< Exodus 6 >

1 Then the LORD said to Moses, Now shalt thou see what I will do to Pharaoh; for with a strong hand shall he let them go, and with a strong hand shall he drive them from his land.
Kisha Yahweh akasema na Musa, “Sasa utaona nitakacho fanya kwa Farao. Utaona hili, kwa kuwa ata waacha waenda kwa mkono wangu hodari. Kwasababu ya mkono wangu hodari, ata waondoa nje ya nchi.”
2 And God spoke to Moses, and said to him, I [am] the LORD:
Mungu akasema na Musa na kumwambia, “Mimi ni Yahweh.
3 And I appeared to Abraham, to Isaac, and to Jacob, by [the name of] God Almighty, but by my name JEHOVAH was I not known to them.
Nilimtokea Ibrahimu, Isaka, na Yakobo kama Mungu mwenye nguvu; lakini kwa jina langu, Yahweh, sikujuliikana kwao.
4 And I have also established my covenant with them, to give them the land of Canaan, the land of their pilgrimage, in which they were strangers.
Pia niliimarisha agano langu na wao, ilikuwapatia nchi ya Kanani, nchi walioishi kama sio raia, nchi walio tanga tanga.
5 And I have also heard the groaning of the children of Israel, whom the Egyptians keep in bondage: and I have remembered my covenant.
Zaidi ya yote, nimesikia kilio cha Waisraeli ambao wa Misri wame wa chukua watumwa, na nimekumbuka agano langu.
6 Wherefore say to the children of Israel, I [am] the LORD, and I will bring you from under the burdens of the Egyptians, and I will deliver you from their bondage, and I will redeem you with out-stretched arm, and with great judgments:
Kisha basi, sema kwa Waisraeli, 'Mimi ni Yahweh. Nitawatoa kwenye utumwa chini ya wa Misri, na kuwaweka huru na nguvu zao. Nitawaokoa kwa kudhihirisha nguvu zangu, na kwa matendo ya ajabu ya hukumu.
7 And I will take you to me for a people, and I will be to you a God: and ye shall know that I [am] the LORD your God, who bringeth you out from under the burdens of the Egyptians.
Nitawaleta kwangu kama watu wangu, na nitakuwa Mungu wenu. Mtajua kuwa mimi ndiye Yahweh Mungu wenu, aliye watoa kwenye utumwa chini ya wa Misri.
8 And I will bring you into the land, concerning which I swore to give it to Abraham, to Isaac, and to Jacob; and I will give it to you for a heritage: I [am] the LORD.
Nitawaleta kwenye nchi niliyo muahidi kumpa Ibrahimu, Isaka, na Yakobo. Nitawapa kama mali yenu. Mimi ni Yahweh.”'
9 And Moses spoke so to the children of Israel: but they hearkened not to Moses, by reason of anguish of spirit, and cruel bondage.
Musa alipo waambia haya Waisraeli, hawakumsiliza kwasababu ya mateso magumu ya utumwa wao.
10 And the LORD spoke to Moses, saying,
Hivyo Yahweh akazungumza na Musa na kumwambia,
11 Go in, speak to Pharaoh, king of Egypt, that he let the children of Israel depart from his land.
“Nenda umwambie Farao, mfalme wa Misri, awaache watu wa Israeli waondoke kwenye nchi yake.”
12 And Moses spoke before the LORD, saying, Behold, the children of Israel have not hearkened to me; how then shall Pharaoh hear me, who [am] of uncircumcised lips?
Musa akamwambia Yahweh, “Kama Waisraeli hawajanisikiliza mimi, kwa nini Farao anisikillize mimi, tangu mimi sio mzuri wakuzungumza?”
13 And the LORD spoke to Moses, and to Aaron, and gave them a charge to the children of Israel, and to Pharaoh, king of Egypt, to bring the children of Israel out of the land of Egypt.
Yahweh akasema na Musa na Aruni. Akawapa amri ya Waisraeli na Farao, mfalme wa Misri, awatoe Waisraeli kutoka nchi ya Misri.
14 These [are] the heads of their father's houses: The sons of Reuben the first-born of Israel; Hanoch, and Pallu, Hezron, and Carmi: these [are] the families of Reuben.
Hawa walikuwa vichwa wa nyumba za baba yao: wana wa Rubeni, mzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa Hanoki, Palu, Hezroni, na Karmi. Hawa walikuwa mababu wa ukoo wa Rubeni.
15 And the sons of Simeon; Jemuel, and Jamin, and Ohad, and Jachin, and Zohar, and Shaul the son of a Canaanitish woman: these [are] the families of Simeon.
Wana wa Simeoni walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Zohari, na Shauli - mwana wa mwanamke wa Kanani. Hawa walikuwa mababu wa ukoo wa Simeoni.
16 And these [are] the names of the sons of Levi, according to their generations; Gershon, and Kohath, and Merari. And the years of the life of Levi [were] a hundred and thirty-seven years.
Hapa yameorodheshwa majina ya wana wa Lawi, pamoja na uzo wao. Walikuwa ni Gerishoni, Kohathi, na Merari. Lawi aliishi mpaka alipo kuwa na miaka 137.
17 The sons of Gershon; Libni, and Shimi, according to their families.
Wana wa Gerishoni walikuwa Libni na Shimei.
18 And the sons of Kohath; Amram, and Izhar, and Hebron, and Uzziel: and the years of the life of Kohath [were] a hundred and thirty-three years.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na uzieli. Kohathi aliishi hadi miaka 133.
19 And the sons of Merari; Mahali and Mushi: these [are] the families of Levi, according to their generations.
Wana wa Merari walikuwa Mahli na Mushi. Hawa walikuja kuwa mababu wa ukoo wa Walawi, pamoja na uzao wao.
20 And Amram took him Jochebed, his father's sister, for a wife; and she bore him Aaron and Moses. And the years of the life of Amram [were] a hundred and thirty-seven years.
Amramu alimuoa Yokebedi, dada yake baba yake. Alimzalia Aruni na Musa. Amramu aliishi miaka 137 na akafa.
21 And the sons of Izhar; Korah, and Nepheg, and Zichri.
Wana wa Izhari walikuwa Kora, Nefegi, na Zikri.
22 And the sons of Uzziel; Mishael, and Elzaphan, and Zithri.
Wana wa Uzieli walikuwa Mishaeli, Elizafani na Sithri.
23 And Aaron took him Elisheba daughter of Amminadab, sister of Naashon, for a wife; and she bore him Nadab and Abihu, Eleazar and Ithamar.
Aruni alimuoa Elisheba, binti wa Aminadabu, dada wa Nashoni. Alimzaa Nadabu na Abihu, Eleazari na Ithamari.
24 And the sons of Korah; Assir, and Elkanah, and Abiasaph: these [are] the families of the Korhites.
Wana wa Kora walikuwa Asiri, Elikana na Abiasa. Hawa walikuwa mababu wa ukoo wa Wakora.
25 And Eleazar, Aaron's son, took him [one] of the daughters of Putiel for a wife; and she bore to him Phinehas: these [are] the heads of the fathers of the Levites, according to their families.
Eleazari, mwana wa Aruni, alimuoa mmoja wa mabinti Wa Putieli. Alimzalia Fineazi. Hawa walikuwa vichwa wa nyumba za baba yao miongoni mwa Walawi, pamoja na uzao wao.
26 These [are] that Aaron and Moses, to whom the LORD said, Bring out the children of Israel from the land of Egypt according to their armies.
Hawa wanaume wawili walikuwa Musa na Aruni ambao Yahweh alisema, “Waleteni Waisraeli kutoka nchi ya Misri, kwa makundi ya wanaume wapiganaji.”
27 These [are] they who spoke to Pharaoh, king of Egypt, to bring out the children of Israel from Egypt: these [are] that Moses and Aaron.
Aruni na Musa wakazungumza na Farao, mfalme wa Misri, awaruhusu Waisraeli watoke Misri. Hawa walikuwa Musa na Aruni wale wale.
28 And it came to pass, on the day [when] the LORD spoke to Moses in the land of Egypt,
Pale Yahweh alipo zungumza na Musa katika nchi ya Misri,
29 That the LORD spoke to Moses, saying, I [am] the LORD: speak thou to Pharaoh, king of Egypt, all that I say to thee.
alimwambia, “Mimi ni Yahweh. Sema kwa Farao, mfalme wa MIsri, kila kitu nitacho kwambia.”
30 And Moses said before the LORD, Behold, I [am] of uncircumcised lips, and how shall Pharaoh hearken to me?
Lakini Musa alimwambia Yahweh, “Mimi sio mzuri wa kuongea, hivyo kwanini Farao anisikilize mimi?”

< Exodus 6 >