< Micah 1 >

1 The word of the Lord, that came vnto Micah the Morashite in the dayes of Iotham, Ahaz, and Hezekiah Kings of Iudah, which he sawe concerning Samaria, and Ierusalem.
Neno la Bwana lilimjia Mika, Mmoreshethi, wakati wa utawala wa Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda; ufunuo aliouona kuhusu Samaria na Yerusalemu.
2 Heare, al ye people: hearke thou, O earth, and all that therein is, and let the Lord God be witnes against you, euen ye Lord from his holy Teple.
Sikieni, enyi mataifa, enyi nyote, sikilizeni, ee dunia na wote mliomo ndani yake, ili Bwana Mwenyezi ashuhudie dhidi yenu, Bwana kutoka Hekalu lake takatifu.
3 For beholde, the Lord commeth out of his place, and will come downe, and tread vpon the hie places of the earth.
Tazama! Bwana anakuja kutoka mahali pake; anashuka na kukanyaga mahali palipoinuka juu pa dunia.
4 And the mountaines shall melt vnder him (so shall the valleys cleaue) as waxe before the fire, and as the waters that are powred downewarde.
Milima inayeyuka chini yake na mabonde yanagawanyika kama nta mbele ya moto, kama maji yatiririkayo kasi kwenye mteremko.
5 For the wickednes of Iaakob is all this, and for the sinnes of the house of Israel: what is the wickednes of Iaakob? Is not Samaria? and which are the hie places of Iudah? Is not Ierusalem?
Yote haya ni kwa sababu ya kosa la Yakobo, ni kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. Kosa la Yakobo ni lipi? Je, sio Samaria? Je, mahali pa juu pa Yuda pa kuabudia miungu ni nini? Je, sio Yerusalemu?
6 Therefore I wil make Samaria as an heape of the fielde, and for the planting of a vineyard, and I will cause the stones thereof to tumble downe into the valley, and I will discouer the foundations thereof.
“Kwa hiyo nitaufanya Samaria kuwa lundo la kokoto, mahali pa kuotesha mizabibu. Nitayamwaga mawe yake katika bonde na kuacha wazi misingi yake.
7 And all the grauen images thereof shalbe broken, and all the giftes thereof shalbe burnt with the fire, and all the idoles thereof will I destroy: for she gathered it of the hire of an harlot, and they shall returne to the wages of an harlot.
Sanamu zake zote zitavunjwa vipande vipande; zawadi zake zote za Hekalu zitachomwa kwa moto; nitaharibu vinyago vyake vyote. Kwa kuwa alikusanya zawadi zake kutokana na ujira wa kahaba, nazo zitatumika tena kulipa mishahara ya kahaba.”
8 Therefore I will mourne and howle: I wil goe without clothes, and naked: I will make lamentation like the dragons, and mourning as the ostriches.
Kwa ajili ya hili nitalia na kuomboleza; nitatembea bila viatu na tena uchi. Nitabweka kama mbweha na kuomboleza kama bundi.
9 For her plagues are grieuous: for it is come into Iudah: the enemie is come vnto the gate of my people, vnto Ierusalem.
Kwa sababu jeraha lake halitibiki; limekuja Yuda. Limefika hasa kwenye lango la watu wangu, hata Yerusalemu kwenyewe.
10 Declare ye it not at Gath, neither weepe ye: for the house of Aphrah roule thy selfe in the dust.
Usiliseme hili huko Gathi; usilie hata kidogo. Huko Beth-le-Afra gaagaa mavumbini.
11 Thou that dwellest at Shaphir, go together naked with shame: she that dwelleth at Zaanan, shall not come forth in ye mourning of Beth-ezel: the enemie shall receiue of you for his standing.
Piteni mkiwa uchi na wenye aibu, ninyi mkaao Shafiri. Wale waishio Saanani hawatatoka nje. Beth-Eseli iko katika maombolezo; kinga yake imeondolewa kwako.
12 For the inhabitant of Maroth wayted for good, but euill came from the Lord vnto the gate of Ierusalem.
Wale waishio Marothi wanagaagaa kwa maumivu wakingoja msaada, kwa sababu maangamizi yamekuja kutoka kwa Bwana, hata katika lango la Yerusalemu.
13 O thou inhabitant of Lachish, binde the charet to the beastes of price: she is the beginning of the sinne to the daughter of Zion: for the transgressions of Israel were found in thee.
Enyi mkaao Lakishi, fungeni farasi kwenye magari ya vita. Mlikuwa chanzo cha dhambi kwa Binti Sayuni, kwa kuwa makosa ya Israeli yalikutwa kwako.
14 Therefore shalt thou giue presents to Moresheth Gath: the houses of Achzib shalbe as a lye to the Kings of Israel.
Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi zawadi za kuagana. Mji wa Akzibu utaonyesha wazi udanganyifu kwa wafalme wa Israeli.
15 Yet will I bring an heire vnto thee, O inhabitant of Mareshah, he shall come vnto Adullam, the glorie of Israel.
Nitawaleteeni atakayewashinda ninyi mnaoishi Maresha. Yeye aliye utukufu wa Israeli atakuja Adulamu.
16 Make thee balde: and shaue thee for thy delicate children: enlarge thy baldenesse as the eagle, for they are gone into captiuity from thee.
Nyoeni nywele zenu katika kuomboleza kwa ajili ya watoto wenu mnaowafurahia; jifanyieni upara kama tai, kwa kuwa watawaacha na kwenda uhamishoni.

< Micah 1 >