< Genesis 46 >

1 So Jacob left [Canaan], taking with him all his family and possessions. When they arrived at Beersheba, he offered sacrifices to God, the one whom his father Isaac worshiped.
Hivyo Israeli akaondoka na vyote vilivyokuwa mali yake, naye alipofika Beer-Sheba, akamtolea dhabihu Mungu wa Isaki baba yake.
2 That night, God called to Jacob in a vision, saying, “Jacob! Jacob!” He replied, “I am here!”
Mungu akanena na Israeli katika maono usiku na kusema, “Yakobo! Yakobo!” Akajibu, “Mimi hapa.”
3 God said, “I am God, the one your father worshiped. Do not be afraid to go down to Egypt, because I will give you many descendants, and they will become a great nation there.
Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa baba yako, usiogope kushuka Misri, kwa maana huko nitakufanya taifa kubwa.
4 I will go down to Egypt with you, and later I will bring [your descendants] back to Canaan again. And Joseph will be with you [MTY] when you die.” [IDM]
Nitashuka Misri pamoja nawe, nami hakika nitakurudisha tena Kanaani. Mikono ya Yosefu mwenyewe ndiyo itakayofunga macho yako.”
5 Jacob left Beersheba, and his sons took their father, their wives, and their children, in the carts that the king had sent for them to travel in.
Ndipo Yakobo akaondoka Beer-Sheba nao wana wa Israeli wakamchukua baba yao Yakobo na watoto wao na wake zao katika magari ya kukokotwa yale Farao aliyokuwa amempelekea kumsafirisha.
6 So Jacob and all his family went to Egypt. They took with them the livestock and all the other possessions that they had acquired in Canaan.
Wakachukua pia mifugo yao na mali walizokuwa wamezipata Kanaani, Yakobo na uzao wake wote wakashuka Misri.
7 Jacob went to Egypt with all his sons and his daughters and grandsons and granddaughters—his whole family.
Akawachukua wanawe na binti zake, wajukuu wake wa kiume na wa kike, yaani uzao wake wote mpaka Misri.
8 (Here is/I will now give you) a list of the names of the members of Jacob’s family who went with him to Egypt: Reuben, Jacob’s oldest son; Reuben’s sons Hanoch, Pallu, Hezron, and Carmi; Simeon and his sons Jemuel, Jamin, Ohad, Jakin, Zohar, and Shaul, who was the son of a Canaan people-group woman; Levi and his sons Gershon, Kohath, and Merari; Judah and his sons, Shelah, Perez, and Zerah (his other sons, Er, and Onan, had died in Canaan); Perez and his two sons Hezron and Hamul; Issachar and his sons Tola, Puah, Jashub, and Shimron; Zebulon and his sons Sered, Elon, and Jahleel; (Those were the sons of Jacob and Leah, and their daughter Dinah, who were born in Paddan-Aram/Mesopotamia: There were 33 of them, altogether.) They had Gad and his sons Zephon, Haggi, Shuni, Ezbon, Eri, Arodi, and Areli; Asher and his sons Imnah, Ishvah, Ishvi, and Beriah; and their sister Serah; Beriah’s sons Heber and Malkiel; (Those were the children and grandchildren of Jacob and Zilpah, the slave girl whom Laban gave to his daughter Leah: There were 16 of them, altogether.) Joseph and Benjamin, the sons of Jacob’s wife Rachel; (Ephraim and Manasseh were Joseph’s two sons. [They did not go down to Egypt] because they were already in Egypt. They were sons of Asenath, the daughter of On, who was the priest in the temple in On [city].) Benjamin and his sons Bela, Beker, Ashbel, Gera, Naaman, Ehi, Rosh, Muppim, Huppim, and Ard; (Those were the sons and grandsons of Rachel and Jacob: There were 14 people altogether.) Dan and his son Hushim; Naphtali and his sons Jahziel, Guni, Jezer, and Shillem. (Those were the sons and grandsons of Jacob and Bilhah, the slave girl whom Laban gave to his daughter Rachel: There were seven people altogether.)
Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli (Yakobo na wazao wake), waliokwenda Misri: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo.
9
Wana wa Reubeni ni: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
Wana wa Simeoni ni: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani.
Wana wa Lawi ni: Gershoni, Kohathi na Merari.
Wana wa Yuda ni: Eri, Onani, Shela, Peresi na Zera (lakini Eri na Onani walifariki katika nchi ya Kanaani). Wana wa Peresi ni: Hesroni na Hamuli.
Wana wa Isakari ni: Tola, Puva, Yashubu na Shimroni.
Wana wa Zabuloni ni: Seredi, Eloni na Yaleeli.
Hawa ndio wana wa Lea aliomzalia Yakobo huko Padan-Aramu pamoja na binti yake Dina. Jumla ya wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
Wana wa Gadi ni: Sefoni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi na Areli.
Wana wa Asheri ni: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera. Wana wa Beria ni: Heberi na Malkieli.
Hawa ndio watoto Zilpa aliomzalia Yakobo, ambao Labani alimpa binti yake Lea; jumla yao walikuwa kumi na sita.
Wana wa Raheli mke wa Yakobo ni: Yosefu na Benyamini.
Huko Misri, Asenathi binti wa Potifera, aliyekuwa kuhani wa mji wa Oni, alimzalia Yosefu wana wawili, Manase na Efraimu.
Wana wa Benyamini ni: Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu na Ardi.
Hawa ndio wana wa Raheli aliomzalia Yakobo; jumla yao ni kumi na wanne.
Mwana wa Dani ni: Hushimu.
Wana wa Naftali ni: Yaseeli, Guni, Yeseri na Shilemu.
Hawa walikuwa wana wa Bilha aliomzalia Yakobo, ambaye Labani alikuwa amempa Raheli binti yake; jumla yao walikuwa saba.
26 Altogether there were 66 people who were Jacob’s descendants who went to Egypt with him. That number does not include his sons’ wives.
Wote waliokwenda Misri pamoja na Yakobo, waliokuwa wazao wake hasa pasipo kuhesabu wakwe zake, walikuwa watu sitini na sita.
27 Including Jacob and Joseph and Joseph’s two sons who were born in Egypt, there were 70 members of Jacob’s family when they were all there in Egypt.
Pamoja na wana wawili waliozaliwa na Yosefu huko Misri, jumla yote ya jamaa ya Yakobo, waliokwenda Misri, walikuwa sabini.
28 Jacob sent Judah to go ahead of the rest of them to talk with Joseph and ask for directions on how to travel to Goshen. Then [Judah returned to the rest of his family and] they all traveled to the Goshen region. When they arrived there,
Basi Yakobo akamtanguliza Yuda aende kwa Yosefu ili amwelekeze njia ya Gosheni. Walipofika nchi ya Gosheni,
29 Joseph got his chariot ready and went to Goshen to meet his father. When Joseph arrived, he threw his arms around his father’s neck and cried a long time.
gari kubwa zuri la Yosefu liliandaliwa, naye akaenda Gosheni kumlaki baba yake Israeli. Mara Yosefu alipofika mbele yake, alimkumbatia baba yake, akalia kwa muda mrefu.
30 Jacob said to Joseph, “I have seen you and I know that you are still alive! So now I am ready to die.”
Israeli akamwambia Yosefu, “Sasa niko tayari kufa, kwa kuwa nimejionea mwenyewe kwamba bado uko hai.”
31 Then Joseph said to his [older] brothers [and younger brother] and to the rest of his father’s family, “I will go to the king and say to him, ‘My [older] brothers [and younger brother] and my father and the rest of his family, who were living in Canaan land, have all come to me.
Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake na watu wa nyumbani mwa baba yake, “Nitapanda kwa Farao na kumwambia, ‘Ndugu zangu na watu wa nyumbani mwa baba yangu, waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, wamekuja kwangu.
32 The men are all shepherds. They take care of their livestock, and they have brought with them their sheep and goats and cattle, and everything else that they own.’
Watu hao ni wachunga mifugo, huchunga mifugo, wamekuja na makundi ya kondoo, mbuzi na ngʼombe pamoja na kila kitu walicho nacho.’
33 When the king summons you and asks, ‘What work do you do?’
Farao atakapowaita na kuwaulizeni, ‘Kazi yenu ni nini?’
34 answer him by saying, ‘From the time when we were young, we have taken care of livestock, just as our ancestors did.’ If you tell him that, he will let you live in the Goshen region.” Joseph told them to say that because the people of Egypt despised all shepherds.
Mjibuni, ‘Watumwa wako wamekuwa wachunga mifugo tangu ujana wetu mpaka sasa, kama baba zetu walivyofanya.’ Ndipo mtakaporuhusiwa kukaa katika nchi ya Gosheni, kwa kuwa wachunga mifugo wote ni chukizo kwa Wamisri.”

< Genesis 46 >