< Exodus 18 >

1 and to hear: hear Jethro priest Midian relative Moses [obj] all which to make: do God to/for Moses and to/for Israel people his for to come out: send LORD [obj] Israel from Egypt
Basi Yethro, kuhani wa Midiani, baba mkwe wa Mose, akawa amesikia kila kitu Mungu alichomfanyia Mose na watu wake wa Israeli, pia jinsi Bwana alivyowatoa Israeli Misri.
2 and to take: take Jethro relative Moses [obj] Zipporah woman: wife Moses after parting gift her
Baada ya Mose kumrudisha mkewe Sipora, Yethro baba mkwe wake alimpokea
3 and [obj] two son: child her which name [the] one Gershom for to say sojourner to be in/on/with land: country/planet foreign
pamoja na wanawe wawili. Jina la mmoja aliitwa Gershomu, kwa kuwa Mose alisema, “Nimekuwa mgeni katika nchi ya kigeni.”
4 and name [the] one Eliezer for God father my in/on/with helper my and to rescue me from sword Pharaoh
Mwingine aliitwa Eliezeri, kwa kuwa alisema, “Mungu wa baba yangu alikuwa msaada wangu, akaniokoa kutoka upanga wa Farao.”
5 and to come (in): come Jethro relative Moses and son: child his and woman: wife his to(wards) Moses to(wards) [the] wilderness which he/she/it to camp there mountain: mount [the] God
Yethro, baba mkwe wa Mose, pamoja na wana wawili wa Mose na mkewe, wakamjia Mose huko jangwani, mahali alipokuwa amepiga kambi karibu na mlima wa Mungu.
6 and to say to(wards) Moses I relative your Jethro to come (in): come to(wards) you and woman: wife your and two son: child her with her
Yethro alikuwa ametuma ujumbe kwake Mose, kusema, “Mimi Yethro baba mkwe wako ninakuja kwako pamoja na mke wako na wanao wawili.”
7 and to come out: come Moses to/for to encounter: meet relative his and to bow and to kiss to/for him and to ask man: anyone to/for neighbor his to/for peace: well-being and to come (in): come [the] tent [to]
Kwa hiyo Mose akatoka kumlaki baba mkwe wake, akainama na kumbusu. Wakasalimiana, kisha wakaingia hemani.
8 and to recount Moses to/for relative his [obj] all which to make: do LORD to/for Pharaoh and to/for Egypt upon because Israel [obj] all [the] hardship which to find them in/on/with way: journey and to rescue them LORD
Mose akamwambia baba mkwe wake kuhusu kila kitu Bwana alichomfanyia Farao na Wamisri kwa ajili ya Israeli, na pia kuhusu shida zote walizokutana nazo njiani na jinsi Bwana alivyowaokoa.
9 and to rejoice Jethro upon all [the] welfare which to make: do LORD to/for Israel which to rescue him from hand: power Egypt
Yethro akafurahishwa sana kusikia juu ya mambo yote mazuri Bwana aliyowatendea Waisraeli kuwaokoa kutoka mkono wa Wamisri.
10 and to say Jethro to bless LORD which to rescue [obj] you from hand: owner Egypt and from hand: owner Pharaoh which to rescue [obj] [the] people from underneath: owning hand: owner Egypt
Yethro akasema, “Sifa na ziwe kwa Bwana, aliyekuokoa wewe kutoka mikononi mwa Wamisri na Farao, na aliyewaokoa watu kutoka mikononi mwa Wamisri.
11 now to know for great: large LORD from all [the] God for in/on/with word: because which to boil upon them
Sasa najua ya kuwa Bwana ni mkuu kuliko miungu mingine yote, kwa kuwa amewatendea hivi wale waliowatenda Israeli kwa ujeuri.”
12 and to take: bring Jethro relative Moses burnt offering and sacrifice to/for God and to come (in): come Aaron and all old: elder Israel to/for to eat food: bread with relative Moses to/for face: before [the] God
Kisha Yethro, baba mkwe wa Mose, akaleta sadaka ya kuteketezwa na dhabihu nyingine kwa Mungu, naye Aroni pamoja na wazee wote wa Israeli wakaja kula chakula pamoja na baba mkwe wa Mose mbele za Mungu.
13 and to be from morrow and to dwell Moses to/for to judge [obj] [the] people and to stand: stand [the] people upon Moses from [the] morning till [the] evening
Siku iliyofuata, Mose akachukua nafasi yake kama hakimu wa watu, nao wakasimama kumzunguka kuanzia asubuhi hadi jioni.
14 and to see: see relative Moses [obj] all which he/she/it to make: do to/for people and to say what? [the] word: thing [the] this which you(m. s.) to make: do to/for people why? you(m. s.) to dwell to/for alone you and all [the] people to stand upon you from morning till evening
Baba mkwe wake alipoona yote Mose anayowafanyia watu, akasema, “Ni nini hiki unachowafanyia watu? Kwa nini wewe unakuwa mwamuzi wa watu hawa peke yako, wakati watu hawa wamesimama wakikuzunguka tangu asubuhi mpaka jioni?”
15 and to say Moses to/for relative his for to come (in): come to(wards) me [the] people to/for to seek God
Mose akamjibu, “Kwa sababu watu wananijia kutaka mapenzi ya Mungu.
16 for to be to/for them word: case to come (in): come to(wards) me and to judge between man: anyone and between neighbor his and to know [obj] statute: decree [the] God and [obj] instruction his
Kila wakiwa na shauri huletwa kwangu, nami huamua kati ya mtu na mwenzake na kuwajulisha juu ya amri na sheria za Mungu.”
17 and to say relative Moses to(wards) him not pleasant [the] word: thing which you(m. s.) to make: do
Baba mkwe wa Mose akamjibu, “Unachofanya sio kizuri.
18 to wither to wither also you(m. s.) also [the] people [the] this which with you for heavy from you [the] word: thing not be able to make: do him to/for alone you
Wewe pamoja na watu hawa wanaokujia mtajichosha bure. Kazi ni nzito sana kwako, huwezi kuibeba mwenyewe.
19 now to hear: obey in/on/with voice my to advise you and to be God with you to be you(m. s.) to/for people opposite [the] God and to come (in): bring you(m. s.) [obj] [the] word: case to(wards) [the] God
Sasa nisikilize mimi, nitakupa shauri, naye Mungu na awe pamoja nawe. Yapasa wewe uwe mwakilishi wa watu mbele za Mungu na ulete mashauri yao kwake.
20 and to warn [obj] them [obj] [the] statute: decree and [obj] [the] instruction and to know to/for them [obj] [the] way: conduct to go: walk in/on/with her and [obj] [the] deed: work which to make: do [emph?]
Uwafundishe amri na sheria, tena uwaonyeshe namna ya kuishi na kazi zinazowapasa wao kufanya.
21 and you(m. s.) to see from all [the] people human strength afraid God human truth: faithful to hate unjust-gain and to set: put upon them ruler thousand ruler hundred ruler fifty and ruler ten
Lakini uchague watu wenye uwezo miongoni mwa watu wote, watu wanaomwogopa Mungu, watu waaminifu wanaochukia mali ya dhuluma, uwateuwe wawe maafisa juu ya maelfu, mamia, hamsini na makumi.
22 and to judge [obj] [the] people in/on/with all time and to be all [the] word: thing [the] great: large to come (in): bring to(wards) you and all [the] word: thing [the] small to judge they(masc.) and to lighten from upon you and to lift: bear with you
Waweke wawe waamuzi wa watu kwa wakati wote, lakini waambie wakuletee kila shauri lililo gumu; yale yaliyo rahisi wayaamue wao wenyewe. Hii itafanya mzigo wako kuwa mwepesi, kwa sababu watashirikiana nawe.
23 if [obj] [the] word: thing [the] this to make: do and to command you God and be able to stand: stand and also all [the] people [the] this upon place his to come (in): come in/on/with peace
Kama ukifanya hivi, na ikiwa Mungu ameagiza hivyo, utaweza kushinda uchovu, nao watu hawa wote watarudi nyumbani wameridhika.”
24 and to hear: hear Moses to/for voice relative his and to make: do all which to say
Mose akamsikiliza baba mkwe wake na kufanya kila kitu alichosema.
25 and to choose Moses human strength from all Israel and to give: make [obj] them head: leader upon [the] people ruler thousand ruler hundred ruler fifty and ruler ten
Mose akawachagua watu wenye uwezo kutoka Israeli yote, akawafanya kuwa viongozi wa watu, maafisa juu ya maelfu, mamia, hamsini na makumi.
26 and to judge [obj] [the] people in/on/with all time [obj] [the] word: case [the] severe to come (in): bring [emph?] to(wards) Moses and all [the] word: case [the] small to judge they(masc.)
Wakatumika kama waamuzi wa watu kwa wakati wote. Mashauri magumu wakayaleta kwa Mose, lakini yale yaliyo rahisi wakayaamua wenyewe.
27 and to send: depart Moses [obj] relative his and to go: went to/for him to(wards) land: country/planet his
Kisha Mose akaagana na Yethro baba mkwe wake, naye akarudi kwa nchi yake.

< Exodus 18 >