< 2 Chronicles 35 >

1 and to make: do Josiah in/on/with Jerusalem Passover to/for LORD and to slaughter [the] Passover in/on/with four ten to/for month [the] first
Yosia akaadhimisha Pasaka kwa Bwana katika Yerusalemu, mwana-kondoo wa Pasaka akachinjwa siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza.
2 and to stand: appoint [the] priest upon charge their and to strengthen: strengthen them to/for service: ministry house: temple LORD
Akawaweka makuhani kwenye wajibu wao na kuwatia moyo katika utumishi wa Hekalu la Bwana.
3 and to say to/for Levi ([the] to understand *QK) to/for all Israel [the] holy to/for LORD to give: put [obj] ark [the] holiness in/on/with house: home which to build Solomon son: child David king Israel nothing to/for you burden in/on/with shoulder now to serve: minister [obj] LORD God your and [obj] people his Israel
Akawaambia Walawi, waliowafundisha Waisraeli wote na waliokuwa wamejiweka wakfu kwa ajili ya kazi ya Bwana, “Liwekeni hilo Sanduku takatifu katika Hekalu lile alilojenga Solomoni mwana wa Daudi mfalme wa Israeli. Halipaswi kubebwa huku na huko mabegani mwenu. Sasa mtumikieni Bwana Mungu wenu na watu wake Israeli.
4 (and to establish: prepare *QK) to/for house: household father your like/as division your in/on/with writing David king Israel and in/on/with writing Solomon son: child his
Jiandaeni kwa kufuata jamaa zenu katika migawanyo yenu, kufuatana na maelezo yaliyoandikwa na Daudi mfalme wa Israeli na mwanawe Solomoni.
5 and to stand: stand in/on/with Holy Place to/for division house: household [the] father to/for brother: compatriot your son: descendant/people [the] people and division house: household father to/for Levi
“Simameni mahali patakatifu kwa kufuata migawanyo ya jamaa za baba zenu kulingana na koo zenu na pawepo Walawi kwa ajili ya kila mgawanyo wa nyumba ya baba zenu.
6 and to slaughter [the] Passover and to consecrate: consecate and to establish: prepare to/for brother: compatriot your to/for to make: do like/as word LORD in/on/with hand: by Moses
Chinjeni mwana-kondoo wa Pasaka, jitakaseni, nanyi kwa niaba ya koo zenu fanyeni maandalizi, mkitenda sawasawa na neno la Bwana kwa mkono wa Mose.”
7 and to exalt Josiah to/for son: descendant/people [the] people flock lamb and son: young animal goat [the] all to/for Passover to/for all [the] to find to/for number thirty thousand and cattle three thousand these from property [the] king
Ndipo Yosia akawapa watu wote wana-mbuzi waliokuwepo jumla ya kondoo wapatao 30,000 kwa ajili ya sadaka ya Pasaka, pia na ngʼombe 10,000, vyote hivi kutoka mali binafsi ya mfalme.
8 and ruler his to/for voluntariness to/for people to/for priest and to/for Levi to exalt Hilkiah and Zechariah and Jehiel leader house: temple [the] God to/for priest to give: give to/for Passover thousand and six hundred and cattle three hundred
Pia maafisa wake, wakatoa kwa hiari yao wakawapa watu, makuhani na Walawi. Hilkia, Zekaria na Yehieli, waliokuwa maafisa wakuu wa Hekalu la Mungu, wakawapa makuhani sadaka za Pasaka wana-kondoo na wana-mbuzi 2,600 na mafahali 300.
9 (and Conaniah *Qk) and Shemaiah and Nethanel brother: male-sibling his and Hashabiah and Jeiel and Jozabad ruler [the] Levi to exalt to/for Levi to/for Passover five thousand and cattle five hundred
Konania na nduguze wawili, Shemaya na Nethaneli, pamoja na Hashabia, Yeieli na Yozabadi waliokuwa viongozi wa Walawi, nao pia wakawapa Walawi wana-kondoo na wana-mbuzi 5,000 na mafahali 500, kwa ajili ya sadaka za Pasaka.
10 and to establish: prepare [the] service and to stand: stand [the] priest upon post their and [the] Levi upon division their like/as commandment [the] king
Huduma ilipomalizika kuandaliwa makuhani wakasimama mahali pao na Walawi katika migawanyo yao kama mfalme alivyokuwa ameamuru.
11 and to slaughter [the] Passover and to scatter [the] priest from hand: themselves their and [the] Levi to strip
Wana-kondoo wa Pasaka wakachinjwa, nao makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa, wakati Walawi wakiwa wanawachuna wale wanyama ngozi.
12 and to turn aside: turn aside [the] burnt offering to/for to give: give them to/for division to/for house: household father to/for son: descendant/people [the] people to/for to present: bring to/for LORD like/as to write in/on/with scroll: book Moses and so to/for cattle
Wakatenga sadaka za kuteketezwa ili waweze kugawia ili migawanyo kwa kufuata jamaa za baba zao ili watoe sadaka kwa Bwana kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose. Wakafanya vivyo hivyo kwa wale mafahali.
13 and to boil [the] Passover in/on/with fire like/as justice: judgement and [the] holiness to boil in/on/with pot and in/on/with pot and in/on/with pot and to run: run to/for all son: descendant/people [the] people
Wakawaoka wale wanyama wa Pasaka kwenye moto kama ilivyoamriwa, wakachemsha zile sadaka takatifu kwenye vyungu, masufuria makubwa na vikaango na kuwagawia watu wote upesi.
14 and after to establish: prepare to/for them and to/for priest for [the] priest son: descendant/people Aaron in/on/with to ascend: offer up [the] burnt offering and [the] fat till night and [the] Levi to establish: prepare to/for them and to/for priest son: descendant/people Aaron
Hatimaye wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani, kwa sababu wale makuhani, yaani, wazao wa Aroni, walikuwa wanatoa sadaka za kuteketezwa pamoja na zile sehemu zilizonona mpaka usiku. Hivyo Walawi wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Aroni.
15 and [the] to sing son: descendant/people Asaph upon office their like/as commandment David and Asaph and Heman and Jeduthun seer [the] king and [the] gatekeeper to/for gate and gate nothing to/for them to/for to turn aside: depart from upon service their for brother: male-relative their [the] Levi to establish: prepare to/for them
Waimbaji, wazao wa Asafu, walikuwa katika nafasi zao, kama ilivyoagizwa na Mfalme Daudi, Asafu, Hemani na Yeduthuni mwonaji wa Mfalme. Mabawabu katika kila lango hawakuhitaji kuacha nafasi zao kwa sababu Walawi wenzao walifanya maandalizi kwa ajili yao.
16 and to establish: prepare all service: ministry LORD in/on/with day [the] he/she/it to/for to make: do [the] Passover and to ascend: offer up burnt offering upon altar LORD like/as commandment [the] king Josiah
Kwa hiyo wakati ule huduma yote ya Bwana ilifanyika katika kuadhimisha Pasaka, kutoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana kama alivyoamuru Mfalme Yosia.
17 and to make: do son: descendant/people Israel [the] to find [obj] [the] Passover in/on/with time [the] he/she/it and [obj] feast [the] unleavened bread seven day
Waisraeli waliokuwepo wakaadhimisha Pasaka wakati huo na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa siku saba.
18 and not to make: do Passover like him in/on/with Israel from day Samuel [the] prophet and all king Israel not to make: do like/as Passover which to make: do Josiah and [the] priest and [the] Levi and all Judah and Israel [the] to find and to dwell Jerusalem
Kulikuwa hakujafanyika Pasaka kama hii katika Israeli tangu siku za nabii Samweli wala hakukuwa na mfalme yeyote wa Israeli ambaye kamwe alishaadhimisha Pasaka kama ile aliyofanya Mfalme Yosia, akiwa na makuhani, Walawi na watu wote wa Yuda na watu wa Israeli waliokuwepo huko, pamoja na watu wa Yerusalemu.
19 in/on/with eight ten year to/for royalty Josiah to make: do [the] Passover [the] this
Pasaka iliadhimishwa katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia.
20 after all this which to establish: prepare Josiah [obj] [the] house: home to ascend: rise Neco king Egypt to/for to fight in/on/with Carchemish upon Euphrates and to come out: come to/for to encounter: meet him Josiah
Baada ya haya yote, Yosia alipomaliza kulitengeneza vizuri Hekalu, Neko mfalme wa Misri, akapanda ili kupigana huko Karkemishi katika Mto Frati, naye Yosia akatoka kwenda kupigana naye.
21 and to send: depart to(wards) him messenger to/for to say what? to/for me and to/for you king Judah not upon you you(m. s.) [the] day: today for to(wards) house: home battle my and God to say to/for to dismay me to cease to/for you from God which with me and not to ruin you
Lakini Neko akamtumia wajumbe kusema, “Kuna ugomvi gani kati yangu mimi na wewe, Ee Mfalme wa Yuda? Si wewe ninayekushambulia wakati huu, bali ile nyumba ambayo nina vita nayo, Mungu ameniambia niharakishe, kwa hivyo acha kumpinga Mungu, ambaye yuko pamoja nami, la sivyo atakuangamiza.”
22 and not to turn: turn Josiah face: before his from him for to/for to fight in/on/with him to search and not to hear: hear to(wards) word Neco from lip God and to come (in): come to/for to fight in/on/with valley Megiddo
Lakini hata hivyo, Yosia hakukubali kumwacha, bali alijibadilisha ili kupigana naye vita. Hakusikiliza yale Neko aliyokuwa amemwambia kwa agizo la Mungu bali alikwenda kupigana naye katika tambarare ya Megido.
23 and to shoot [the] to shoot to/for king Josiah and to say [the] king to/for servant/slave his to pass: bring me for be weak: ill much
Wapiga upinde wakampiga Mfalme Yosia, naye akawaambia maafisa wake, “Niondoeni, nimejeruhiwa vibaya sana.”
24 and to pass: bring him servant/slave his from [the] chariot and to ride him upon chariot [the] second which to/for him and to go: take him Jerusalem and to die and to bury in/on/with grave father his and all Judah and Jerusalem to mourn upon Josiah
Kwa hiyo wakamshusha kutoka kwenye gari lake la farasi, wakamweka kwenye gari lingine alilokuwa nalo na kumleta Yerusalemu, ambako alifia. Akazikwa katika makaburi ya baba zake, nayo Yuda yote na Yerusalemu wakamwombolezea Yosia.
25 and to chant Jeremiah upon Josiah and to say all [the] to sing and [the] to sing in/on/with dirge their upon Josiah till [the] day: today and to give: make them to/for statute: decree upon Israel and look! they to write upon [the] dirge
Nabii Yeremia akatunga maombolezo kwa ajili ya kifo chake, nao waimbaji wote, wanaume kwa wanawake, hufanya ukumbusho wa Yosia katika maombolezo hadi leo. Haya yakafanywa desturi katika Israeli, nayo yameandikwa katika Maombolezo.
26 and remainder word: deed Josiah and kindness his like/as to write in/on/with instruction LORD
Matukio mengine ya utawala wa Yosia na matendo yake mema, kulingana na yale yaliyoandikwa katika sheria ya Bwana:
27 and word: deed his [the] first and [the] last look! they to write upon scroll: book king Israel and Judah
matukio yote, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.

< 2 Chronicles 35 >