< Revelation 7 >

1 And after that, I sawe foure Angels stand on the foure corners of the earth, holding the foure windes of the earth, that the winds should not blow on the earth, neither on the sea, neither on any tree.
Baada ya haya niliona malaika wanne wamesimama kwenye kona nne za dunia, wamezuia pepo nne za nchi kwa nguvu ili kwamba pasiwe na upepo unaovuma katika nchi, juu ya bahari au dhidi ya mti wowote.
2 And I sawe another Angel come vp from the East, which had the seale of the liuing God, and hee cried with a loud voice to the foure Angels to who power was giuen to hurt the earth, and the sea, saying,
Nikaona malaika mwingine akija kutoka mashariki, aliyekuwa na muhuri wa Mungu aliye hai. Akalia kwa sauti kuu kwa malaika wanne ambao walipewa ruhusa ya kudhuru nchi na bahari:
3 Hurt ye not the earth, neither the sea, neither the trees, til we haue sealed the seruants of our God in their foreheads.
“Msiidhuru nchi, bahari, au miti mpaka tutakapokuwa tumekwishaweka muhuri katika paji za vichwa vya watumishi wa Mungu wetu.”
4 And I heard the number of them, which were sealed, and there were sealed an hundreth and foure and fourtie thousand of all the tribes of the children of Israel.
Nikasikia idadi ya wale waliotiwa muhuri: 144, 000, ambao walitiwa muhuri kutoka kila kabila ya watu wa Israel:
5 Of the tribe of Iuda were sealed twelue thousande. Of the tribe of Ruben were sealed twelue thousande. Of the tribe of Gad were sealed twelue thousande.
12, 000 kutoka katika kabila ya Yuda walitiwa muhuri, 12, 000 kutoka katika kabila ya Rubeni, 12, 000 kutoka katika kabila ya Gadi.
6 Of the tribe of Aser were sealed twelue thousand. Of the tribe of Nephthali were sealed twelue thousand. Of the tribe of Manasses were sealed twelue thousand.
12, 000 kutoka katika kabila ya Asheri, 12, 000 kutoka katika kabila ya Naftali, 12, 000 kutoka katika kabila ya Manase.
7 Of the tribe of Simeon were sealed twelue thousande. Of the tribe of Leui were sealed twelue thousande. Of the tribe of Issachar were sealed twelue thousand. Of the tribe of Zabulon were sealed twelue thousand.
12, 000 kutoka kabila ya Simioni, 12, 000 kutoka kabila ya Lawi, 12, 000 kutoka kabila ya Isakari,
8 Of the tribe of Ioseph were sealed twelue thousande. Of the tribe of Beniamin were sealed twelue thousand.
12, 000 kutoka kabila ya Zebuloni, 12, 000 kutoka kabila ya Yusufu, na 12, 000 kutoka kabila ya Benyamini walitiwa muhuri.
9 After these thinges I behelde, and loe a great multitude, which no man coulde number, of all nations and kindreds, and people, and tongues, stoode before the throne, and before the Lambe, clothed with long white robes, and palmes in their hands.
Baada ya mambo haya nilitazama, na kulikuwa na umati mkubwa ambao hapana mtu angeweza kuuhesabu - kutoka kila taifa, kabila, jamaa, na lugha - wamesimama mbele ya kiti cha enzi na mbele ya Mwanakondoo. Walikuwa wamevaa kanzu nyeupe na wana matawi ya mitende mikononi mwao,
10 And they cried with a loud voice, saying, Saluation commeth of our God, that sitteth vpon the throne, and of the Lambe.
na walikuwa wakiita kwa sauti ya juu: “Wokovu ni kwa Mungu ambaye ameketi katika kiti cha enzi, na kwa Mwanakondoo!”
11 And all the Angels stoode rounde about the throne, and about the Elders, and the foure beastes, and they fell before the throne on their faces, and worshipped God,
Malaika wote waliokuwa wamesimama kuzunguka kiti cha enzi na kuwazunguka wale wazee pamoja na wenye uhai wanne, wakainama chini ardhini na wakaweka nyuso zao juu ya ardhi mbele ya kiti cha enzi na wakamwabudu Mungu,
12 Saying, Amen. Praise, and glorie, and wisdom, and thankes, and honour, and power, and might bee vnto our God for euermore, Amen. (aiōn g165)
wakisema, “Amina! Sifa, utukufu, hekima, shukurani, heshima, uwezo na nguvu viwe kwa Mungu wetu milele na milele! Amina!” (aiōn g165)
13 And one of the Elders spake, saying vnto me, What are these which are araied in log white robes? and whence came they?
Kisha mmoja wa wale wazee akaniuliza, “hawa ni akina nani waliovaa kanzu nyeupe, na wametoka wapi?
14 And I saide vnto him, Lord, thou knowest. And he saide to me, These are they, which came out of great tribulation, and haue washed their long robes, and haue made their long robes white in the blood of the Lambe.
Nikamwambia, “Bwana mkubwa, unajua wewe,” na akaniambia, “Hawa ni wale waliotoka katika dhiki kuu. Wamezifua kanzu zao na kuzifanya nyeupe kwa damu ya Mwanakondoo.
15 Therefore are they in the presence of the throne of God, and serue him day and night in his Temple, and he that sitteth on the throne, wil dwell among them.
Kwa sababu hii, wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, na wanamwabudu yeye usiku na mchana katika hekalu lake. Yeye aliye keti juu ya kiti cha enzi atasambaza hema yake juu yao.
16 They shall hunger no more, neither thirst any more, neither shall the sunne light on them, neither any heate.
Hawataona njaa tena, wala kiu tena. Jua halitawachoma, wala joto la kuunguza.
17 For the Lambe, which is in the middes of the throne, shall gouerne them, and shall leade them vnto the liuely fountaines of waters, and God shall wipe away all teares from their eyes.
Kwa kuwa Mwanakondoo aliye katikati ya kiti cha enzi atakuwa mchungaji wao, na atawaongoza katika chemchemi ya maji ya uzima, na Mungu atafuta kila chozi katika macho yao.”

< Revelation 7 >