< Ezekiel 26 >

1 Almost twelve [after we had been taken to Babylonia], on the first day of the month, Yahweh gave me another message. He said to me,
Mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
2 “You human, [the people of] Tyre [city] shouted joyfully and said about Jerusalem, ‘[Jerusalem, ] the city from which many traders/merchants went to many nations, is now destroyed. And now people from all over the world will come to us to buy and sell things. Because Jerusalem has now been ruined, we will prosper!’
“Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema kuhusu Yerusalemu, ‘Aha! Lango la kwenda kwa mataifa limevunjika, nayo milango yake iko wazi mbele yangu, sasa kwa kuwa amekuwa magofu nitastawi.’
3 Therefore, this is what [I, ] Yahweh the Lord, say: ‘I am now the enemy of [you people of] Tyre. I will [the armies of] many nations to come and attack your [city], like the waves of the sea beat against the shores.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na wewe, ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi dhidi yako, kama bahari inayovurumisha mawimbi yake.
4 Their soldiers will destroy the walls around Tyre and tear down its towers. Tyre will become a place where people from many nations steal valuable things, [and then the city will be completely destroyed]. Then they will scrape away the rubble and cause the city to become a bare rock.
Watavunja kuta za Tiro na kuibomoa minara yake, nitakwangua udongo wake na kuufanya mwamba mtupu.
5 Out in the sea, Tyre will become an island where men spread [their fishing] nets to dry them. [That will surely happen because] I, Yahweh the Lord, have predicted it.
Itakuwa huko katikati ya bahari patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki, kwa maana nimenena, asema Bwana Mwenyezi. Atakuwa nyara kwa mataifa,
6 The people in small villages on the coast near Tyre will be killed [their enemies’] swords. Then people will know that I, Yahweh, [have the power to do what I say that I will do].’
nayo makao yake huko bara yataangamizwa kwa upanga. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.
7 This is what I, Yahweh the Lord, [is going to happen]: ‘From the north, I am going to bring the most powerful king [in the world], King Nebuchadnezzar of Babylon, [with his army] to attack Tyre. They will bring horses and chariots, and men who ride the horses [and men who drive the chariots]; it will be a huge army.
“Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kutoka kaskazini nitamleta dhidi ya Tiro Mfalme Nebukadneza wa Babeli, mfalme wa wafalme, akiwa na farasi na magari ya vita, wapanda farasi na jeshi kubwa.
8 [In the battles in the small villages] on the coast, their soldiers will kill [many] people with their swords. [Then] they will set up devices to batter the wall around the city of Tyre, and they will build a dirt ramp up to the top of the wall, and they will all hold up shields [to protect themselves from arrows being shot from the ground].
Atayaharibu makao yako huko bara kwa upanga, ataweka jeshi kukuzingira, atakuzingira mpaka kwenye kuta za ngome zako na kuinua ngao zake dhidi yako.
9 The king will direct the soldiers who operate the (rams/things) to batter the walls, and who will use their iron bars to tear down the towers in the wall.
Ataelekeza mapigo ya vyombo vyake vya kubomolea dhidi ya kuta zako na kubomoa minara yako kwa silaha zake.
10 The king will have a huge number of horses, [the stamping of their hooves will result in] the city being covered with dust. [It will be as though] the walls will tremble because of the noise made by the horses, the [supply] wagons, and the chariots when they enter the city where the walls have been broken down.
Farasi zake zitakuwa nyingi sana kiasi kwamba utafunikwa na mavumbi watakayotimua. Kuta zako zitatikisika kwa mshindo wa farasi wa vita, magari makubwa na magari ya vita wakati aingiapo malango yako kama watu waingiao mji ambao kuta zake zimebomolewa kote.
11 The horses will trample all of the [of the city] with their hooves. The soldiers will kill the people with their swords; and they will cause your strong pillars to (collapse/fall to the ground).
“Kwato za farasi zake zitakanyaga barabara zako zote, atawaua watu wako kwa upanga na nguzo zako zilizo imara zitaanguka chini.
12 They will take away all the people’s valuable possessions and steal the things that the merchants sell. They will tear down the walls of the houses and destroy their fine houses. Then they will throw into the sea the stones [from the walls] of those houses and the timber and the rubble.
Watateka utajiri wako na kuchukua nyara bidhaa zako, watazivunja kuta zako na kuzibomoa nyumba zako nzuri, watatupa baharini mawe yako, mbao zako na kifusi chako.
13 No longer will you sing noisy songs, and people will not play their harps any more.
Nitakomesha kelele za nyimbo zako, na uimbaji wako wa kinubi kamwe hautasikika tena.
14 The enemy soldiers will cause the city to become a bare rock and [only] a place where men spread [their fishing] nets. And the city will never be rebuilt. [Those things will surely happen] because [I], Yahweh the Lord, have [that they will happen].’
Nitakufanya mwamba mtupu, nawe utakuwa mahali pa kutandazia nyavu za kuvulia samaki. Kamwe hutajengwa tena, kwa maana Mimi Bwana nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
15 This is [also] what [I], Yahweh the Lord, say about [the people of] Tyre: ‘When the wounded [people in Tyre] groan and many people are slaughtered and the city is destroyed, [it will surely be as though] [RHQ] the areas along the coast will tremble.
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa Tiro: ‘Je, nchi za pwani hazitatetemeka kwa kishindo cha anguko lako, wakati majeruhi wanapolia kwa maumivu makali na wakati mauaji yanaendelea ndani yako?
16 Then all the kings [in the cities] along the coast will step down from their thrones and lay aside their robes and their embroidered clothes. They will be terrified, and they will sit on the ground, trembling. They will be appalled because of what has happened to the city of Tyre.
Ndipo wakuu wote wa mataifa ya pwani watashuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuweka kando majoho yao na kuvua nguo zao zilizotariziwa. Wakiwa wamevikwa hofu kuu, wataketi chini ardhini, wakiwa wanatetemeka kila dakika na wakikustajabia.
17 Then they will sing a sad song about the city, and they will sing this: “The famous city [APO], in which many [who sailed on] the seas lived, is now destroyed! The people of that city had great power [because they had many ships that sailed] on the seas; they caused all the people who lived near them to be terrified.
Ndipo wao watakuombolezea na kukuambia: “‘Tazama jinsi ulivyoharibiwa, ee mji uliokuwa na sifa, wewe uliyekaliwa na mabaharia! Ulikuwa na nguvu kwenye bahari, wewe na watu wako; wote walioishi huko, uliwatia hofu kuu.
18 Now on the day when that city is destroyed, [it is as though the people in] the areas along the coast tremble and the [the people on the] islands in the sea are terrified because of that city being ruined.”’
Sasa nchi za pwani zinatetemeka katika siku ya anguko lako; visiwa vilivyomo baharini vinaogopa kwa kuporomoka kwako.’
19 This is also what [I], Yahweh the Lord, say: ‘When I cause the city [of Tyre] to become desolate/empty, like [other] cities in which people no [longer] live, and when I cause the huge waves of the sea to cover it,
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitakapokufanya uwe mji wa ukiwa, kama miji isiyokaliwa tena na watu, nitakapoleta vilindi vya bahari juu yako na maji yake makuu yatakapokufunika,
20 then I will bring the people of that city down to be with those who have gone down to where the dead people are, people who lived long ago. I will cause them to remain in the place below the earth that is like old/ancient ruins, with those who have gone down to that pit [previously], and they will never return to the earth, to where people are alive.
ndipo nitakapokushusha chini pamoja na wale washukao shimoni, kwa watu wa kale, nami nitakufanya uishi katika pande za chini za nchi kama katika magofu ya kale, pamoja na wale washukao shimoni, nawe hutarudi au kurejea kwenye makao yako katika nchi ya walio hai.
21 I will cause them to die in a horrible way (OR, people will be very afraid because of what happens to that city), and that will be the end of (them/their lives). People will search for that city but it will no longer exist. [That is what I, ] Yahweh the Lord, declare [will happen].’”
Nitakufikisha mwisho wa kutisha wala hutakuwepo tena. Watu watakutafuta, lakini kamwe hutaonekana tena, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ezekiel 26 >