< Hosea 7 >

1 When I would have brought healing to Israel, then was disclosed the iniquity of Ephraim, and the wicked doings of Samaria, for they have wrought falsehood, —when, a thief, would enter, a band roamed about, outside,
Wakati wowote ninapotaka kuponya Israeli, dhambi ya Efraimu inafunuliwa, pamoja na matendo maovu ya Samaria, kwa sababu wanafanya udanganyifu; mwizi huingia, na kundi la wanyang'anyi hushambulia mitaani.
2 And they say not to their own hearts, that, all their wickedness, I remember, now, have their doings, beset them about, right before my face, have they been done.
Hawatambui mioyoni mwao kwamba ninakumbuka matendo yao mabaya. Sasa matendo yao huwazunguka; yapo mbele ya uso wangu.
3 By their wickedness, they gladden a king, and, by their flatteries, —rulers.
Kwa sababu ya uovu wao wamemfanya mfalme awe na furaha, na maofisa wao kwa uongo wao.
4 They all, are adulterers, like an oven too hot for the baker, —who leaveth off stoking, after kneading the dough, till the whole be leavened.
Wote ni wazinzi, kama tanuru iliyochomwa na mwokaji, ambaye huacha kuuchochea moto tangu kukanda unga mpaka kuwa chachu.
5 In the day of our king, the rulers, have made themselves ill, with the heat of wine, —he hath extended his hand with scoffers.
Siku ya mfalme wetu, viongozi walijifanya wagonjwa na ukali wa divai. Alinyoosha mkono wake kwa wale waliokuwa wakidhihaki.
6 For they have made ready, like an oven, their heart, by their lying in wait, —all the night, their baker sleepeth, in the morning, he, kindleth up as it were a blazing fire.
kwa mioyo kama tanuri, wao hupanga mipango yao ya udanganyifu. Hasira zao hulala usiku wote; asubuhi huwaka juu kama moto.
7 They all, become hot as an oven, and devour their judges, —all their kings, have fallen, there hath been none among them crying unto me.
Wote wamepata moto kama tanuru, na huwaangamiza wale wanaowatawala. Wafalme wao wote wameanguka; hakuna hata mmoja wao ananiita.
8 As for Ephraim! with the peoples, hath he been mingling himself, —Ephraim, is a cake not turned.
Efraimu anajichanganya mwenyewe kati ya watu. Efraimu ni mkate ambayo haujawahi kugeuzwa.
9 Foreigners have, eaten up, his strength, and, he, knoweth it not, —even gray hairs, are sprinkled upon him, and, he, knoweth it not.
Wageni wamekula nguvu zake, lakini hajui. Nywele za mvi hunyunyiza juu yake, lakini hajui.
10 Therefore doth the Excellency of Israel, answer, to his face; yet have they not returned unto Yahweh their God, nor have they sought him, in spite of all this!
Kiburi cha Israeli kinawashuhudia; hata hivyo, hawajarudi kwa Bwana, Mungu wao, wala hawakumtafuta licha ya hayo yote.
11 So then, Ephraim, hath become, like a simple dove, having no understanding, on Egypt, have they called, to Assyria, have they gone,
Efraimu ni kama njiwa, baradhuli na asiye na busara, humwita kwenda Misri, kisha huruka kwenda Ashuru.
12 Whithersoever they go, I will spread over them my net, like a bird of the heavens, will I bring them down, I will chastise them, by the time the report can reach the flock of them.
Wakienda, nitasambaza wavu wangu juu yao, nami nitawaangusha kama ndege wa angani. Nitawaadhibu katika kusonga kwao pamoja.
13 Woe to them! for they have taken flight from me, destruction to them! for they have transgressed against me, —when, I, would have ransomed them, then, they, spake—concerning me—falsehoods.
Ole wao! Kwa maana wamepotea kutoka kwangu. Uharibifu unawajia! Wao wameasi dhidi yangu! Napenda kuwaokoa, lakini waliongea uongo dhidi yangu.
14 Neither made they outcry unto me, in their heart, although they kept on howling upon their beds, over corn and new wine, they gathered themselves together, they rebelled against me.
Wala hawakunililia kwa moyo wao wote, lakini wanaomboleza kwenye vitanda vyao. Wanakusanyika kwa ajili ya nafaka na divai mpya, nao wananiasi mimi.
15 When, I, had warned them, I strengthened their arm, —yet, against me, kept they on devising wickedness.
Ingawa niliwafundisha na kuimarisha mikono yao, sasa wanapanga mabaya dhidi yangu.
16 They would return—not to him who is on high! They have become like a deceitful bow, their rulers, shall fall by the sword, for the rage of their tongue, this, [shall be] their derision in the land of Egypt.
Wanarudi, lakini harudi kwangu, Niliye Juu. Wao ni kama upinde usiotumainika. Maofisa wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya udhalimu wa vinywa. Hii itakuwa ni aibu yao katika nchi ya Misri.

< Hosea 7 >