< Amos 7 >

1 Yahweh our God showed me [in a vision] that he was going to send locusts [to destroy our crops]. It was going to happen right after the king’s share of the hay had been harvested/cut and before the rest of the hay was ready to be harvested.
Hivi ndivyo ambavyo Bwana Yahwe alivyonionyesha. Tazama, aliumba kundi kubwa la nzige wakati wa kuchipuka kwa mmea, na, tazama, ulikuwa ni mmea wa mwisho baada ya mavuno ya mfalme.
2 [And in the vision I saw] those locusts come, and they ate everything that was green. Then I cried out, “Yahweh our Lord, please forgive us! We Israeli people are very helpless; (how will we be able to survive [RHQ]?/we will not be able to survive!)”
Wakati walipomaliza kula mbogamboga za nchi, kisha nikasema, “Bwana Yahwe, tafadhali nisamehe; Je Yakobo ataishije? kwa kuwa yeye ni mdogo sana.”
3 So Yahweh changed his mind and said, “That will not happen.”
Yahwe akapunguza hasira kuhusu hili. “Haitatokea,” akasema.
4 Then this is what Yahweh our Lord showed me [in another vision]: He was calling to a fire to [come and] punish [his people]. [In the vision I saw that] the fire dried up the ocean and also burned [everything on] the land.
Hivi ndivyo ambavyo Bwana Yahwe alivyonionyesha: Tazama, Bwana Yahwe aliita juu ya moto kuhukumu. Nao ukakausha sana, kilindi chini ya dunia na kutaka kuitekeza nchi, pia.
5 Then I cried out again, “Yahweh our Lord, I plead with you, please stop this! We Israeli people are very helpless; how will we be able to survive [RHQ]?”
Lakini nikasema, “Bwana Yahwe, acha tafadhali; Yakobo ataishije? Kwa kuwa yeye ni mdigo sana.”
6 So Yahweh changed his mind again, and said, “That also will not happen.”
Yahwe akagairi kuhusiana na hili, “Hili halitajitokeza pia,” asema Bwana Yahwe.
7 Then Yahweh showed me [another vision]. I saw him standing beside a wall. [It was very straight because] it had been built using a (plumb line/cord with a weight on one end to determine if walls are vertically straight). Yahweh had the plumb line in his hand.
Hivi ndivyo ambavyo Yahwe alivyo nionyesha: Tazama, Bwana amesimama karibu na ukuta, pamoja na uzi wa timiza kwenye mkono wake.
8 Yahweh asked me, “Amos, what do you see?” I replied, “A plumb line.” Then Yahweh said, “Look, I am going to use a plumb line among my Israeli people, [to show that they are like a wall that is not straight]. I will not change my mind again about punishing them.
Yahwe akanambia, “Amosi, unaona nini?” nikasema, “Uzi wa timazi.” Kisha Bwana akasema, “Tazama, nitaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli. Sintowaharibu tena.
9 The places on hills where [the descendants of] [MTY] Isaac worship [idols] will be destroyed. And the other important shrines in Israel will also be destroyed. And I will enable [your enemies] to attack your people with swords and they will get rid of [King] Jeroboam and all his descendants.”
Mahala pa juu pa Isaka pataharibiwa, patakatifu pa Israeli pataangamia, na nitainuka juu ya nyumba ya Yeroboamu kwa upanga.”
10 Then Amaziah, the priest at Bethel, sent [a message] to Jeroboam, the King of Israel. In the message he said, “Amos is plotting against you among the Israeli people [MTY]. [I am worried that] the people of this country will not be able to refute his words.
Kisha Amazia, yule kuhani wa Betheli, akatuma ujumbe kwa Yeroboamu, mfalme wa Israeli: “amosi amefanya njama dhidi yako katikati ya nyumba ya Israeli. Nchi haiwezi kubeba maneno yote haya.
11 This is what he is saying: ‘Jeroboam will soon be killed by [someone using] a sword, and the people of Israel will be (exiled/forced to leave their land and go to another country).’”
Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Amosi, 'Yeroboamu atakufa kwa upanga, na hakika Israeli itakwenda utumwani kutoka nchi yake.”'
12 Then Amaziah [came to me and] said, “You prophet, get out of here! Go back to the country of Judah! Earn money to [buy food to be able] to live there, and do your prophesying there!
Amazia akamwambia Amosi, “Mwonaji, nenda, kimbia irudie nchi ya Yuda, na hapo ule mkate na kutabiri.
13 Do not prophesy any more here at Bethel, because this is where the national temple, the king’s temple, is!”
Lakini usitabiri tena hapa katika Betheli, kwa kuwa ni patakatifu pa mfalme na nyumba ya kifalme.”
14 I replied to Amaziah, “I was [previously] not a prophet, and my father was not a prophet; I was a shepherd. I also took care of sycamore-fig trees.
Kisha Amosi akamwambia Amazia, “Mimi sio nabii wala mwana wa nabii. Mimi ni mchungaji wa mifugo, na mtunza mikuyu.
15 But Yahweh took me away from taking care of my sheep, and he said to me, ‘Go to Israel and prophesy to my people there!’
Lakini Yahwe akanichukua kutoka kuchunga mifugo na kunambia, 'Nenda, katabiri kwa watu wangu Israeli.'
16 You said to me, ‘Do not prophecy saying terrible things will happen to [the people of] Israel; stop saying those things!’
Sasa sikia neno la Yahwe. Wewe usemaye, 'Usitabiri juu ya Israeli, na usiongee juu ya nyumba ya Isaka.
17 Therefore listen to what Yahweh says about you: ‘Your wife will become a prostitute in this city, and your sons and daughters will be killed by [your enemies’] swords. Others will measure your land and divide it up [among themselves]; and you yourself will die in a foreign country. And the people of Israel will certainly be forced to leave their country and go (into exile/to live in another country).’”
Kwa hiyo hivi ndivyo Yahwe asemavyo, 'Mke wako atakuwa kahaba katika mji; wana wako waume na binti zako wataanguka kwa upanga; nchi yako itapimwa na kugawanywa; utakufa katika nchi najisi, na Israeli hakika itakwenda utumwani kutoka nchi yake.”'

< Amos 7 >