< Nombres 3 >

1 Et ce sont ici les générations d’Aaron et de Moïse, au jour où l’Éternel parla à Moïse sur la montagne de Sinaï.
Hii ni hesabu ya jamaa ya Aroni na Mose kwa wakati ambao Bwana alizungumza na Mose katika Mlima Sinai.
2 Et ce sont ici les noms des fils d’Aaron: le premier-né, Nadab, et Abihu, Éléazar et Ithamar.
Majina ya wana wa Aroni yalikuwa: Nadabu mzaliwa wa kwanza na Abihu, Eleazari na Ithamari.
3 Ce sont là les noms des fils d’Aaron, les sacrificateurs oints qui furent consacrés pour exercer la sacrificature.
Hayo yalikuwa majina ya wana wa Aroni, makuhani wapakwa mafuta, waliokuwa wamesimikwa kuhudumu kama makuhani.
4 Et Nadab et Abihu moururent devant l’Éternel, lorsqu’ils présentèrent un feu étranger devant l’Éternel dans le désert de Sinaï, et ils n’eurent point de fils; et Éléazar et Ithamar exercèrent la sacrificature en présence d’Aaron, leur père.
Hata hivyo Nadabu na Abihu walikufa mbele za Bwana walipotoa sadaka kwa moto usioruhusiwa mbele zake katika Jangwa la Sinai. Hawakuwa na wana; kwa hiyo Eleazari na Ithamari walihudumu peke yao kama makuhani wakati wote wa maisha ya Aroni baba yao.
5 Et l’Éternel parla à Moïse, disant:
Bwana akamwambia Mose,
6 Fais approcher la tribu de Lévi, et fais-la se tenir devant Aaron, le sacrificateur, afin qu’ils le servent,
“Walete watu wa kabila la Lawi mbele ya Aroni kuhani ili wamsaidie.
7 et qu’ils accomplissent ce qui appartient à son service, et au service de toute l’assemblée, devant la tente d’assignation, pour faire le service du tabernacle;
Watafanya huduma kwa ajili yake na kwa jumuiya yote katika Hema la Kukutania kwa kufanya kazi za Maskani.
8 et ils auront la charge de tous les ustensiles de la tente d’assignation, et de ce qui se rapporte au service des fils d’Israël, pour faire le service du tabernacle.
Watatunza samani zote za Hema la Kukutania, wakitimiza wajibu wa kuhudumia Waisraeli kwa kufanya kazi ya Maskani.
9 Et tu donneras les Lévites à Aaron et à ses fils; ils lui sont absolument donnés d’entre les fils d’Israël.
Wakabidhi Walawi kwa Aroni na wanawe; hao ndio Waisraeli ambao wanakabidhiwa kwake kabisa.
10 Et tu établiras Aaron et ses fils, afin qu’ils accomplissent les devoirs de leur sacrificature; et l’étranger qui approchera sera mis à mort.
Waweke Aroni na wanawe kuhudumu kama makuhani; mtu mwingine yeyote atakayesogea mahali patakatifu ni lazima auawe.”
11 Et l’Éternel parla à Moïse, disant:
Bwana akamwambia Mose,
12 Et moi, voici, j’ai pris les Lévites du milieu des fils d’Israël, à la place de tout premier-né d’entre les fils d’Israël qui ouvre la matrice; et les Lévites seront à moi;
“Nimewatwaa Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli badala ya mzaliwa wa kwanza wa kiume wa kila mwanamke wa Mwisraeli. Walawi ni wangu,
13 car tout premier-né est à moi. Le jour où j’ai frappé tout premier-né dans le pays d’Égypte, je me suis sanctifié tout premier-né en Israël, depuis l’homme jusqu’à la bête: ils seront à moi. Je suis l’Éternel.
kwa kuwa wazaliwa wote wa kwanza ni wangu. Nilipowaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, nilimtenga kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli awe wangu, akiwa mwanadamu au mnyama. Watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.”
14 Et l’Éternel parla à Moïse, dans le désert de Sinaï, disant:
Bwana akamwambia Mose katika Jangwa la Sinai,
15 Dénombre les fils de Lévi selon leurs maisons de pères, selon leurs familles: tu dénombreras tous les mâles depuis l’âge d’un mois et au-dessus.
“Wahesabu Walawi kwa jamaa zao na koo zao. Mhesabu kila mwanaume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi.”
16 Et Moïse les dénombra selon le commandement de l’Éternel, comme il lui avait été commandé.
Kwa hiyo Mose akawahesabu, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
17 Ce sont ici les fils de Lévi, selon leurs noms: Guershon, et Kehath, et Merari.
Haya yalikuwa majina ya wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
18 Et ce sont ici les noms des fils de Guershon, selon leurs familles: Libni et Shimhi.
Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya koo za Wagershoni: Libni na Shimei.
19 Et les fils de Kehath, selon leurs familles: Amram, et Jitsehar, Hébron, et Uziel.
Koo za Wakohathi zilikuwa ni: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
20 Et les fils de Merari, selon leurs familles: Makhli et Mushi. Ce sont là les familles de Lévi, selon leurs maisons de pères.
Koo za Wamerari zilikuwa ni: Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kufuatana na jamaa zao.
21 De Guershon, la famille des Libnites et la famille des Shimhites; ce sont là les familles des Guershonites:
Kulikuwa na koo za Walibni na Washimei kwa Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wagershoni.
22 ceux d’entre eux qui furent dénombrés, en comptant tous les mâles depuis l’âge d’un mois et au-dessus, ceux qui furent dénombrés furent 7 500.
Idadi ya waume wote waliokuwa na mwezi mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 7,500.
23 Les familles des Guershonites campèrent derrière le tabernacle, vers l’occident;
Ukoo wa Wagershoni walitakiwa kuweka kambi zao upande wa magharibi, nyuma ya Maskani.
24 et le prince de la maison de père des Guershonites était Éliasaph, fils de Laël.
Kiongozi wa jamaa za Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli.
25 Et la charge des fils de Guershon, à la tente d’assignation, était le tabernacle et la tente, sa couverture, et le rideau de l’entrée de la tente d’assignation,
Katika Hema la Kukutania, Wagershoni walikuwa na wajibu wa kutunza Maskani na hema, vifuniko vyake, pazia katika mlango wa kuingilia ndani ya Hema la Kukutania,
26 et les tentures du parvis, et le rideau de l’entrée du parvis qui entoure le tabernacle et l’autel, et ses cordages pour tout son service.
mapazia ya ua, pazia katika ingilio la ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pamoja na kamba, na kila kinachohusika kwa matumizi yake.
27 Et de Kehath, la famille des Amramites, et la famille des Jitseharites, et la famille des Hébronites, et la famille des Uziélites; ce sont là les familles des Kehathites:
Kwa Kohathi kulikuwepo koo za Waamramu, Waishari, Wahebroni na Wauzieli; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wakohathi.
28 en comptant tous les mâles, depuis l’âge d’un mois et au-dessus, il y en eut 8 600, qui avaient la charge du lieu saint.
Hesabu ya waume wote wenye mwezi mmoja au zaidi ilikuwa watu 8,600. Wakohathi waliwajibika kutunza mahali patakatifu.
29 Les familles des fils de Kehath campèrent à côté du tabernacle, vers le midi;
Koo za Wakohathi zilitakiwa kuweka kambi zao upande wa kusini wa Maskani.
30 et le prince de la maison de père des familles des Kehathites était Élitsaphan, fils d’Uziel.
Kiongozi wa jamaa za koo za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli.
31 Et leur charge était l’arche, et la table, et le chandelier, et les autels, et les ustensiles du lieu saint, avec lesquels on fait le service, et le rideau et tout le service qui s’y rattachait.
Waliwajibika kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, madhabahu, na vile vyombo vya mahali patakatifu vinavyotumika kuhudumu, pazia, na kila kitu kinachohusika na matumizi yake.
32 – Et le prince des princes des Lévites était Éléazar, fils d’Aaron, le sacrificateur; il était établi sur ceux qui avaient la charge du lieu saint.
Kiongozi mkuu wa Walawi alikuwa Eleazari mwana wa kuhani, Aroni. Aliwekwa juu ya wale waliowajibika kutunza mahali patakatifu.
33 De Merari, la famille des Makhlites et la famille des Mushites; ce sont là les familles de Merari:
Kwa Merari kulikuwa na koo za Wamahli na Wamushi; hizi zilikuwa koo za Merari.
34 et ceux d’entre eux qui furent dénombrés, en comptant tous les mâles depuis l’âge d’un mois et au-dessus, furent 6 200.
Hesabu ya waume wote wenye umri wa mwaka mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 6,200.
35 Et le prince de la maison de père des familles de Merari était Tsuriel, fils d’Abikhaïl. Ils campèrent du côté du tabernacle, vers le nord.
Kiongozi wa jamaa za koo za Wamerari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa walitakiwa kuweka kambi zao upande wa kaskazini mwa Maskani.
36 Et la surveillance des ais du tabernacle, et de ses traverses, et de ses piliers, et de ses bases, et de tous ses ustensiles, et tout le service qui s’y rattachait,
Wamerari waliwekwa kutunza miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo, vitako na vifaa vyake vyote na kila kitu kilichohusika na matumizi yake,
37 et les piliers du parvis tout autour, et leurs bases, et leurs pieux, et leurs cordages, furent confiés aux fils de Merari.
na pia nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema na kamba zake.
38 Et ceux qui campèrent devant le tabernacle, vers l’orient, devant la tente d’assignation, vers le levant, furent Moïse et Aaron et ses fils, veillant au service du sanctuaire pour ce qui était confié aux fils d’Israël. – Et l’étranger qui approchera sera mis à mort.
Mose, na Aroni na wanawe walitakiwa kuweka kambi zao mashariki mwa Maskani, kuelekea mawio ya jua, mbele ya Hema la Kukutania. Wao walihusika na utunzaji wa mahali patakatifu kwa niaba ya Waisraeli. Mtu mwingine yeyote aliyepasogelea mahali patakatifu angeuawa.
39 Tous les Lévites dénombrés, que Moïse et Aaron dénombrèrent selon leurs familles, selon le commandement de l’Éternel, tous les mâles, depuis l’âge d’un mois et au-dessus, furent 22 000.
Jumla ya hesabu ya Walawi waliohesabiwa na Mose na Aroni kwa amri ya Bwana, kufuatana na koo, pamoja na kila mume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walikuwa 22,000.
40 Et l’Éternel dit à Moïse: Dénombre tous les premiers-nés mâles des fils d’Israël, depuis l’âge d’un mois et au-dessus, et relève le nombre de leurs noms.
Bwana akamwambia Mose, “Wahesabu wazaliwa wa kwanza wa kiume wote wa Waisraeli wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi na uorodheshe majina yao.
41 Et tu prendras les Lévites pour moi (je suis l’Éternel), à la place de tous les premiers-nés parmi les fils d’Israël, et le bétail des Lévites à la place de tous les premiers-nés parmi le bétail des fils d’Israël.
Nitwalie Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya wazaliwa wa mifugo ya Waisraeli. Mimi ndimi Bwana.”
42 Et Moïse fit le dénombrement de tous les premiers-nés parmi les fils d’Israël, comme l’Éternel lui avait commandé;
Hivyo Mose akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru.
43 et tous les premiers-nés mâles, selon le nombre des noms, depuis l’âge d’un mois et au-dessus, selon leur dénombrement, furent 22 273.
Jumla ya hesabu ya wazaliwa wa kwanza waume wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walioorodheshwa kwa majina, walikuwa 22,273.
44 Et l’Éternel parla à Moïse, disant:
Bwana akamwambia Mose,
45 Prends les Lévites, à la place de tous les premiers-nés parmi les fils d’Israël, et le bétail des Lévites, à la place de leur bétail; et les Lévites seront à moi. Je suis l’Éternel.
“Watwae Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya mifugo yao. Walawi watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.
46 Et quant à ceux qu’il faut racheter, les 273 parmi les premiers-nés des fils d’Israël, qui sont de plus que les Lévites,
Ili kukomboa wazao wa kwanza 273 wa Waisraeli ambao wamezidi hesabu ya Walawi,
47 tu prendras cinq sicles par tête; tu les prendras selon le sicle du sanctuaire, le sicle à 20 guéras,
kusanya shekeli tano kwa kila mmoja, kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini.
48 et tu donneras à Aaron et à ses fils l’argent de ceux qui sont rachetés, qui sont de plus que les [Lévites].
Mpe Aroni na wanawe hizo fedha kwa ajili ya ukombozi wa idadi ya Waisraeli waliozidi.”
49 Et Moïse prit l’argent du rachat, de ceux qui étaient de plus que le nombre de ceux qui avaient été rachetés par les Lévites;
Kwa hiyo Mose akakusanya fedha za ukombozi kutoka kwa wale ambao hesabu yao ilizidi wale waliokombolewa na Walawi.
50 il prit l’argent de la part des premiers-nés des fils d’Israël, 1 365 [sicles], selon le sicle du sanctuaire.
Kutokana na wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli alikusanya fedha yenye uzito wa shekeli 1,365 kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu.
51 Et Moïse donna l’argent des rachetés à Aaron et à ses fils, selon le commandement de l’Éternel, comme l’Éternel l’avait commandé à Moïse.
Mose akampa Aroni na wanawe ile fedha ya ukombozi, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.

< Nombres 3 >