< Leviticus 20 >

1 And the Lord spoke to Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose,
2 Thus shalt thou say to the children of Israel: If any man of the children of Israel, or of the strangers, that dwell in Israel, give of his seed to the idol Moloch, dying let him die: the people of the land shall stone him.
“Sema na wana wa Israeli: ‘Mwisraeli yeyote au mgeni anayeishi katika Israeli ambaye atamtoa yeyote miongoni mwa watoto wake kuwa sadaka kwa mungu Moleki, mtu huyo lazima auawe. Watu wa jumuiya hiyo watampiga kwa mawe.
3 And I will set my face against him: and I will cut him off from the midst of his people, because he hath given of his seed to Moloch, and hath defiled my sanctuary, and profaned my holy name.
Mimi nitauelekeza uso wangu dhidi ya mtu huyo, nami nitamkatilia mbali na watu wake. Kwa maana kwa kumtoa mmoja wa watoto wake kwa mungu Moleki, amenajisi madhabahu yangu na kulinajisi Jina langu takatifu.
4 And if the people of the land neglecting, and as it were little regarding my commandment, let alone the man that hath given of his seed to Moloch, and will not kill him:
Ikiwa watu wa jumuiya watafumba macho wakati mtu huyo anapomtoa mmoja wa watoto wake kwa mungu Moleki, nao wakaacha kumuua,
5 I will set my face against that man, and his kindred, and will cut off both him and all that consented with him, to commit fornication with Moloch, out of the midst of their people.
mimi nitauelekeza uso wangu dhidi ya mtu huyo pamoja na jamaa yake, nami nitawakatilia mbali yeye na watu wote waliofanya ukahaba na Moleki.
6 The soul that shall go aside after magicians, and soothsayers, and shall commit fornication with them, I will set my face against that soul, and destroy it out of the midst of its people.
“‘Mimi nitauelekeza uso wangu dhidi ya mtu anayeenda kwa waaguzi na wenye pepo, na hivyo kujifanyia ukahaba kwa kuwafuata, nami nitamkatilia mbali na watu wake.
7 Sanctify yourselves, and be ye holy because I am the Lord your God.
“‘Jitakaseni basi, nanyi kuweni watakatifu, kwa sababu mimi ndimi Bwana Mungu wenu.
8 Keep my precepts, and do them. I am the Lord that sanctify you.
Shikeni amri zangu na kuzifuata. Mimi ndimi Bwana, niwafanyaye ninyi watakatifu.
9 He that curseth his father, or mother, dying let him die: he hath cursed his father, and mother, let his blood be upon him.
“‘Ikiwa mtu yeyote atamlaani baba yake au mama yake, lazima auawe. Amemlaani baba yake au mama yake, nayo damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.
10 If any man commit adultery with the wife of another, and defile his neighbour’s wife, let them be put to death, both the adulterer and the adulteress.
“‘Ikiwa mtu atazini na mke wa mtu mwingine, yaani mke wa jirani yake, wazinzi hao wawili lazima wauawe.
11 If a man lie with his stepmother, and discover the nakedness of his father, let them both be put to death: their blood be upon them.
“‘Kama mtu atakutana kimwili na mke wa baba yake, hakumheshimu baba yake. Mwanaume huyo na mwanamke huyo wote wauawe; damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.
12 If any man lie with his daughter in law, let both die, because they have done a heinous crime: their blood be upon them.
“‘Ikiwa mtu atakutana kimwili na mke wa mwanawe, lazima wote wawili wauawe. Walichokifanya ni upotovu; damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.
13 If any one lie with a man as with a woman, both have committed an abomination, let them be put to death: their blood be upon them.
“‘Kama mwanaume akikutana kimwili na mwanaume mwenzake kama vile mwanaume afanyavyo na mwanamke, wanaume hao wawili wamefanya lililo chukizo sana. Lazima wauawe; nayo damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.
14 If any man after marrying the daughter, marry her mother, he hath done a heinous crime: he shall be burnt alive with them: neither shall so great an abomination remain in the midst of you.
“‘Ikiwa mwanaume ataoa binti pamoja na mama yake, huo ni uovu. Wote watatu ni lazima wachomwe moto, ili kwamba pasiwepo na uovu katikati yenu.
15 He that shall copulate with any beast or cattle, dying let him die, the beast also ye shall kill.
“‘Kama mwanaume akikutana kimwili na mnyama, ni lazima auawe, na pia ni lazima mnyama huyo auawe.
16 The woman that shall lie under any beast, shall be killed together with the same: their blood be upon them.
“‘Kama mwanamke atamsogelea mnyama kukutana naye kimwili, muueni mwanamke huyo pamoja na mnyama pia. Lazima wauawe; damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.
17 If any man take his sister, the daughter of his father, or the daughter of his mother, and see her nakedness, and she behold her brother’s shame: they have committed a crime: they shall be slain, in the sight of their people, because they have discovered one another’s nakedness, and they shall bear their iniquity.
“‘Ikiwa mtu anamwoa dada yake, binti aliyezaliwa na baba yake au mama yake, nao wakakutana kimwili, ni aibu. Lazima wakatiliwe mbali machoni pa watu wao. Huyo mwanaume amemwaibisha dada yake, hivyo atawajibika kwa ajili ya uovu huo.
18 If any man lie with a woman in her flowers, and uncover her nakedness, and she open the fountain of her blood, both shall be destroyed out of the midst of their people.
“‘Ikiwa mwanaume atalala na mwanamke aliye katika hedhi yake na kukutana naye kimwili, amefunua mtiririko wa hedhi yake, naye huyo mwanamke amejifunua uchi wake. Wote wawili lazima wakatiliwe mbali na watu wao.
19 Thou shalt not uncover the nakedness of thy aunt by thy mother, and of thy aunt by thy father: he that doth this, hath uncovered the shame of his own flesh, both shall bear their iniquity.
“‘Usikutane kimwili na dada wa mama yako wala wa baba yako, kwa maana hilo litamwaibisha jamaa wa karibu; ninyi wawili mtawajibika kwa ajili ya uovu huo.
20 If any mall lie with the wife of his uncle by the father, or of his uncle by the mother, and uncover the shame of his near akin, both shall bear their sin: they shall die without children.
“‘Ikiwa mwanaume atakutana kimwili na shangazi yake, amemwaibisha mjomba wake. Nao watawajibika kwa ajili ya uovu huo; watakufa bila kuzaa mtoto.
21 He that marrieth his brother’s wife, doth an unlawful thing, he hath uncovered his brother’s nakedness: they shall be without children.
“‘Ikiwa mwanaume ataoa mke wa ndugu yake, hili ni tendo chafu; amemwaibisha ndugu yake. Nao hawatazaa mtoto.
22 Keep my laws and my judgments, and do them: lest the land into which you are to enter to dwell therein, vomit you also out.
“‘Zishikeni amri na sheria zangu zote na kuzifuata, ili nchi ninayowaleta kuishi isiwatapike.
23 Walk not after the laws of the nations, which I will cast out before you. For they have done all these things, and therefore I abhorred them.
Kamwe msiishi kwa kufuata desturi za mataifa nitakayoyafukuza mbele yenu. Kwa sababu walifanya mambo haya yote, nami nikachukizwa sana nao.
24 But to you I say: Possess their land which I will give you for an inheritance, a land flowing with milk and honey. I am the Lord your God, who have separated you from other people.
Lakini niliwaambia ninyi, “Mtaimiliki nchi yao; nitawapa ninyi kuwa urithi, nchi inayotiririka maziwa na asali.” Mimi ndimi Bwana Mungu wenu, ambaye amewatenga kutoka mataifa.
25 Therefore do you also separate the clean beast from the unclean, and the clean fowl from the unclean: defile not your souls with beasts, or birds, or any things that move on the earth, and which I have shewn you to be unclean.
“‘Kwa hiyo, ninyi lazima mweze kutofautisha kati ya wanyama walio safi na wasio safi, pia kati ya ndege wasio safi na walio safi. Msijitie unajisi kutokana na mnyama yeyote, au ndege, wala kitu chochote kitambaacho juu ya ardhi, vile ambavyo nimevitenga kuwa najisi kwa ajili yenu.
26 You shall be holy unto me, because I the Lord am holy, and I have separated you from other people, that you should be mine.
Mtakuwa watakatifu kwangu, kwa sababu Mimi, Bwana, ni mtakatifu, nami nimewatenga kutoka mataifa kuwa wangu mwenyewe.
27 A man, or woman, in whom there is a pythonical or divining spirit, dying let them die: they shall stone them: their blood be upon them.
“‘Mwanaume au mwanamke ambaye ni mchawi, mwaguzi au mwenye kupunga pepo miongoni mwenu lazima auawe. Mtawapiga kwa mawe; nayo damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.’”

< Leviticus 20 >