< Exodus 33 >

1 Afterward the Lord sayd vnto Moses, Depart, goe vp from hence, thou, and the people (which thou hast brought vp out of lande of Egypt) vnto the lande which I sware vnto Abraham, to Izhak and to Iaakob, saying, Vnto thy seede will I giue it.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Ondoka mahali hapa, wewe pamoja na hao watu uliowapandisha kutoka Misri, mpande mpaka nchi niliyomwahidi Abrahamu, Isaki na Yakobo kwa kiapo, nikisema, ‘Nitawapa wazao wenu nchi hii.’
2 And I will send an Angel before thee and will cast out the Canaanites, the Amorites, and the Hittites, and the Perizzites, the Hiuites, and the Iebusites:
Nitamtuma malaika mbele yenu, naye atawafukuza Wakanaani, Waamori, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
3 To a lande, I say, that floweth with milke and hony: for I will not goe vp with thee, because thou art a stiffe necked people, least I consume thee in the way.
Pandeni mwende katika nchi itiririkayo maziwa na asali. Lakini mimi sitakwenda pamoja nanyi, kwa sababu ninyi ni watu wenye shingo ngumu, nisije nikawaangamiza njiani.”
4 And when the people heard this euill tydings, they sorowed, and no man put on his best rayment.
Watu waliposikia habari hizo za huzuni, wakaanza kuomboleza wala hakuna mtu aliyevaa mapambo yoyote.
5 (For the Lord had said to Moses, Say vnto the children of Israel, Ye are a stiffe necked people, I wil come suddenly vpon thee, and consume thee: therefore now put thy costly rayment from thee, that I may know what to do vnto thee)
Kwa kuwa Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Waambie Waisraeli, ‘Ninyi ni watu wenye shingo ngumu. Kama ningefuatana nanyi hata kwa muda mfupi, ningewaangamiza. Sasa vueni mapambo yenu, nami nitaamua nitakalowatendea.’”
6 So the children of Israel layed their good raiment from them, after Moses came downe from the mount Horeb.
Hivyo Waisraeli wakavua mapambo yao katika Mlima wa Horebu.
7 Then Moses tooke his tabernacle, and pitched it without the host farre off from the hoste, and called it Ohel-moed. And whe any did seeke to the Lord, he went out vnto the Tabernacle of the Congregation, which was without the hoste.
Basi Mose alikuwa na desturi ya kuchukua hema na kuliweka wakfu nje ya kambi umbali kiasi, akaliita “Hema la Kukutania.” Kila aliyekuwa akiulizia shauri kwa Bwana, angelikwenda katika Hema la Kukutania nje ya kambi.
8 And when Moses went out vnto the Tabernacle, all the people rose vp, and stood euery man at his tent doore, and looked after Moses, vntil he was gone into the Tabernacle.
Wakati wowote Mose alipokwenda kwenye Hema, watu wote waliinuka na kusimama kwenye maingilio ya mahema yao, wakimwangalia Mose mpaka aingie kwenye Hema.
9 And assoone as Moses was entred into the Tabernacle, the cloudie pillar descended and stood at the doore of the Tabernacle, and the Lord talked with Moses.
Kila mara Mose alipoingia ndani ya hema, nguzo ya wingu ingeshuka chini na kukaa kwenye ingilio, wakati Mungu akizungumza na Mose.
10 Nowe when all the people saw the cloudie pillar stand at the Tabernacle doore, all the people rose vp, and worshipped euery man in his tent doore.
Kila mara watu walipoona hiyo nguzo ya wingu ikiwa imesimama kwenye ingilio la hema, wote walisimama wakaabudu, kila mmoja kwenye ingilio la hema lake.
11 And the Lord spake vnto Moses, face to face, as a man speaketh vnto his friende. After he turned againe into the hoste, but his seruant Ioshua the sonne of Nun a yong man, departed not out of the Tabernacle.
Bwana angezungumza na Mose uso kwa uso, kama vile mtu azungumzavyo na rafiki yake. Kisha Mose angerudi kambini, lakini msaidizi wake kijana Yoshua mwana wa Nuni hakuondoka mle Hemani.
12 Then Moses sayde vnto the Lord, See, thou sayest vnto me, Leade this people forth, and thou hast not shewed me whom thou wilt sende with mee: thou hast sayde moreouer, I knowe thee by name, and thou hast also found grace in my sight.
Mose akamwambia Bwana, “Umekuwa ukiniambia, ‘Ongoza watu hawa,’ lakini hujanifahamisha ni nani utakayemtuma pamoja nami. Umesema, ‘Ninakujua wewe kwa jina lako, nawe umepata kibali mbele zangu.’
13 Nowe therefore, I pray thee, if I haue founde fauour in thy sight, shewe mee nowe thy way, that I may knowe thee, and that I may finde grace in thy sight: consider also that this nation is thy people.
Ikiwa umependezwa nami, nifundishe njia zako ili nipate kukujua, nami nizidi kupata kibali mbele zako. Kumbuka kuwa taifa hili ni watu wako.”
14 And he answered, My presence shall go with thee, and I will giue thee rest.
Bwana akajibu, “Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha.”
15 Then he sayd vnto him, If thy presence go not with vs, cary vs not hence.
Kisha Mose akamwambia, “Kama Uso wako hauendi pamoja nasi, usituondoe hapa.
16 And wherein nowe shall it be knowen, that I and thy people haue found fauour in thy sight? shall it not be when thou goest with vs? so I, and thy people shall haue preeminence before all the people that are vpon the earth.
Mtu yeyote atajuaje kuwa mimi pamoja na watu wako tumepata kibali mbele zako, usipokwenda pamoja nasi? Ni nini kingine kitakachoweza kututofautisha mimi na watu wako miongoni mwa watu wengine wote walio katika uso wa dunia?”
17 And the Lord sayde vnto Moses, I will doe this also that thou hast saide: for thou hast founde grace in my sight, and I knowe thee by name.
Bwana akamwambia Mose, “Nitakufanyia jambo lile uliloomba, kwa sababu ninapendezwa nawe, nami ninakujua kwa jina lako.”
18 Againe he sayde, I beseech thee, shewe me thy glory.
Kisha Mose akasema, “Basi nionyeshe utukufu wako.”
19 And he answered, I wil make all my good go before thee, and I wil proclaime the Name of the Lord before thee: for I will shewe mercy to whom I will shewe mercy, and will haue compassion on whom I will haue compassion.
Ndipo Bwana akasema, “Nitapitisha wema wangu wote mbele yako, nami nitalitangaza Jina langu, Bwana, mbele ya uso wako. Nitamrehemu yeye nimrehemuye, na pia nitamhurumia yeye nimhurumiaye.”
20 Furthermore he sayde, Thou canst not see my face, for there shall no man see me, and liue.
Lakini Mungu akasema, “Hutaweza kuuona uso wangu, kwa kuwa hakuna mtu yeyote awezaye kuniona akaishi.”
21 Also the Lord sayd, Behold, there is a place by me, and thou shalt stand vpon the rocke:
Kisha Bwana akasema, “Kuna mahali karibu nami ambapo unaweza kusimama juu ya mwamba.
22 And while my glory passeth by, I will put thee in a cleft of the rocke, and will couer thee with mine hand whiles I passe by.
Utukufu wangu unapopita, nitakuweka gengeni kwenye mwamba na kukufunika kwa mkono wangu mpaka nitakapokwisha kupita.
23 After I will take away mine hande, and thou shalt see my backe parts: but my face shall not be seene.
Kisha nitaondoa mkono wangu nawe utaona mgongo wangu; lakini kamwe uso wangu hautaonekana.”

< Exodus 33 >