< Joshua 20 >

1 The Lord also spake vnto Ioshua, saying,
Baada ya hayo, Yahweh akamwambia Yoshua,
2 Speake to the children of Israel, and say, Appoint you cities of refuge, whereof I spake vnto you by the hand of Moses,
“Waambia watu wa Israeli, na kusema, 'Chagueni miji ya makimbilio ambayo niliwaambia kupitia kwa Musa.
3 That the slaier that killeth any person by ignorance, and vnwittingly, may flee thither, and they shall be your refuge from the auenger of blood.
Fanyeni hivi ili mtu akiua mtu bila kukusudia aweze kwenda huko. Miji hii itakuwa ni sehemu ya kukimbilia kutoka kwa mtu yeyote yule anayetaka kulipiza kisasi kwa damu ya mtu aliyeuliwa.
4 And he that doeth flee vnto one of those cities, shall stand at the entring of the gate of the citie, and shall shewe his cause to the Elders of the citie: and they shall receiue him into the citie vnto them, and giue him a place, that hee may dwell with them.
Atakimbilia kwa mji mmoja miongoni mwa miji hiyo na atasimama mlangoni mwa lango la mji, na ataeleza kesi yake kwa wazee wa mji ule. Kisha watamwingiza ndani ya mji na watampatia sehemu yake ya kuishi miongoni mwao.
5 And if the auenger of blood pursue after him, they shall not deliuer the slaier into his hand because hee smote his neighbour ignorantly, neither hated he him before time:
Na kama mtu akija akataka kulipiza kisasi kwa damu ya mtu yule ambaye aliuliwa, ndipo watu wa mji hawatatakiwa kumtoa kwa wenye mamlaka mtu huyo aliyeua. Hawaruhusiwi kufanya hivyo kwasababu alimwua jirani bila kukusudia na hakuwa na chuki naye hapo awali.
6 But hee shall dwell in that citie vntill hee stande before the Congregation in iudgement, or vntill the death of the hie Priest that shall be in those daies: then shall the slaier returne, and come vnto his owne citie, and vnto his owne house, euen vnto the citie from whence he fled.
Ni lazima akae katika mji ule mpaka pale atakapokuwa amesimama mbele ya kusanyiko kwa ajili ya kuhukumiwa, hadi pale atakapokufa mtu yule anayetumika katika nafasi ya kuhani mkuu katka siku hizo. Na kisha mtu yule aliyeua bila kukusudia aweza kurudi nyumbani kwake, katika mji ule ulikotoka.
7 Then they appointed Kedesh in Galil in mount Naphtali, and Shechem in mount Ephraim, and Kiriath-arba, (which is Hebron) in the mountaine of Iudah.
Kwahiyo, Waisraeli wakaichaguia Kedeshi iliyoko Galilaya katika nchi ya milima ya Nafutali, Shekemu katika nchi ya milima ya Efraimu, na Kiriathi Arba (ambayo ndio Herbroni) katika nchi ya milima ya Yuda.
8 And on the other side Iorden toward Iericho Eastward, they appoynted Bezer in the wildernesse vpon the plaine, out of the tribe of Reuben, and Ramoth in Gilead, out of the tribe of Gad, and Golan in Bashan, out of the tribe of Manasseh.
Katika ng'ambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko, walichagua mji wa Bezeri huko nyikani katika nyanda za kabila la Rubeni; na Ramothi Gileadi kutoka kabila la Gadi; na Golani katika Bashani, kutoka katika kabila la Manase.
9 These were the cities appoynted for all the children of Israel, and for the stranger that soiourned among them, that whosoeuer killed any person ignorantly, might flee thither, and not die by the hande of the auenger of blood, vntill hee stoode before the Congregation.
Hii ni miji iliyochaguliwa kwa ajili ya watu wote wa Israeli na kwa ajili ya wageni wanaoishi miongoni mwao, ili kwamba mtu yeyote amwuaye mtu bila kukusudia aweza kukimbilia huko kwa ajili ya kupata usalama. Mtu huyu hatakufa kwa mkono wa mtu yule anayetake kulipiza kisasi cha damu iliyomwagwa, mpaka hapo kwanza mtuhumiwa atakaposimama mbele ya kusanyiko la watu.

< Joshua 20 >