< 1 Chroniques 12 >

1 Or ce sont ici ceux qui allèrent trouver David à Tsiklag, lorsqu'il y était encore enfermé à cause de Saül fils de Kis, et qui étaient des plus vaillants, pour donner du secours dans la guerre,
Hawa ndio watu waliomjia Daudi huko Siklagi, wakati alikuwa amefukuzwa mbele ya Sauli mwana wa Kishi (walikuwa miongoni mwa mashujaa waliomsaidia Daudi vitani,
2 Equipés d'arcs, se servant de la main droite et de la gauche à jeter des pierres, et à tirer des flèches avec l'arc. D'entre les parents de Saül, qui étaient de Benjamin,
walikuwa na pinde na walikuwa na uwezo wa kupiga mishale au kutupa mawe kwa kombeo wakitumia mkono wa kushoto au wa kulia; hawa walikuwa ndugu zake Sauli kutoka kabila la Benyamini):
3 Ahihézer le Chef, et Joas, enfants de Sémaha, qui était de Guibha, et Jéziël, et Pelet enfants de Hazmaveth, et Beraca, et Jéhu Hanathothite,
Mkuu wao alikuwa Ahiezeri, na wa pili Yoashi, wote wana wa Shemaa Mgibeathi; pia Yezieli na Peleti wana wa Azmawethi; Beraka, Yehu Mwanathothi,
4 Et Jismahja Gabaonite, vaillant entre les trente, et même plus que les trente, et Jérémie, Jahaziël, Johanan, et Jozabad Guédérothite,
na Ishmaya Mgibeoni, shujaa miongoni mwa wale Thelathini, ambaye alikuwa kiongozi wa wale Thelathini; Yeremia, Yahazieli, Yohanani, Yozabadi, Mgederathi,
5 Elhuzaï, Jérimoth, Béhalia, Sémaria, et Séphatia Haruphien,
Eluzai, Yeremothi, Bealia, Shemaria, Shefatia, Mharufi;
6 Elkana, Jisija, Hazaréël, Johézer et Jasobham Corites,
Elikana, Ishia, Azareli, Yoezeri na Yashobeamu, wana wa Kora;
7 Et Johéla et Zébadia, enfants de Jéroham de Guédor.
Yoela na Zebadia, wana wa Yerohamu, kutoka Gedori.
8 Quelques-uns aussi des Gadites se retirèrent vers David, dans la forteresse au désert, hommes forts et vaillants, experts à la guerre, [et] maniant le bouclier et la lance. Leurs visages étaient [comme] des faces de lion, et ils semblaient des daims sur les montagnes, tant ils couraient légèrement.
Baadhi ya Wagadi wakajitenga na kujiunga na Daudi katika ngome yake huko jangwani. Walikuwa mashujaa hodari, waliokuwa tayari kwa vita na wenye uwezo wa kutumia ngao na mkuki. Nyuso zao zilikuwa nyuso za simba na walikuwa na wepesi kama paa milimani.
9 Hézer le premier, Hobadia le second, Eliab le troisième,
Ezeri alikuwa mkuu wao, Obadia alikuwa wa pili katika uongozi, Eliabu wa tatu,
10 Mismanna le quatrième, Jérémie le cinquième,
Mishmana wa nne, Yeremia wa tano,
11 Hattaï le sixième; Eliël le septième,
Atai wa sita, Elieli wa saba,
12 Johanan le huitième, Elzabad le neuvième,
Yohanani wa nane, Elzabadi wa tisa,
13 Jérémie le dixième, Macbannaï le onzième.
Yeremia wa kumi, na Makbanai wa kumi na moja.
14 Ceux-là d'entre les enfants de Gad furent Capitaines de l'armée; le moindre avait la charge de cent hommes, et le plus distingué, de mille.
Hawa Wagadi walikuwa majemadari. Aliyekuwa wa mwisho kuliko wote aliweza kuongoza askari 100, na aliyekuwa na uweza zaidi ya wote aliongoza 1,000.
15 Ce sont ceux qui passèrent le Jourdain au premier mois, au temps qu'il a accoutumé de se déborder sur tous ses rivages; et ils chassèrent ceux qui demeuraient dans les vallées, vers l'Orient et l'Occident.
Wao ndio walivuka Mto Yordani katika mwezi wa kwanza ukiwa umefurika hadi kwenye kingo zake zote na kusababisha watu wote waliokuwa wanaishi kwenye mabonde kukimbilia mashariki na wengine magharibi.
16 Il vint aussi des enfants de Benjamin et de Juda vers David à la forteresse.
Wabenyamini wengine na baadhi ya watu kutoka Yuda pia walikuja kwa Daudi katika ngome yake.
17 Et David sortit au devant d'eux et prenant la parole, il leur dit: Si vous êtes venus en paix vers moi pour m'aider, mon cœur vous sera uni; mais si c'est pour me trahir, [et me livrer] à mes ennemis, quoique je ne sois coupable d'aucune violence, que le Dieu de nos pères le voie, et qu'il en fasse la punition.
Daudi akatoka nje kuwalaki na akawaambia, “Kama mmekuja kwangu kwa amani, kunisaidia, mimi niko tayari kuwaruhusu ninyi kuungana nami. Lakini kama mmekuja ili kunisaliti kwa adui zangu wakati mimi mikono yangu haina hatia, basi Mungu wa baba zetu aone na awahukumu.”
18 Et l'esprit revêtit Hamasaï un des principaux Capitaines, [qui dit]: Que la paix soit avec toi, ô David! qu'elle soit avec toi, fils d'Isaï! que la paix soit à ceux qui t'aident, puisque ton Dieu t'aide! Et David les reçut, et les établit entre les Capitaines de ses troupes.
Kisha Roho akaja juu ya Amasai, mkuu wa wale Thelathini, naye akasema: “Sisi tu watu wako, ee Daudi! Nasi tuko pamoja na wewe, ee mwana wa Yese! Ushindi, naam, ushindi uwe kwako, pia ushindi kwa wale walio upande wako, kwa kuwa Mungu wako atakusaidia.” Kwa hiyo Daudi akawapokea na kuwafanya viongozi wa vikosi vyake vya uvamizi.
19 Il y en eut aussi de ceux de Manassé qui s'allèrent rendre à David, quand il vint avec les Philistins pour combattre contre Saül; mais ils ne leur donnèrent point de secours, parce que les Gouverneurs des Philistins, après en avoir délibéré entr'eux, le renvoyèrent, en disant: Il se tournera vers son Seigneur Saül, au péril de nos têtes.
Baadhi ya watu kutoka kabila la Manase wakajiunga na Daudi wakati alikwenda pamoja na Wafilisti, kupigana na Sauli. (Daudi na watu wake hawakuwasaidia Wafilisti kwa sababu, baada ya ushauri, watawala wao walimrudisha. Wakasema, “Itatugharimu vichwa vyetu kama Daudi atatuasi na kurudi kwa Sauli bwana wake.”)
20 Quand donc il retournait à Tsiklag, Hadna, Jozabad, Jédihaël, Micaël, Jozabad, Elihu, et Tsillethaï, Chefs des milliers qui étaient en Manassé, se tournèrent vers lui.
Daudi alipokwenda Siklagi, hawa ndio watu wa kabila la Manase waliojiunga naye: Adna, Yozabadi, Yediaeli, Mikaeli, Yozabadi, Elihu na Silethai, viongozi wa vikosi vya watu 1,000 katika kabila la Manase.
21 Et ils aidèrent David contre la troupe des Hamalécites, car ils étaient tous forts et vaillants, et ils furent faits Capitaines dans l'armée.
Walimsaidia Daudi dhidi ya makundi ya uvamizi, kwa kuwa wote walikuwa mashujaa hodari na walikuwa majemadari katika jeshi lake.
22 Et même à toute heure il venait des gens vers David pour l'aider, de sorte qu'il eut une grande armée, comme une armée de Dieu.
Siku baada ya siku watu walikuja kumsaidia Daudi, mpaka akawa na jeshi kubwa, kama jeshi la Mungu.
23 Or ce sont ici les dénombrements des hommes équipés pour la guerre, qui vinrent vers David à Hébron, afin de faire tomber sur lui le Royaume de Saül, suivant le commandement de l'Eternel.
Hawa ndio watu waliojiandaa kwa ajili ya vita waliokuja kwa Daudi huko Hebroni ili kumtwalia ufalme kutoka kwa Sauli, kama Bwana alivyokuwa amesema:
24 Des enfants de Juda, qui portaient le bouclier et la javeline, six mille huit cents, équipés pour la guerre.
watu wa Yuda, wanaochukua ngao na mikuki walikuwa 6,800 wote wakiwa tayari kwa vita.
25 Des enfants de Siméon, forts et vaillants pour la guerre, sept mille et cent.
Watu wa Simeoni, mashujaa waliokuwa tayari kwa vita walikuwa 7,100.
26 Des enfants de Lévi, quatre mille six cents.
Watu wa Lawi walikuwa 4,600,
27 Et Jéhojadah, conducteur de ceux d'Aaron et avec lui trois mille sept cents.
pamoja na Yehoyada, kiongozi wa jamaa ya Aroni, aliyekuwa pamoja na watu 3,700,
28 Et Tsadoc, jeune homme fort et vaillant, et vingt et deux des principaux de la maison de son père.
na Sadoki, kijana shujaa na hodari, aliyekuwa pamoja na maafisa ishirini na wawili kutoka jamaa yake.
29 Des enfants de Benjamin, parents de Saül, trois mille; car jusqu'alors la plus grande partie d'entr'eux avait tâché de soutenir la maison de Saül.
Watu wa Benyamini, ndugu zake Sauli, walikuwa 3,000; wengi wao walikuwa wameendelea kuwa waaminifu kwa Sauli mpaka wakati huo.
30 Des enfants d'Ephraïm vingt mille huit cents, forts et vaillants, [et] hommes de réputation dans la maison de leurs pères.
Watu wa Efraimu, mashujaa hodari 20,800, watu waliokuwa maarufu katika koo zao.
31 De la demi-Tribu de Manassé dix-huit mille, qui furent nommés par leur nom pour aller établir David Roi.
Watu wa nusu ya kabila la Manase, waliotajwa kwa majina ili waje kumweka Daudi kuwa mfalme, watu 18,000.
32 Des enfants d'Issacar, fort intelligents dans la connaissance des temps, pour savoir ce que devait faire Israël, deux cents de leurs Chefs, et tous leurs frères se conduisaient par leur avis.
Watu wa Isakari, waliofahamu majira na kujua kile ambacho Israeli inapasa kufanya, walikuwa viongozi 200, pamoja na jamaa zao wote chini ya uongozi wao.
33 De Zabulon, cinquante mille combattants, rangés en bataille avec toutes sortes d'armes, et gardant leur rang d'un cœur assuré.
Watu wa Zabuloni, askari wenye uzoefu mkubwa walioandaliwa tayari kwa vita wakiwa na silaha za kila aina, ili kumsaidia Daudi kwa uaminifu thabiti, walikuwa 50,000.
34 De Nephthali, mille capitaines, et avec eux trente-sept mille, portant le bouclier et la hallebarde.
Watu wa Naftali, maafisa 1,000, pamoja na watu 37,000 waliochukua ngao na mikuki.
35 Des Danites, vingt-huit mille six cents, rangés en bataille.
Watu wa Dani 28,600 waliokuwa tayari kwa vita.
36 D'Aser, quarante mille combattants, et gardant leur rang en bataille.
Watu wa Asheri, askari 40,000 wenye uzoefu mkubwa waliondaliwa kwa ajili ya vita.
37 De ceux de delà le Jourdain, [savoir] des Rubénites, des Gadites, et de la demi-Tribu de Manassé, six-vingt mille, avec tous les instruments de guerre pour combattre.
Na pia watu kutoka mashariki ya Yordani, watu wa Reubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, wakiwa na kila aina ya silaha, watu 120,000.
38 Tous ceux-ci, gens de guerre, rangés en bataille, vinrent tous de bon cœur à Hébron, pour établir David Roi sur tout Israël; et tout le reste d'Israël était aussi d'un même sentiment pour établir David Roi.
Wote hawa walikuwa watu wapiganaji waliojitolea kutumika katika safu zao. Walikuja Hebroni wakiwa wameamua kikamilifu kumfanya Daudi mfalme juu ya Israeli yote. Waisraeli wengine wote walikuwa pia na nia hiyo moja ya kumfanya Daudi kuwa mfalme.
39 Et ils furent là avec David, mangeant et buvant pendant trois jours; car leurs frères leur avaient préparé des vivres.
Watu hawa wakakaa huko na Daudi siku tatu, wakila na kunywa, kwa sababu jamaa zao zilikuwa zimewapatia mahitaji yao.
40 Et même ceux qui étaient les plus proches d'eux jusqu'à Issacar, et Zabulon, et Nephthali, apportaient du pain sur des ânes et sur des chameaux, sur des mulets, et sur des bœufs, de la farine, des figues sèches, des raisins secs, du vin, [et] de l'huile, [et ils amenaient] des bœufs, et des brebis en abondance; car il y avait joie en Israël.
Pia, majirani zao hata wale walio mbali hadi Isakari, Zabuloni na Naftali, walikuja wakiwaletea vyakula walivyovibeba kwa punda, ngamia, nyumbu na maksai. Kulikuwepo na wingi wa unga, maandazi ya tini, maandazi ya zabibu kavu, divai, mafuta, ngʼombe na kondoo, kwa maana kulikuwa na furaha katika Israeli.

< 1 Chroniques 12 >