< Numbers 12 >

1 and to speak: speak Miriam and Aaron in/on/with Moses upon because [the] woman [the] Cushite which to take: marry for woman Cushite to take: marry
Kisha Miriamu na Haruni wakasema kinyume na Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi ambaye alikuwa amemwoa.
2 and to say except surely in/on/with Moses to speak: speak LORD not also in/on/with us to speak: speak and to hear: hear LORD
Walisema. “Hivi BWANA amesema na Musa tu? Ni kweli hajawahi kusema nasi pia? Sasa BWANA akasikia kile walichokuwa wanaongea. Sasa
3 and [the] man Moses (poor *Qk) much from all [the] man which upon face [the] land: planet
Musa alikuwa mtu mpole sana, mpole kuliko mtu yeyote duniani.
4 and to say LORD suddenly to(wards) Moses and to(wards) Aaron and to(wards) Miriam to come out: come three your to(wards) tent meeting and to come out: come three their
Wakati huo, BWANA akanena na Musa, Haruni na Miriamu: “tokeni nje ninyi watatu kwenye hema ya kukutania.” kwa hiyo wale watatu wakatokanje.
5 and to go down LORD in/on/with pillar cloud and to stand: stand entrance [the] tent and to call: call to Aaron and Miriam and to come out: come two their
Kisha BWANA akashuka katika nguzo ya wingu. Akasimama kwenye lango la hema na akamwita Haruni na Miriamu. wote wakaja mbele.
6 and to say to hear: hear please word my if to be prophet your LORD in/on/with vision to(wards) him to know in/on/with dream to speak: speak in/on/with him
BWANA akasema, “Sasa sikilizeni maneo yangu, Nabii wangu anapokuwa nanyi, Mimi nitajifunua kwake kwa maono na kusema naye katika ndoto.
7 not so servant/slave my Moses in/on/with all house: household my be faithful he/she/it
Lakini si hivyo kwa mtumishi wangu Musa. Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote.
8 lip to(wards) lip to speak: speak in/on/with him and appearance and not in/on/with riddle and likeness LORD to look and why? not to fear to/for to speak: speak in/on/with servant/slave my in/on/with Moses
Mimi huongea na Musa moja kwa moja, si kwa maono wala mafumbo. Yeye huniona umbo langu. Kwa hiyo, kwa nini hamuogoopi kumnenea kinyume, mtumishi wangu Musa?”
9 and to be incensed face: anger LORD in/on/with them and to go: went
Hasira ya BWANA ikawawakia, kisha akawaacha.
10 and [the] cloud to turn aside: remove from upon [the] tent and behold Miriam be leprous like/as snow and to turn Aaron to(wards) Miriam and behold be leprous
Lile wingu likainuka juu ya hema, Miriamu akapata ukoma ghafla - akawa mweupe kama theluji. Naye Haruni alipogeuka kumwona Miriamu, akamwona amepata ukoma.
11 and to say Aaron to(wards) Moses please lord my not please to set: accuse upon us sin which be foolish and which to sin
Haruni akamwambia Musa, “Bwana wangu, usituadhibu kwa uovu wetu huu. Tumenena katka upumbuvu, na tumetenda dhambi.
12 not please to be like/as to die which in/on/with to come out: produce he from womb mother his and to eat half flesh his
Tafadhali nakuomba usimwache akawa kama mtoto mchanga aliyekufa ambaye nusu ya nyama yake imeoza tangu kuzaliwa”
13 and to cry Moses to(wards) LORD to/for to say God please to heal please to/for her
Kwa hiyo Musa akamwomba BWANA, akasema, “Mungu ninakusihi umponye tafadhali.”
14 and to say LORD to(wards) Moses and father her to spit to spit in/on/with face her not be humiliated seven day to shut seven day from outside to/for camp and after to gather
BWANA akamwambia Musa, “kama baba yake angemtemea usoni angepata aibu kwa muda wa siku saba. Umfungie nje ya kambi kwa muda wa siku saba. Kisha umrejeshe ndani tena.”
15 and to shut Miriam from outside to/for camp seven day and [the] people not to set out till to gather Miriam
Kwa hiyo Miriamu akafungiwa nje ya kambi kwa siku saba. Watu hawakusafiri mpaka aliporudi kambini.
16 and after to set out [the] people from Hazeroth and to camp in/on/with wilderness Paran
Kisha watu wakasafiri kutoka Hazeroti na kuweka kambi kwenye jangwa la Parani.

< Numbers 12 >