< Deuteronomy 26 >

1 And whanne thou hast entrid in to the lond which thi Lord God schal yyue to thee to welde, and thou hast gete it, and hast dwellid therynne,
Utakapofika katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupatia kama urithi, na utakapoimiliki na kuishi ndani yake,
2 thou schalt take the firste fruytis of alle thi fruytis, and thou schalt putte in a panyere; and thou schalt go to the place which thi Lord God chees, that his name be inwardly clepid there.
basi unatakiwa kuchukua baadhi ya mavuno yote ya kwanza ya ardhi uliyoyaleta kutoka katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupatia. Unatakiwa kuyaweka ndani ya kikapu na kuelekea katika eneo ambalo Yahwe Mungu wako atapachagua kama mahali patakatifu.
3 And thou schalt go to the preest, that schal be in tho daies, and thou schalt seie to hym, Y knowleche to dai bifor thi Lord God, that Y entride in to the lond, for which he swoor to oure fadris, that he schulde yyue it to vs.
Unatakiwa kwenda kwa kuhani ambaye atakuwa akihudumu katika siku hizo na kumwambia, “Siku ya leo ninakiri kwa Yahwe Mungu wako ya kuwa nimekuja katika nchi ambayo Yahwe aliapa kwa mababu zetu kutupatia”.
4 And the preest schal take the panyere of thin hond, and schal sette bifor the auter of thi Lord God.
Kuhani anatakiwa kuchukua kikapu mkononi mwako na kukiweka madhabahuni ya Yahwe Mungu wako.
5 And thou schalt speke in the siyt of thi Lord God, Sirus pursuede my fadir, `which fadir yede doun in to Egipt, and was a pilgrym there in feweste noumbre; and he encreesside in to a greet folk, and strong, and of multitude without noumbre.
Unapaswa kusema mbele ya Yahwe Mungu wako, “Babu yangu alikuwa Mwaremi mzururaji. Alikwenda chini hadi Misri na kukaa kule, na idadi ya watu wake ilikuwa chache. Kule akawa taifa kubwa, lenye nguvu na idadi kubwa.
6 And Egipcians turmentiden vs, and pursueden, and puttiden greuouseste birthuns.
Wamisri walitutendea vibaya na kututesa. Walitulazimisha kufanya kazi za watumwa.
7 And we crieden to the Lord God of oure fadris, which herde vs, and bihelde oure mekenesse, and trauel, and angwischis;
Tulimlilia Yahwe, Mungu wa baba zetu, naye akasikia sauti yetu na kuona mateso yetu, kazi zetu na mateso yetu.
8 and he ledde vs out of Egipt in myyti hond, and arm holdun forth, in grete drede, in myraclis, and grete wondris,
Yahwe alituondoa Misri kwa mkono wake mkuu, kwa mkono wake ulionyoshwa, kwa hofu kuu, kwa ishara na miujiza;
9 and ledde vs in to this place; and yaf to vs a lond flowynge with mylk and hony.
na ametuleta katika sehemu hii na kutupatia nchi hii, nchi inayotiririka kwa maziwa na asali.
10 And therfor Y offre now to thee the fyrste fruytis of the fruitis of the lond which the Lord yaf to me. And thou schalt leeue tho in the siyt of thi Lord God. And whanne thi Lord God is worchipid,
Tazama sasa, nimeleta mavuno ya kwanza kutoka katika nchi ambayo wewe, Yahwe, umenipatia.” Unapaswa kuweka chini mbele ya Yahwe Mungu wako na kuabudu mbele zake;
11 thou schalt ete in alle the goodis whiche thi Lord God yaf to thee and to thin hows, thou, and the dekene, and the comelyng which is with thee.
na unapaswa kufurahia katika mema yote ambayo Yahwe Mungu wako amekufanyia, kwa ajili na nyumba yako – wewe, na Mlawi, na mgeni aliye miongoni mwako.
12 Whanne thou hast fillid the tithe of alle thi fruytis, in the thridde yeer of tithis, thou schalt yyue to the dekene, and to the comelyng, and to the fadirles, ether modirles child, and to widewe, that thei ete with ynne thi yatis, and be fillid.
Utakapomaliza kutoa zaka yote ya mavuno katika mwaka wa tatu, yaani, mwaka wa kutoa zaka, basi unapaswa kuwapatia Mlawi, kwa mgeni, kwa yatima, na kwa mjane, ili kwamba waweze kula ndani ya malango yenu ya mji na kujazilishwa.
13 And thou schalt speke in the siyt of thi Lord God, Y haue take awai that that is halewid of myn hows, and Y yaf it to the dekene, and to the comelyng, to the fadirles, ethir modirles child, and to the widewe, as thou comaundidist to me; Y passide not thi comaundementis, Y foryat not thin heest.
Unatakiwa kusema mbele ya Yahwe Mungu wako, “Nimetoa kutoka nyumbani mwangu vitu ambavyo ni mali ya Yahwe, na kumpatia Mlawi, mgeni, yatima, na mjane, kulingana na amri zote ulizonipatia. Sijavunja amri yako yoyote, wala sijazisahau.
14 Y ete not of tho thingis in my morenyng, nether Y departide tho in ony vnclennesse, nethir Y spendide of tho ony thing in biriyng of deed body, `that is, in makynge feestis therof in biryynge of deed men. Y obeiede to the vois of my Lord God, and Y dide alle thingis as thou comaundidist to me.
Sijala kati yao wakati wa maombolezo yangu, wala sijaziweka mahali pengine nilipokuwa mchafu, wala sijazitoa kati yao kwa heshima ya wafu. Nimesikiliza sauti ya Yahwe Mungu wangu; Nimetii kila kitu ulichoniamuru kukifanya.
15 Bihold thou fro thi seyntuarie, fro the hiy dwellyng place of heuene, and blesse thou thi puple Israel, and the lond which thou hast youe to vs, as thou `hast swoore to oure fadris; the lond flowynge with mylk and hony.
Tazama chini kutoka mahali patakatifu unapoishi, kutoka mbinguni, na ubariki watu wako Israeli, na nchi uliyotupatia, kama ulivyoapa kwa mababu zetu, nchi inayotiririka kwa maziwa na asali.
16 To dai thi Lord God comaundide to thee, that thou do these comaundementis and domes, that thou kepe and fille of al thin herte, and of al thi soule.
Leo Yahwe Mungu wako anawaamuru kuzitii sheria na amri hizi; basi utazishikilia na kuzitenda kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote.
17 Thou hast chose the Lord to day, that he be God to thee, and thou go in hise weies, and thou kepe hise cerymonyes, and heestis, and domes, and obeie to his comaundement.
Umetamka leo ya kuwa Yahwe ni Mungu wako, na kwamba utatembea katika njia zake na kushikilia sheria zake, maagizo yake na amri zake, na kwamba utaisikiliza sauti yake.
18 Lo! the Lord chees thee to day, that thou be a special puple to hym, as he spak to thee, and that thou kepe alle hise comaundementis;
Leo Yahwe ametamka ya kwamba mu watu ambao ni mali yake, kama alivyoahidi kwenu, na kwamba mnapaswa kushikilia amri zake zote.
19 and he schal make thee hiyere than alle folkis, whiche he made in to his preisyng, and name, and glorie; that thou be an holi puple of thi Lord God, as he spak to thee.
Na atawaweka juu zaidi ya mataifa mengine aliyoyaumba nanyi mtapokea sifa, umaarufu na heshima. Mtakuwa watu waliowekwa kando kwa Yahwe Mungu wako, kama alivyosema.”

< Deuteronomy 26 >