< Luke 10 >

1 After this, the Master appointed seventy-two other disciples, and sent them on as his Messengers, two and two, in advance, to every town and place that he was himself intending to visit.
Baada ya mambo hayo, Bwana akachagua sabini wengine, na kuwatuma wawili wawili wamtangulie katika kila mji na eneo alilotarajia kwenda.
2 “The harvest,” he said, “is abundant, but the labourers are few. Therefore pray to the Owner of the harvest to send labourers to gather in his harvest.
Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache. Hivyo basi muombeni Bwana wa mavuno, ili kwamba atume haraka wafanyakazi katika mavuno yake.
3 Now, go. Remember, I am sending you out as my Messengers like lambs among wolves.
Enendeni katika miji. Angalieni, ninawatuma kama kondoo katikati ya mbwa mwitu.
4 Do not take a purse with you, or a bag, or sandals; and do not stop to greet any one on your journey.
Msibebe mfuko wa pesa, wala mikoba ya wasafiri, wala viatu, wala msimsalimie yeyote njiani.
5 Whatever house you go to stay at, begin by praying for a blessing on it.
Katika nyumba yeyote mtakayo ingia, kwanza semeni, 'Amani iwe katika nyumba hii.'
6 Then, if any one there is deserving of a blessing, your blessing will rest upon him; but if not, it will come back upon yourselves.
kama mtu wa amani yupo pale, amani yenu itabaki juu yake, lakini kama sivyo, itarudi kwenu.
7 Remain at that same house, and eat and drink whatever they offer you; for the worker is worth his wages. Do not keep changing from one house to another.
Bakini katika nyumba hiyo, kuleni na mnywe watakachokitoa, kwa maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msihame kutoka nyumba hii kwenda nyingine.
8 Whatever town you visit, if the people welcome you, eat what is set before you;
Mji wowote muuingiao, na wakawapokea, kuleni chochote kitakachowekwa mbele yenu,
9 cure the sick there, and tell people ‘The Kingdom of God is close at hand.
na ponyeni wagonjwa waliomo humo. Semeni kwao, 'Ufalme wa Mungu umekuja karibu yanu'
10 But, whatever town you go to visit, if the people do not welcome you, go out into its streets and say
Lakini katika mji wowote mtakaoingia, na wasiwapokee, nendeni nje katika barabara na semeni,
11 ‘We wipe off the very dust of your town which has clung to Our feet; still, be assured that the Kingdom of God is close at Hand.’
'Hata vumbi katika mji wenu lililonata miguu mwetu tunalikung'uta dhidi yenu! Lakini tambueni hili, Ufalme wa Mungu umekaribia.'
12 I tell you that the doom of Sodom will be more bearable on ‘That Day’ than the doom of that town.
Ninawambieni kwamba siku ya hukumu itakuwa ni usitahamilivu zaidi kwa Sodoma kuliko mji huo.
13 Alas for you, Chorazin! Alas for you, Bethsaida! For, if the Miracles which have been done in you had been done in Tyre and Sidon, they would have sat in sackcloth and ashes and repented long ago.
Ole kwako Korazini, Ole kwako Bethsaida! Kama kazi kuu zilizo fanyika ndani yako ingalifanyika Tiro na Sidoni, Wangelitubu zamani sana, wakikaa ndani ya nguo za gunia na majivu.
14 Yet the doom of Tyre and Sidon will be more bearable at the Judgment than yours.
Lakini itakuwa usitahamilivu zaidi siku ya hukumu kwa Tiro na Sidoni zaidi yenu.
15 And you, Capernaum! Will you ‘exalt yourself to heaven’? ‘You shall go down to the Place of Death.’ (Hadēs g86)
Wewe Kapernaumu, Unafikiri utainuliwa mpaka Mbinguni? Hapana, utashushwa chini mpaka kuzimu (Hadēs g86)
16 He who listens to you is listening to me, and he who rejects you is rejecting me; while he who rejects me is rejecting him who sent me as his Messenger.”
Atakaye wasikiliza ninyi anisikiliza mimi, na yeyote atakaye wakataa anikataa mimi, na yeyote anikataaye mimi anmtakaa aliyenituma”
17 When the seventy-two returned, they exclaimed joyfully: “Master, even the demons submit to us when we use your name.”
Wale sabini walirudi kwa furaha, wakisema, “Bwana, hata mapepo wanatutii katika jina lako.”
18 And Jesus replied: “I have had visions of Satan, fallen, like lightning from the heavens.
Yesu akawaambia, “Nilimwona Shetani akianguka kutoka mbinguni kama radi.
19 Remember, I have given you the power to ‘trample upon serpents and scorpions,’ and to meet all the strength of the Enemy. Nothing shall ever harm you in any way.
Tazama, nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za adui, na hapana chochote kwa njia yoyote kitakachowadhuru.
20 Yet do not rejoice in the fact that the spirits submit to you, but rejoice that your names have been enrolled in Heaven.”
Hata hivyo msifurahi tu katika hili, kwamba roho zinawatii, lakini furahini zaidi kwamba majina yenu yameandikwa mbinguni.”
21 At that same time, moved to exultation by the Holy Spirit, Jesus said: “I thank thee, Father, Lord of Heaven and earth, that, though thou hast hidden these things from the wise and learned, thou hast revealed them to the childlike! Yes, Father, I thank thee that this has seemed good to thee.
Katika mda uleule alifurahi sana katika Roho Mtakatifu, na kusema, “Ninakusifu wewe, Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa sababu umeyaficha mambo haya kutoka kwa wenye hekima na akili, na kuyafunua kwa wasio fundishwa, kama watoto wadogo. Ndio, Baba, kwa kuwa ilipendeza katika machoni pako.”
22 Everything has been committed to me by my Father; nor does any one know who the Son is, except the Father, or who the Father is, except the Son and those to whom the Son may choose to reveal him.”
“Kila kitu kimekabidhiwa kwangu na Baba yangu, na hakuna afahamuye Mwana ni nani ila Baba, na hakuna afahamuye Baba ni nani ila Mwana, na ye yote ambaye Mwana hutamani kujifunua kwake.”
23 Then, turning to his disciples, Jesus said to them alone: “Blessed are the eyes that see what you are seeing;
Akawageukia wanafunzi, akasema faraghani, “Wamebarikiwa wayaonayo haya ambayo ninyi mnayaona.
24 for, I tell you, many Prophets and Kings wished for the sight of the things which you are seeing, yet never heard them.”
Ninawambia ninyi, kwamba manabii wengi na wafalme walitamani kuona mambo myaonayo, na hawakuyaona, na kusikia kusikia mnayoyaikia, na hawakuyasikia.”
25 Just then a Student of the Law came forward to test Jesus further. “Teacher,” he said, “what must I do if I am to ‘gain Immortal Life’?” (aiōnios g166)
Tazama, mwalimu fulani wa sheria ya Kiyahudi alisimama na kumjaribu, akisema, “Mwalimu, nifanye nini niurithi izima wa milele?” (aiōnios g166)
26 “What is said in the Law?” answered Jesus. “What do you read there?”
Yesu akamwambia, “Kimeandikwa nini katika sheria? Unaisoma je?”
27 His reply was — “‘Thou shalt love the Lord thy God with all thy heart, and with all thy soul, and with all thy strength, and with all thy mind; and thy neighbour as thou dost thyself.’”
Akajibu akasema, “Utampenda Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote, na jirani yako kama nafsi yako mwenyewe.”
28 “You have answered right,” said Jesus; “do that, and you shall live.”
Yesu akasema, “Umejibu kwa usahihi. Fanya hivi na utaishi.”
29 But the man, wanting to justify himself, said to Jesus: “And who is my neighbour?”
Lakini mwalimu, akitamani kujihesabia haki mwenyewe, Akamwambia Yesu, “Na jirani yangu ni nani?”
30 To which Jesus replied: “A man was once going down from Jerusalem to Jericho when he fell into the hands of robbers, who stripped him of everything, and beat him, and went away leaving him half dead.
Yesu akijibu akasema, “Mtu fulani alikuwa akitelemka kutoka Yerusalem kwenda Yeriko. Akaangukia kati ya wanyang'anyi, waliomnyang'anya mali yake, na kumpiga na kumuacha karibu akiwa nusu mfu.
31 As it chanced, a priest was going down by that road. He saw the man, but passed by on the opposite side.
Kwa bahati kuhani fulani alikuwa akishuka katika njia hiyo, alipo muona alipita upande mwingine.
32 A Levite, too, did the same; he came up to the spot, but, when he saw the man, passed by on the opposite side.
Vivyo hivyo Mlawi pia, alipofika mahali pale na kumuona, akapita upande mwingine.
33 But a Samaritan, traveling that way, came upon the man, and, when he saw him, he was moved with compassion.
Lakini Msamaria mmoja, alipokuwa akisafiri, alipita pale alipokuwa mtu huyo. alipomuona, alisukumwa kwa huruma.
34 He went to him and bound up his wounds, dressing them with oil and wine, and then put him on his own mule, and brought him to an inn, and took care of him.
Alimkaribia na kumfunga vidonda vyake, akimwiga mafuta na divai juu yake. Alimpandisha juu ya mnyama wake, na kumpeleka katika nyumba ya wageni na kumhudumia.
35 The next day he took out four shillings and gave them to the inn-keeper. ‘Take care of him,’ he said, ‘and whatever more you may spend I will myself repay you on my way back.’
Siku ilyofuata alichukua dinari mbili, na akampatia mmiliki wa nyumba ya wageni na kumwambia, 'Muhudumie na chochote cha ziada utakacho tumia, nitakulipa nitakaporudi.'
36 Now which, do you think, of these three men,” asked Jesus, “proved himself a neighbour to the man who fell into the robbers’ hands?”
Ni yupi kati ya hawa watatu, unafikiri, alikuwa ni jirani kwake yeye aliyeangukia kati ya wanyang'anyi?”
37 “The one that took pity on him,” was the answer; on which Jesus said: “Go and do the same yourself.”
Mwalimu alisema, “Ni yule aliyeonesha huruma kwake.” Yesu akamwambia, “Nenda na ukafanye vivyo hivyo”
38 As they continued their journey, Jesus came to a village, where a woman named Martha welcomed him to her house.
Sasa walipokuwa wakisafiri, waliingia katika kijiji fulani, na mwanamke mmoja jina lake Martha alimkaribisha nyumbani kwake.
39 She had a sister called Mary, who seated herself at the Master’s feet, and listened to his teaching;
Alikuwa na dada aliyeitwa Mariamu, aliekaa miguuni pa Bwana na kusikiliza neno lake.
40 but Martha was distracted by the many preparations that she was making. So she went up to Jesus and said: “Master, do you approve of my sister’s leaving me to make preparations alone? Tell her to help me.”
Lakini Martha alijipa shughuli nyingi za kuandaa mlo. Alikwenda kwa Yesu, na kusema, “Bwana, haujali kwamba dada yangu ameniacha nihudumu peke yangu? Hivyo basi mwambie anisaidie.”
41 “Martha, Martha,” replied the Master, “you are anxious and trouble yourself about many things;
Lakini Bwana alimjibu na kumwambia, “Martha, Martha, una sumbuka juu ya mambo mengi,
42 but only a few are necessary, or rather one. Mary has chosen the good part, and it shall not be taken away from her.”
lakini ni kitu kimoja tu cha muhimu. Mariamu amechagua kilicho chema, ambacho hakitaondolewa kutoka kwake.”

< Luke 10 >