< Ezekiel 21 >

1 Then came the word of Yahweh unto me, saying:
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 Son of man Set thy face against Jerusalem, And drop thy word against the holy places And prophesy against the soil of Israel.
“Mwanadamu, weka uso wako kuelekea Yerusalemu, na neno juu ya patakatifu; tabiri juu ya nchi ya Israeli.
3 Thou shalt say then to the soil of Israel Thus saith Yahweh, Behold me against thee, Therefore will I bring forth my sword out of its sheath, —and will cut off from thee the righteous and the lawless.
Sema juu ya nchi ya Israeli, 'Yahwe asema hivi: Tazama! Ni juu yako! Nitautoa upanga wangu kutoka kwenye ala yake na kuwakatilia mbali wote yaani mtu mwenye haki na mtu mwovu kutoka kwako!
4 Because I have cut off from thee the righteous and the lawless, Therefore shall my sword go forth out of its sheath against all flesh from south to north:
Ili niwakatilie mbali wote, mwenye haki na mwovu kutoka kwako, upanga wangu utatoka kwenye ala yake juu ya wote wenye mwili kutoka kusini hata kaskazini.
5 So shall all flesh know that, I, Yahweh have brought forth my sword out of its sheath, — it shall not return any more.
Kisha wote wenye mwili watajua yakwamba mimi, Yahwe, nimeutoa upanga wangu kutoka kwenye ala yake. Hautarudi tena!'
6 Thou, therefore O son of man sigh, — In the sharp pain of thy loins and in bitterness, shalt thou sigh before their eyes.
Kwa hiyo, mwanadamu, gumia kama kuvunjika kwa viuno vyako! Katika uchungu gumia mbele ya macho yao!
7 And it shall come to pass when they shall say unto thee, Wherefore art thou sighing? that thou shalt say, For the report because it cometh, When every heart shall melt. And all hands be unnerved And every spirit shall become faint. And all knees shall be weak as water, Lo! it cometh and shall be brought to pass, Saith My Lord, Yahweh.
Kisha itatokea kwamba watakuuliza, 'Kwa sababu gani unalia?' Kisha utasema, 'Kwa sababu ya habari inayokuja, kwa kuwa kila moyo utakuwa dhaifu, na kila mkono utasita! Kila roho itazimia, na kila goti litatiririrka kama maji. Tazama! Inakuja na itakuwa kama hivi! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
8 And the word of Yahweh came unto me. saying:
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
9 Son of man, Prophesy and thou shalt say, Thus saith My Lord, — Say, A sword! a sword! Sharpened moreover also furbished:
“Mwanadamu, tabiri na sema, 'Bwana asema hivi: sema: Upanga! Upanga! Utachongwa na kusuguliwa!
10 To make a slaughter, is it sharpened, That it may flash as lightning, is it furbished. Or shall we flourish the royal rod of my son which despiseth every tree?
Utanolewa ili kushiriki katika machinjio makubwa! Utasuguliwa ili uwe kama mng'ao wa radi! Je! Tufanye furaha katika fimbo ya mwana wa mfalme? Upanga ujao huchukia kila hiyo fimbo!
11 It hath. however been given to be furbished that it may be grasped by the hand: The same is a sword sharpened. Yea the same, is furbished, Ready to be given into the hand of the slayer.
Hivyo upanga utatolewa kwa ajili ya kusuguliwa, na kisha kushikika kwa mkono! Upanga umechongwa na umesuguliwa na utatolewa kwenye mkono wa yule auaye!'
12 Make an outcry and howl son of man, For the same hath come against my people, the same is against all the princes of Israel, - Who are thrown to the sword with my people, Therefore smite thou upon thy thigh.
Ita msaada na omboleza, mwanadamu! Kwa kuwa upanga umekuja juu ya watu wangu! Uko juu ya wakuu wote wa Israeli. Wametolewa dhidi ya upanga pamoja na watu wangu. Kwa hiyo, piga paja lako!
13 For trial hath been made, What then, even though the royal rod despiseth, shall it not be? Demandeth My Lord. Yahweh.
Kwa kuwa kuna kujaribiwa, lakini itakuwaje kama fimbo ya kifalme haitakuwepo tena? -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
14 Thou, therefore, son of man, Prophesy, and smite thy hands together, And let the sword smite twice thrice the sword of the slain! the same is the great sword of the slain, that which hemmeth them in.
Basi wewe, mwanadamu, tabiri, na piga makofi, kwa kuwa upanga utakushambulia hata mara tatu! Upanga kwa wale watakaochinjwa! Utakuwa upanga kwa ajili ya kuchinjia, ukiwatoboa pande zote!
15 That the heart may melt And the overthrow be multiplied at all their gates, I have recompensed a slaying by the sword: Surely it hath been made ready to flash like lightning, keen for slaughter.
Ili kuyeyusha mioyo yao na kuongeza kuanguka kwao, nimeweka machinjio ya upanga juu ya malango! Ole! Umeundwa kama mng'ao wa radi, umetengwa kwa ajili ya kuua!
16 One firm stroke to the right. Turn to the left, - Whithersoever thine edge is directed,
Wewe, upanga! Nyooka upande wa kuume! Nyooka upande wa kushoto! Nenda popote ulipoelekeza uso wako.
17 Yea even I myself, will smite my hands together, And will cause mine indignation to find rest, — I Yahweh, have spoken.
Kwa kuwa pia nitapiga mikono yangu miwili kwa pamoja (makofi), na kisha nitaleta ghadhabu yangu kwa waliobakia! Mimi, Yahwe, nimesema hivi!”
18 Then came the word of Yahweh unto me saying:
Neno la Yahwe likanijia tena, kusema,
19 Thou, therefore son of man. Appoint thee two ways For the sword of the king of Babylon to enter, Out of one land shall those two ways come, — And a hand, engrave thou, At the head of the way to the city, engrave it.;
“Sasa wewe, mwanadamu, teua njia mbili kwa ajili ya upanga wa mfalme wa Babeli upate kuja. Njia hizo mbili zitaanza katika nchi moja, na kibao cha barabarani kitamwonyesha mmoja wao kama kuuelekea mji.
20 A way, shalt thou appoint, for the sword to enter. Even to Rabbah of the sons of Ammon, — And to Judah against Jerusalem, the defenced,
Onyesha njia moja kwa ajili ya jeshi la Wababeli kuja Raba, mji wa Waamoni. Onyesha nyingine kuelekea jeshi la Yuda na mji wa Yerusalemu, ambayo imeimarishwa.
21 For the king of Babylon, hath come to a stand, At the parting of the way At the head of the two ways To divine a divination: He hath shaken with arrows He hath asked of the household gods, He hath inspected the liver.
Kwa kuwa mfalme wa Babeli atasimama kwenye makutano ya barabara, kwenye njia panda, ili kufanya uganga. Alitingisha mishale na kuuliza mwelekeo kutoka kwa sanamu na atalichunguza ini.
22 On his right hand, hath come the divination—Jerusalem! To plant battering-rams To open a hole by breach To lift up the voice with a war-shout, — To plant battering-rams against the gates, To cast up an earth-work To build a siege-wall.
Katika mkono wake wa kuume kutakuwa na dalili kuhusu Yerusalemu, kuweka mitambo ya kubomolea juu ya hiyo, kufungua kinywa chake kupanga kuchinja, kutoa sauti ya vita, kuweka mitambo ya kubomolea juu ya malango, kujenga ngazi, na kusimamisha wima minara ya boma.
23 Though it will become to them a veritably false divination in their eyes, even when bound by oaths to them Yet, he, calling to mind iniquity, [will determine] that it shall be captured.
Itaonekana kuwa ishara isiyofaa katika macho ya wale walio katika Yerusalemu, wale walioapa kiapo kwa Wababeli! Lakini mfalme atawashtaki kwa kuvunja sheria ya mkataba ili kuwabariki!
24 Therefore Thus saith My Lord. Yahweh, Because ye have brought to mind your iniquity, by revealing your transgressions causing your sins to appear in all your doings, - Because ye have brought yourselves to mind By force shall ye be captured.
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Kwa sababu umeuleta uovu wako kwenye kumbukumbu zangu, makosa yenu yatafunuliwa! Dhambi zenu zitaonekana katika matendo yenu yote! Kwa sababu hii utamkumbusha kila mtu mtakamatwa kwa mkono wa adui yenu!
25 Thou therefore, O profane, lawless one, prince of Israel, - Whose day hath come, in a time of final iniquity:
Kama wewe, mchafu na mtawala mwovu wa Israeli, ambaye siku ya hukumu imekuja, na ambaye mda wa kufanya uovu umekoma,
26 Thus, saith My Lord. Yahweh, Remove the turban, And lift off the crown, — This not that, The abased, exalt, And the exalted, abase.
Bwana Yahwe asema hivi kwako: Toa kilemba na vua taji! Mambo hayatakuwa tena kama yalivyokuwa! Kiinue kilicho chini na kiinue kilichoinuka!
27 An overthrow overthrow overthrow, will I make it, — Even this, hath not befallen until the coming of One to whom belongeth the right Then will I bestow it.
Uharibifu! Uharibifu! Nitaiharibu! Haitakuwa tena hadi atakapokuja yeye ambaye ameteuliwa kutekeleza hukumu.
28 Thou, therefore, son of man Prophesy and say, thus, saith My Lord. Yahweh, As to the sons of Ammon and as to their reproach Yea thou shalt say. A sword! a sword! Drawn for slaughter, Furbished, that when it beginneth, it may flash like lightning;
Basi wewe, mwanadamu, tabiri na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi hawa ni watu wa Amoni kuhusiana na ujio wa aibu yao: Upanga, upanga umechirwa! Umenolewa kwa ajili ya kuchinja, hivyo utakuwa kama kimuli muli cha radi!
29 Since they see for thee, false visions, Since they divine for thee lies, To stretch thee upon the necks of them who are the most profaned of lawless ones, Whose day hath come, in a time of final iniquity,
Wakati manabii wameona maono ya uongo juu yako, wakati watakapofanya matambiko kuuijia kwa uongo juu yako, huu upanga utaanguka chini juu ya shingo za mwovu ambao wako karibu kuuawa, ambao siku ya ghadhabu imekuja na ambao mda wa uovu unakaribia kuisha.
30 Put it back into its sheath! In the place where thou wast created In the land of thy nativity, will I judge thee
Rudisha upanga kwenye gala yake. Katika mahali ulipoumbwa, katika nchi ya chimbuko lako, nitakuhukumu!
31 Then will I pour out upon thee mine indignation, With the fire of mine outburst, will I blow upon thee; and will deliver thee up into the hand of brutish men, skilled to destroy.
Nitamwaga hasira yangu juu yako! Nitapuliza upepo wa moto wa ghadhabu juu yako na kukuweka kwenye mkono wa watu wakatili, watu wajuao kuangamiza!
32 For the fire, shalt thou serve as fuel, Thy blood shall be in the midst of the land, - Thou shalt not be remembered, For I, Yahweh, have spoken.
Utakuwa kuni kwa ajili ya moto! Damu yako itakuwa kati ya nchi. Hutakumbukwa tena, kwa kuwa mimi, Yahwe nimesema hivi!”'

< Ezekiel 21 >