< Hosea 7 >

1 When I would heal Israel, then the iniquity of Ephraim is uncovered, also the wickedness of Samaria; for they commit falsehood, and the thief enters in, and the gang of robbers ravages outside.
kila mara nilipotaka kumponya Israeli, dhambi za Efraimu zinafichuliwa na maovu ya Samaria yanafunuliwa. Wanafanya udanganyifu, wevi huvunja nyumba, maharamia hunyangʼanya barabarani,
2 They don’t consider in their hearts that I remember all their wickedness. Now their own deeds have engulfed them. They are before my face.
lakini hawafahamu kwamba ninakumbuka matendo yao yote mabaya. Dhambi zao zimewameza, ziko mbele zangu siku zote.
3 They make the king glad with their wickedness, and the princes with their lies.
“Wanamfurahisha sana mfalme kwa maovu yao, wakuu wao kwa uongo wao.
4 They are all adulterers. They are burning like an oven that the baker stops stirring, from the kneading of the dough, until it is leavened.
Wote ni wazinzi, wanawaka kama tanuru ambayo moto wake mwokaji hana haja ya kuuchochea kuanzia kukanda unga hadi umekwisha kuumuka.
5 On the day of our king, the princes made themselves sick with the heat of wine. He joined his hand with mockers.
Katika sikukuu ya mfalme wetu wakuu wanawaka kwa mvinyo, naye anawaunga mkono wenye mizaha.
6 For they have prepared their heart like an oven, while they lie in wait. Their anger smoulders all night. In the morning it burns as a flaming fire.
Mioyo yao ni kama tanuru, wanamwendea kwa hila. Hasira yao inafoka moshi usiku kucha, wakati wa asubuhi inalipuka kama miali ya moto.
7 They are all hot as an oven, and devour their judges. All their kings have fallen. There is no one amongst them who calls to me.
Wote ni moto kama tanuru; wanawaangamiza watawala wao. Wafalme wake wote wanaanguka, wala hakuna yeyote kati yao aniitaye mimi.
8 Ephraim mixes himself amongst the nations. Ephraim is a pancake not turned over.
“Efraimu anajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate ambao haukuiva.
9 Strangers have devoured his strength, and he doesn’t realise it. Indeed, grey hairs are here and there on him, and he doesn’t realise it.
Wageni wananyonya nguvu zake, lakini hafahamu hilo. Nywele zake zina mvi hapa na pale, lakini hana habari.
10 The pride of Israel testifies to his face; yet they haven’t returned to the LORD their God, nor sought him, for all this.
Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yake, lakini pamoja na haya yote harudi kwa Bwana Mungu wake wala kumtafuta.
11 “Ephraim is like an easily deceived dove, without understanding. They call to Egypt. They go to Assyria.
“Efraimu ni kama hua, hudanganywa kwa urahisi na hana akili: mara anaita Misri, mara anageukia Ashuru.
12 When they go, I will spread my net on them. I will bring them down like the birds of the sky. I will chastise them, as their congregation has heard.
Wakati watakapokwenda, nitatupa wavu wangu juu yao; nitawavuta chini waanguke kama ndege wa angani. Nitakaposikia wakikusanyika pamoja, nitawanasa.
13 Woe to them! For they have wandered from me. Destruction to them! For they have trespassed against me. Though I would redeem them, yet they have spoken lies against me.
Ole wao, kwa sababu wamepotoka kutoka kwangu! Maangamizi ni yao kwa sababu wameniasi! Ninatamani kuwakomboa, lakini wanasema uongo dhidi yangu.
14 They haven’t cried to me with their heart, but they howl on their beds. They assemble themselves for grain and new wine. They turn away from me.
Hawanililii mimi kutoka mioyoni mwao, bali wanaomboleza vitandani mwao. Hukusanyika pamoja kwa ajili ya nafaka na divai mpya, lakini hugeukia mbali nami.
15 Though I have taught and strengthened their arms, yet they plot evil against me.
Niliwafundisha na kuwatia nguvu, lakini wanapanga mabaya dhidi yangu.
16 They return, but not to the Most High. They are like a faulty bow. Their princes will fall by the sword for the rage of their tongue. This will be their derision in the land of Egypt.
Hawamgeukii Yeye Aliye Juu Sana, wako kama upinde wenye kasoro. Viongozi wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya maneno yao ya jeuri. Kwa ajili ya hili watadhihakiwa katika nchi ya Misri.

< Hosea 7 >