< 2 Chronicles 9 >

1 The queen who ruled [the] Sheba [area in Arabia] heard that Solomon had become famous, so she traveled to Jerusalem to ask him questions that were difficult [to answer]. She came with a large group of servants, and she brought camels that were loaded with spices, and valuable gems, and a lot of gold. When she met Solomon, she asked him questions about all the things/topics in which she was interested.
Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni, huyo malkia akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu. Alifika akiwa na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani, alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
2 Solomon answered all her questions. He explained everything that she asked about, even things that were very difficult.
Solomoni akamjibu maswali yake yote, wala hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwake asiweze kumwelezea.
3 The queen realized that Solomon was very wise. She saw his palace,
Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
4 she saw the food that was served on his table [every day]; she saw how his officials were seated at the table, their uniforms, the servants who served the food and wine, and the sacrifices that he took to the temple to be completely burned on the altar. She was extremely amazed.
chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika Hekalu la Bwana alipatwa na mshangao.
5 She said to the king, “Everything that I heard in my own country about you and about how wise you are is true!
Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
6 But I did not believe it was true until I came here and saw it myself. You are [extremely wise and rich, ] more than what people told me.
Lakini sikuamini yaliyosemwa hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana kuliko ile taarifa niliyoisikia.
7 The men who work for you are very fortunate! Your officials who are constantly standing in front of you and listening to the wise things that you say are also fortunate!
Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
8 Praise Yahweh your God, who has shown that he is pleased with you by appointing you to be the king of Israel for him. God has always loved the Israeli people, and desires to assist them forever, and therefore he has appointed you to be their king, in order that you will rule them fairly and righteously.”
Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe, na akakuweka juu ya kiti chake cha ufalme utawale kwa niaba ya Bwana Mungu wako. Kwa sababu ya upendo wa Mungu wako kwa Israeli na shauku yake ya kuwadhibitisha milele, amekufanya wewe mfalme juu yao, ili kudumisha haki na uadilifu.”
9 Then the queen gave to Solomon about 4-1/2 tons of gold and a large amount of spices and gems. Never had King Solomon received more spices than the queen gave him at that time.
Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa vikolezi vizuri kama vile Malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
10 King Solomon gave to the queen of Sheba everything that she wanted. He gave her more than she had given to him. Then she and those who came with her returned to her own land. [In the ships that belonged to King Hiram, ] Hiram’s workers and Solomon’s workers brought gold from Ophir. They also brought a large amount of juniper wood and gems. King Solomon [told his workers] to use that wood to make railings in the temple and in his palace and also to make harps and lyres for the musicians. That wood was the the finest wood that had ever been seen in Israel.
(Watumishi wa Hiramu na wa Solomoni wakaleta dhahabu kutoka Ofiri, tena wakaleta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
Mfalme akatumia hiyo miti ya msandali kuwa ngazi kwa ajili ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa Yuda tangu siku ile.)
Mfalme Solomoni akampa Malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, zaidi ya vile alivyokuwa amemletea mfalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
13 Each year there was brought to Solomon a total of 25 tons of gold.
Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
14 That was in addition to the [taxes] paid to him by the merchants and traders. Also, the kings of Arabia and the governors of [the districts in] Israel brought gold and silver to Solomon.
mbali na mapato yaliyoletwa na wafanyabiashara na wachuuzi. Wafalme wote wa Arabuni na watawala wa nchi wakamletea Solomoni dhahabu na fedha.
15 King Solomon’s [workers took this] gold [and] hammered [it] into thin sheets and covered 200 large shields with those thin sheets of gold; they put almost 7-1/2 pounds of gold on each shield.
Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa. Kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
16 His [workers] made 300 [smaller] shields. They covered each of them with almost 4 pounds of gold. Then the king put those shields in the Hall of the Forest of Lebanon.
Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
17 His [workers] also made for him a large throne. [Part of] it was covered with [decorations made from] ivory and [part of it was covered] with very fine gold.
Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
18 There were six steps in front of the throne. There was a gold footstool that was attached to the throne. At each side of the throne there was an armrest, and alongside each armrest there was a [small statue of a] lion.
Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na mahali pa kuwekea miguu vyote vya dhahabu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
19 On the six steps there were twelve statues of lions, one on each side. No throne like that had ever existed in any other kingdom.
Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
20 All of Solomon’s cups were made of gold, and all the various dishes in the Hall of the Forest of Lebanon were made of gold. [They did not make things from silver], because during the years that Solomon [ruled], silver was not considered to be valuable.
Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo wakati wa Solomoni.
21 The king had a fleet of ships that sailed with the ships that King Hiram owned. Every three years the ships returned [from the places to which they had sailed], bringing gold, silver, ivory, monkeys, and baboons (OR, peacocks).
Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizoendeshwa na watu wa Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
22 King Solomon became richer and wiser than any other king on the earth.
Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
23 Kings from all over the world wanted to come and listen to the wise things that Solomon said, things that God had enabled him to know.
Wafalme wote wa dunia wakatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
24 All the people who came to him brought presents: They brought things made from silver or gold, or robes, or weapons, or spices, or horses, or mules. The people continued to do this every year.
Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja, alileta zawadi, vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
25 Solomon had 4,000 stalls for his horses and chariots, and 12,000 horses. Solomon put some of them in Jerusalem and some of them in other cities where he kept his chariots.
Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 kwa ajili ya farasi na magari ya vita, farasi 12,000 ambao aliwaweka katika miji ya magari ya vita na katika Yerusalemu pamoja naye.
26 Solomon ruled over all the kings in the area from the [Euphrates] River [in the northeast] to the Philistia area [in the west] to the border of Egypt [in the south].
Solomoni akatawala juu ya wafalme wote kuanzia Mto Frati mpaka kwenye nchi ya Wafilisti na kuendelea hadi mpaka wa Misri.
27 [During the years that Solomon was] king, [he] caused silver to become as common in Jerusalem as stones; and he caused cedar trees in the foothills of Judah to become as plentiful as fig trees.
Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
28 Solomon’s agents brought horses from [the] Musri [area] and other places.
Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka nchi nyingine zote.
29 Lists of all the other things that Solomon did are recorded in the scrolls written by the prophet Nathan and by the prophet Ahijah from Shiloh [city], and in [the scroll in which were written] the visions that the prophet Iddo saw concerning [King] Jeroboam.
Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Nathani, katika unabii wa Ahiya Mshiloni na katika maono ya Ido mwonaji kuhusu Yeroboamu mwana wa Nebati?
30 Solomon ruled from Jerusalem all of Israel for 40 years.
Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
31 Then Solomon died and was buried in [the part of Jerusalem called] ‘The City of David’. And his son Rehoboam became the king.
Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Chronicles 9 >