< Joshua 20 >

1 The Lord also spake vnto Ioshua, saying,
Ndipo Bwana akamwambia Yoshua,
2 Speake to the children of Israel, and say, Appoint you cities of refuge, whereof I spake vnto you by the hand of Moses,
“Waambie Waisraeli, watenge miji mikubwa ya kukimbilia, kama nilivyokuagiza kupitia Mose,
3 That the slaier that killeth any person by ignorance, and vnwittingly, may flee thither, and they shall be your refuge from the auenger of blood.
ili mtu yeyote atakayemuua mtu kwa bahati mbaya na pasipo kukusudia aweze kukimbilia huko na kujiepusha na mlipiza kisasi wa damu.
4 And he that doeth flee vnto one of those cities, shall stand at the entring of the gate of the citie, and shall shewe his cause to the Elders of the citie: and they shall receiue him into the citie vnto them, and giue him a place, that hee may dwell with them.
“Anapokimbilia mojawapo ya hii miji mikubwa atasimama kwenye maingilio ya lango la mji mkuu na kueleza wazee wa mji kuhusu shauri lake. Kisha watampokea katika mji wao na kumpa mahali pa kuishi nao.
5 And if the auenger of blood pursue after him, they shall not deliuer the slaier into his hand because hee smote his neighbour ignorantly, neither hated he him before time:
Kama mlipiza kisasi wa damu akimfuatilia, wasimkabidhi yule mshtakiwa, kwa sababu alimuua jirani yake bila kukusudia, na bila kuwa na nia ya kudhuru.
6 But hee shall dwell in that citie vntill hee stande before the Congregation in iudgement, or vntill the death of the hie Priest that shall be in those daies: then shall the slaier returne, and come vnto his owne citie, and vnto his owne house, euen vnto the citie from whence he fled.
Huyu aliyeua atakaa kwenye mji mkubwa huo mpaka awe amesimama kukabili mashtaka yake mbele ya kusanyiko na mpaka kuhani mkuu anayehudumu kwa wakati huo atakapokufa. Ndipo atakapoweza kurudi nyumbani kwake katika mji ambao aliukimbia.”
7 Then they appointed Kedesh in Galil in mount Naphtali, and Shechem in mount Ephraim, and Kiriath-arba, (which is Hebron) in the mountaine of Iudah.
Basi wakatenga Kedeshi katika Galilaya kwenye nchi ya vilima ya Naftali, Shekemu katika nchi ya vilima ya Efraimu, na Kiriath-Arba (yaani Hebroni) kwenye nchi ya vilima ya Yuda.
8 And on the other side Iorden toward Iericho Eastward, they appoynted Bezer in the wildernesse vpon the plaine, out of the tribe of Reuben, and Ramoth in Gilead, out of the tribe of Gad, and Golan in Bashan, out of the tribe of Manasseh.
Katika upande wa mashariki mwa Yordani ya Yeriko wakatenga Bezeri katika jangwa katika uwanda wa juu katika kabila la Reubeni, Ramothi katika Gileadi katika kabila la Gadi, na Golani huko Bashani katika kabila la Manase.
9 These were the cities appoynted for all the children of Israel, and for the stranger that soiourned among them, that whosoeuer killed any person ignorantly, might flee thither, and not die by the hande of the auenger of blood, vntill hee stoode before the Congregation.
Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote aishiye miongoni mwao aliyemuua mtu kwa bahati mbaya, angeweza kukimbilia katika miji mikubwa hiyo iliyotengwa na asiuawe na mlipiza kisasi wa damu kabla hajasimama kukabili mashtaka mbele ya kusanyiko.

< Joshua 20 >