< Luke 4 >

1 And, Jesus, full of Holy Spirit, returned from the Jordan, and was led in the Spirit in the desert,
Yesu alitoka katika mto Yordani akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akaongozwa na Roho mpaka jangwani.
2 forty days, —being tempted by the adversary; and he did eat nothing in those days, —and, when they were concluded, he hungered.
Huko alijaribiwa na Ibilisi kwa muda wa siku arubaini. Wakati huo wote hakula chochote, na baada ya siku hizo akasikia njaa.
3 And the adversary said to him—If thou art God’s, Son, speak unto this stone; that it become bread.
Ndipo Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”
4 And Jesus made answer unto him—It is written: Not, on bread alone, shall, man, live.
Yesu akamjibu, “Imeandikwa: Mtu haishi kwa mkate tu.”
5 And, leading him up, he shewed him all the kingdoms of the inhabited earth, in a moment of time.
Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,
6 And the adversary said to him—Unto thee, will I give this authority, all together, and their glory; because, unto me, hath it been delivered up, and, to whomsoever I please, I give it:
“Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza.
7 Thou, therefore, if thou wilt worship before me, it shall all, be thine.
Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu.”
8 And, answering, Jesus said to him—It is written: The Lord thy God, shalt thou worship, and, unto him alone, render divine service.
Yesu akamjibu, “Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake.”
9 And he led him into Jerusalem, and set him upon the pinnacle of the temple, —and said [to him]—If thou art God’s, Son, cast thyself, from hence, down;
Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu,
10 for it is written—Unto his messengers, will he give command concerning thee, to keep vigilant watch over thee, —
kwa maana imeandikwa: Atawaamuru malaika wake wakulinde,
11 And, On hands, will they take thee up, lest once thou strike, against a stone, thy foot.
na tena, Watakuchukua mikononi mwao usije ukajikwaa mguu wako kwenye jiwe.”
12 And Jesus, answering, said to him—It is said: Thou shalt not put to the test the Lord thy God.
Lakini Yesu akamjibu, “Imeandikwa: Usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 And, having concluded every temptation, the adversary departed from him until a fitting season.
Ibilisi alipokwishamjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.
14 And Jesus returned, in the power of the Spirit, into Galilee; and, a report, went out along the whole of the region, concerning him;
Yesu alirudi Galilaya akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, na habari zake zikaenea katika sehemu zote za jirani.
15 and, he, began teaching in their synagogues, being glorified by all.
Naye akawa anawafundisha watu katika masunagogi yao, akasifiwa na wote.
16 And he came into Nazareth, where he had been brought up, and entered, according to his custom, on the sabbath day, into the synagogue, —and stood up to read.
Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi, kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.
17 And there was handed to him a scroll of the prophet Isaiah; and unfolding the scroll, he found the place where it was written:
Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:
18 The Spirit of the Lord, is upon me, because he hath anointed me—to tell glad tidings unto the destitute; He hath sent me forth, —To proclaim, to captives, a release, and, to the blind, a recovering of sight, —to send away the crushed, with a release;
“Roho wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema. Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa,
19 To proclaim the welcome year of the Lord.
na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana.”
20 And, folding up the scroll, he handed it to the attendant, and sat down; and, the eyes of all, in the synagogue, were intently fixed upon him;
Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
21 and he began to be saying to them—This day, is fulfilled this scripture, in your ears.
Naye akaanza kuwaambia, “Andiko hili mlilosikia likisomwa, limetimia leo.”
22 And, all, were bearing witness to him, and marvelling at the words of favour which were proceeding out of his mouth; and they were saying—Is not, this, the, son of Joseph?
Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakanena, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”
23 And he said unto them—By all means, ye will speak to me this similitude: Physician! heal, thyself, —Whatsoever things we have heard of coming to pass in Capernaum, do here also, in thine own country.
Naye akawaambia, “Bila shaka mtaniambia msemo huu: Mganga jiponye mwenyewe, na pia mtasema: Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye hapa pia katika kijiji chako.”
24 And he said—Verily, I say unto you, No prophet, is, welcome, in his own country,
Akaendelea kusema, “Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi katika kijiji chake.
25 And, of a truth, I say unto you—Many widows, were in the days of Elijah, in Israel, when the heaven was shut up three years and six months, when there came a great famine upon all the land;
Lakini, sikilizeni! Kweli kulikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli nyakati za Eliya. Wakati huo mvua iliacha kunyesha kwa muda wa miaka mitatu na nusu; kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 And, unto none of them, was Elijah sent, save unto Sarepta of Sidonia, unto a woman that was a widow.
Hata hivyo, Eliya hakutumwa kwa mjane yeyote ila kwa mwanamke mjane wa Sarepta, Sidoni.
27 And, many lepers, were in Israel, in the time of Elisha the prophet, and, not one of them, was cleansed, save Naaman the Syrian.
Tena, katika nchi ya Israeli nyakati za Elisha kulikuwa na wenye ukoma wengi. Hata hivyo, hakuna yeyote aliyetakaswa ila tu Naamani, mwenyeji wa Siria.”
28 And all were filled with wrath, in the synagogue, as they heard these things.
Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana.
29 And, rising up, they thrust him forth outside the city, and led him as far as a brow of the hill on which their city was built, —so that they might throw him down headlong.
Wakasimama, wakamtoa nje ya mji wao uliokuwa umejengwa juu ya kilima, wakampeleka mpaka kwenye ukingo wa kilima hicho ili wamtupe chini.
30 But, he, passing through the midst of them, went his way.
Lakini Yesu akapita katikati yao, akaenda zake.
31 And he came down into Capernaum, a city of Galilee. And he was teaching them on the sabbath;
Kisha Yesu akashuka mpaka Kafarnaumu katika mkoa wa Galilaya, akawa anawafundisha watu siku ya Sabato.
32 and they were being struck with astonishment at his teaching, because, with authority, was his word.
Wakastaajabia uwezo aliokuwa nao katika kufundisha.
33 And, in the synagogue, was a man having a spirit of an impure demon; and he cried out with a loud voice—
Na katika lile sunagogi kulikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na roho ya pepo mchafu; akapiga ukelele wa kuziba masikio:
34 Let be! What have we in common with thee, O Jesus, Nazarene! Hast thou come to destroy us? I know thee, who thou art, —The Holy One of God.
“We! Yesu wa Nazareti! Kwa nini unatuingilia? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakufahamu wewe ni nani. Wewe ni mjumbe Mtakatifu wa Mungu!”
35 And Jesus rebuked it, saying—Hold thy peace! and go forth from him. And the demon, throwing him into the midst, went forth from him, doing him no hurt.
Lakini Yesu akamkemea huyo pepo akisema: “Nyamaza! Mtoke mtu huyu!” Basi, huyo pepo baada ya kumwangusha yule mtu chini, akamtoka bila kumdhuru hata kidogo.
36 And amazement came upon all, and they began to converse one with another, saying—What is this word, that, with authority and power, he giveth orders unto the impure spirits, and they go forth?
Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, “Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!”
37 And a noise concerning him began to go out into every place of the country around.
Habari zake zikaenea mahali pote katika mkoa ule.
38 And, rising up, from the synagogue, he went into the house of Simon. Now, the mother-in-law of Simon, was in distress with a great fever; and they made request to him concerning her.
Yesu alitoka katika lile sunagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa na homa kali; wakamwomba amponye.
39 And, standing over her, he rebuked the fever, and it left her; and, instantly arising, she began to minister unto them.
Yesu akaenda akasimama karibu naye, akaikemea ile homa, nayo ikamwacha. Mara yule mama akainuka, akawatumikia.
40 But, as the sun was going in, they one and all, as many as had any sick with divers diseases, brought them unto him; and, he, upon each one of them laying, his hands, was curing them.
Jua lilipokuwa linatua, wote waliokuwa na wagonjwa wao mbalimbali waliwaleta kwake; naye akaweka mikono yake juu ya kila mmoja wao, akawaponya wote.
41 And demons also were going forth from many; crying aloud, and saying—Thou, art the Son of God. And, rebuking them, he suffered them not be talking; because they knew him to be, The Christ.
Pepo waliwatoka watu wengi, wakapiga kelele wakisema: “Wewe u Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea, wala hakuwaruhusu kusema, maana walimfahamu kwamba yeye ndiye Kristo.
42 And, when it was day, going forth, he journeyed into a desert place; and, the multitudes, were seeking after him, and they came unto him, and would have detained him, that he might not depart from them.
Kesho yake asubuhi Yesu aliondoka akaenda mahali pa faragha. Watu wakawa wanamtafuta, na walipofika mahali alipokuwa, wakajaribu kumzuia ili asiondoke kwao.
43 But, he, said unto them—To the other cities also, I must needs tell the good-news of the kingdom of God, because, hereunto, was I sent forth.
Lakini yeye akawaambia, “Ninapaswa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, maana nilitumwa kwa ajili hiyo.”
44 And he was proclaiming in the cities of Judaea.
Akawa anahubiri katika masunagogi ya Yudea.

< Luke 4 >