< Osée 10 >

1 Israël est une vigne dépouillée. On lui avait prodigué les fruits: à mesure que ses fruits augmentaient, il multipliait les autels; plus son pays était prospère, plus ils érigeaient de belles stèles.
Israeli alikuwa mzabibu uliostawi sana, alijizalia matunda mwenyewe. Kadiri matunda yake yalivyoongezeka, alijenga madhabahu zaidi; kadiri nchi yake ilivyostawi, alipamba mawe yake ya ibada.
2 Leur cœur s’est partagé, ils en portent la peine maintenant; Lui-même abattra leurs autels, ruinera leurs stèles.
Moyo wao ni mdanganyifu, nao sasa lazima wachukue hatia yao. Bwana atabomoa madhabahu zao na kuharibu mawe yao ya ibada.
3 Ils disent bien à présent: "De roi, nous n’en avons point! Car nous ne craignons pas l’Eternel, et le roi, à quoi peut-il nous servir?"
Kisha watasema, “Hatuna mfalme kwa sababu hatukumheshimu Bwana. Lakini hata kama tungelikuwa na mfalme, angeweza kutufanyia nini?”
4 Ils débitent de vains discours, des serments frauduleux, contractent des alliances, et le droit est comme une plante vénéneuse poussant dans les sillons des champs.
Wanaweka ahadi nyingi, huapa viapo vya uongo wanapofanya mapatano; kwa hiyo mashtaka huchipuka kama magugu ya sumu katika shamba lililolimwa.
5 Pour le veau de Beth-Awên, les habitants de Samarie tremblent; oui, ses fidèles sont en deuil à son sujet, ainsi que ses prêtres qui naguère se réjouissaient en lui; car le voilà dépouillé de son éclat.
Watu wanaoishi Samaria huogopa kwa ajili ya sanamu ya ndama ya Beth-Aveni. Watu wake wataiombolezea, vivyo hivyo kuhani wake wa kuabudu sanamu, wale waliokuwa wamefurahia fahari yake, kwa sababu itaondolewa kutoka kwao kwenda uhamishoni.
6 Lui-même, on le transporte en Assyrie, comme présent au roi Protecteur; Ephraïm en recueille la honte, Israël est confus de sa résolution.
Itachukuliwa kwenda Ashuru kama ushuru kwa mfalme mkuu. Efraimu atafedheheshwa; Israeli ataaibika kwa ajili ya sanamu zake za mti.
7 Samarie est réduite à rien de même que son roi, tel un morceau de bois à la surface de l’eau.
Samaria na mfalme wake wataelea kama kijiti juu ya uso wa maji.
8 Les hauts-lieux criminels, le péché visible d’Israël, sont détruits; des ronces et des chardons poussent sur leurs autels. Alors ils diront aux montagnes: "Recouvrez-nous!" et aux collines: "Tombez sur nous!"
Mahali pa kuabudia sanamu pa uovu pataharibiwa: ndiyo dhambi ya Israeli. Miiba na mibaruti itaota na kufunika madhabahu zao. Kisha wataiambia milima, “Tufunikeni!” na vilima, “Tuangukieni!”
9 Plus qu’aux jours de Ghibea, tu as prévariqué, ô Israël! S’Ils s’étaient trouvés là, n’auraient-ils pas été atteints à Ghibea par la guerre dirigée contre les fils de l’iniquité?
“Tangu siku za Gibea, mmetenda dhambi, ee Israeli, huko ndiko mlikobaki. Je, vita havikuwapata watenda mabaya huko Gibea?
10 Au gré de mon désir, je veux les châtier; ils verront des peuples s’attrouper contre eux, pour s’être attachés à leurs deux péchés.
Wakati nitakapopenda, nitawaadhibu; mataifa yatakusanywa dhidi yao ili kuwaweka katika vifungo kwa ajili ya dhambi zao mbili.
11 Ephraïm est une génisse bien dressée, aimant à fouler le blé; mais moi, je passerai sur son cou superbe, je ferai atteler Ephraïm; il faudra que Juda laboure, que Jacob traîne la herse.
Efraimu ni mtamba wa ngʼombe aliyefundishwa ambaye hupenda kupura, hivyo nitamfunga nira juu ya shingo yake nzuri. Nitamwendesha Efraimu, Yuda lazima alime, naye Yakobo lazima avunjavunje mabonge ya udongo.
12 Faites vos semailles selon la justice et vous moissonnerez selon la loi d’amour; tracez-vous des sillons. C’Est l’heure de se mettre en quête de l’Eternel, pour qu’il vienne verser sur vous le salut.
Jipandieni wenyewe haki, vuneni matunda ya upendo usio na kikomo, vunjeni ardhi yenu isiyolimwa; kwa kuwa ni wakati wa kumtafuta Bwana, mpaka atakapokuja na kuwanyeshea juu yenu haki.
13 Mais vous avez cultivé l’iniquité et récolté le mal; vous avez mangé le fruit de la tromperie; car tu as eu confiance en ta conduite, dans la multitude de tes guerriers.
Lakini mmepanda uovu, mkavuna ubaya, mmekula tunda la udanganyifu. Kwa sababu mmetegemea nguvu zenu wenyewe na wingi wa mashujaa wenu,
14 Aussi le tumulte de la guerre éclatera-t-il contre tes troupes, et toutes tes forteresses seront-elles ruinées, comme Salmân a détruit Beth-Arbêl au jour du combat, où les mères furent écrasées avec leurs enfants.
mngurumo wa vita utainuka dhidi ya watu wako, ili kwamba ngome zako zote zitaharibiwa: kama Shalmani alivyoharibu Beth-Arbeli katika siku ile ya vita, wakati mama pamoja na watoto wao walipotupwa kwa nguvu ardhini.
15 Voilà le sort que vous prépare Béthel, à cause de l’excès de votre perversité. Dès le lever de l’aurore, c’en est complètement fini du roi d’Israël.
Ndivyo itakavyotokea kwako, ee Betheli, kwa sababu uovu wako ni mkuu. Siku ile itakapopambazuka, mfalme wa Israeli ataharibiwa kabisa.

< Osée 10 >