< Exodus 7 >

1 And the Lord spoke to Moses, saying, Behold, I have made you a god to Pharao, and Aaron your brother shall be your prophet.
Yahweh akasema na Musa, “Ona, nimekufanya kama mungu kwa Farao. Aruni kaka yako atakuwa nabii wako.
2 And you shall say to him all things that I charge you, and Aaron your brother shall speak to Pharao, that he should send forth the children of Israel out of his land.
Utasema kila kitu nitacho kuamuru kusema. Aruni kaka yako ata sema na Farao iliawaachie watu wa Israeli watoke kwenye nchi yake.
3 And I will harden the heart of Pharao, and I will multiply my signs and wonders in the land of Egypt.
Lakini nitaufanya moyo wa Farao mgumu, na nitaonyesha ishara nyingi za nguvu zangu, maajabu mengi, katika nchi ya Misri.
4 And Pharao will not listen to you, and I will lay my hand upon Egypt; and will bring out my people the children of Israel with my power out of the land of Egypt with great vengeance.
Lakini Farao hata kusikiliza, kwahiyo nitaueka mkono wangu juu ya Misri na kutoa makundi yangu ya wanaume wapiganaji, watu wangu, wazao wa Israeli, watoke nchi ya Misri kwa matendo makubwa ya hukumu.
5 And all the Egyptians shall know that I am the Lord, stretching out my hand upon Egypt, and I will bring out the children of Israel out of the midst of them.
Wamisri watajua kuwa mimi ni Yahweh nitapo nyoosha mkono wangu kwa Misri na kuwatoa Waisraeli kutoka miongoni mwao.”
6 And Moses and Aaron did as the Lord commanded them, so did they.
Musa na Aruni wakafanya hivyo; walifanya kama Yahweh alivyo waamuru.
7 And Moses was eighty years old, and Aaron his brother was eighty-three years old, when he spoke to Pharao.
Musa alikuwa na miaka themanini, na Aruni miaka themanini na tatu walipo ongea na Farao.
8 And the Lord spoke to Moses and Aaron, saying,
Yahweh akamwambia Musa na Aruni,
9 Now if Pharao should speak to you, saying, Give us a sign or a wonder, then shall you say to your brother Aaron, Take your rod and cast it upon the ground before Pharao, and before his servants, and it shall become a serpent.
“Wakati Farao atakapo waambia, 'Fanya muujiza,' utamwambia Aruni, 'Chukuwa gongo lako na ulirushe chini mbele ya Farao, ililigeuke nyoka.”'
10 And Moses and Aaron went in before Pharao, and [before] his servants, and they did so, as the Lord commanded them; and Aaron cast down his rod before Pharao, and before his servants, and it became a serpent.
Kisha Musa na Aruni wakaenda kwa Farao, na wakafanya kama Yahweh alivyo waamuru. Aruni akarusha chini gongo lake mbele ya Farao na watumishi wake, na likageuka nyoka.
11 But Pharao called together the wise men of Egypt, and the sorcerers, and the charmers also of the Egyptians did likewise with their sorceries.
Kisha naye Farao akawaita wazee wenye hekima na wachawi. Wakafanya jambo hilo hilo kwa uchawi wao.
12 And they cast down each his rod, and they became serpents, but the rod of Aaron swallowed up their rods.
Kila mtu akarusha chini gongo lake, na magongo yakawa nyoka. Lakini gongo la Aruni lilimeza nyoka zao.
13 and the heart of Pharao was hardened, and he listened not to them, as the Lord charged them.
Moyo wa Farao ulikuwa mgumu, na akusikiliza, kama Yahweh alivyo tabiri.
14 and the Lord said to Moses, The heart of Pharao is made hard, so that he should not let the people go.
Yahweh akasema na Musa, “Moyo wa Farao ni mgumu, na anakataa kuacha watu waende.
15 Go to Pharao early in the morning: behold, he goes forth to the water; and you shall meet him on the bank of the river, and you shall take in your hand the rod that was turned into a serpent.
Nenda kwa Farao asubui anapoenda kwenye maji. Simama kwenye chanzo cha mto kukutana naye, na uchukuwe mkononi mwako gongo ambalo liligeuka nyoka.
16 And you shall say to him, The Lord God of the Hebrews has sent me to you, saying, Send my people away, that they may serve me in the wilderness, and, behold, hitherto you have not listened.
Mwambie, 'Yahweh, Mungu wa Waebrania, amenituma kwako, “Acha watu wangu waende, iliwaniabudu nyikani. Mpaka sasa haujanisikiliza.”
17 These things says the Lord: Hereby shall you know that I am the Lord: behold, I strike with the rod that is in my hand on the water which is in the river, and it shall change it into blood.
Yahweh anasema hili: “Kwa hili utajua kuwa mimi ni Yahweh. Ninaenda kupiga maji ya mto wa Misri kwa gongo langu lililo mikono mwangu, na mto utageuzwa kuwa damu.
18 And the fish that are in the river shall die, and the river shall stink thereupon, and the Egyptians shall not be able to drink water from the river.
Samaki walio kwenye mto watakufa, na mto utanuka. Wa Misri Hawataweza kunywa maji yalio kwenye mto.”'''
19 And the Lord said to Moses, Say to your brother Aaron, Take your rod in your hand, and stretch forth your hand over the waters of Egypt, and over their rivers, and over their canals, and over their ponds, and over all their standing water, and it shall become blood: and there was blood in all the land of Egypt, both in vessels of wood and of stone.
Kisha Yahweh akasema na Musa, “Mwambie Aruni, 'Chukuwa gongo lako na unyooshe mkono kwenye maji ya Misri, na juu ya mito yake, mifereji, visima, na madimbwi yote, ili maji yao ya damu. Fanya hivi ilikuwe na damu nchi nzima ya Misri, hadi kwenye vyombo vyote vya mbao na mawe.”'
20 and Moses and Aaron did so, as the Lord commanded them; and [Aaron] having lifted up [his hand] with his rod, struck the water in the river before Pharao, and before his servants, and changed all the water in the river into blood.
Musa na Aruni walifanya kama Yahweh alivyo waamuru. Aruni alinyanyua gongo na kupiga maji ya mto, machoni pa Farao na watumishi wake. Maji yote kwenye mto yaligeuga damu.
21 And the fish in the river died, and the river stank thereupon; and the Egyptians could not drink water from the river, and the blood was in all the land of Egypt.
Samaki kwenye mto wakafa, na mto ukaanza kunuka. Wamisri hawakuweza kunywa maji kwenye mto, na damu ilikuwa kila mahali katika nchii ya Misri.
22 And the charmers also of the Egyptians did so with their sorceries; and the heart of Pharao was hardened, and he did not listen to them, even as the Lord said.
Lakini wachawi walifanya vivyo hivyo na uchawi wao. Kwaiyo moyo wa Farao ukawa mgumu, na akakataa kuwasikiliza Musa na Aruni, kama Yahweh alivyo sema itatokea.
23 And Pharao turned and entered into his house, nor did he fix his attention even on this thing.
Kisha Farao akarudi na kwenda nyumbani kwake. Wala hakutilia maanani hili.
24 And all the Egyptians dug round about the river, so as to drink water, for they could not drink water from the river.
Wamisri wote walichimba pembeni ya mto kwa ajili ya maji ya kunywa, lakini hawakuweza kunywa maji ya mto.
25 and seven days were fulfilled after the Lord has struck the river.
Siku saba zilipita baada ya Yahweh kushambulia mto.

< Exodus 7 >