< 1 Samuel 21 >

1 David donc s'en alla à Nob, vers Ahimélec le Sacrificateur; et Ahimélec tout effrayé courut au devant de David, et lui dit: D'où vient que tu es seul, et qu'il n'y a personne avec toi?
Daudi akaenda Nobu, kwa Ahimeleki kuhani. Ahimeleki akatetemeka alipokutana naye, akamuuliza, “Kwa nini uko peke yako? Kwa nini hukufuatana na mtu yeyote?”
2 Et David dit à Ahimélec le Sacrificateur: Le Roi m'a commandé quelque chose, et m'a dit: Que personne ne sache rien de l'affaire pour laquelle je t'envoie, ni de ce que je t'ai commandé; et j'ai assigné à mes gens un certain lieu.
Daudi akamjibu Ahimeleki kuhani, akisema, “Mfalme ameniagiza shughuli fulani na kuniambia, ‘Mtu yeyote asijue chochote kuhusu kazi yako wala maagizo yako!’ Kuhusu watu wangu, nimewaambia tukutane mahali fulani.
3 Maintenant donc qu'as-tu en main? donne-moi cinq pains, ou ce qui se trouvera.
Sasa basi, una nini mkononi? Nipatie mikate mitano au chochote unachoweza kupata.”
4 Et le Sacrificateur répondit à David, et dit: Je n'ai point en main de pain commun, mais du pain sacré; mais tes gens se sont-ils au moins gardés des femmes?
Lakini kuhani akamjibu Daudi, “Sina mkate wowote wa kawaida kwa sasa. Hata hivyo, ipo hapa mikate iliyowekwa wakfu, iwapo watu wamejitenga na wanawake.”
5 Et David répondit au Sacrificateur, et lui dit: Qui plus est, depuis que je suis parti, il y a déjà quatre jours, les femmes ont été éloignées de nous, et les vaisseaux de mes gens ont été saints, et ce [pain est] tenu pour commun, vu qu'aujourd'hui on en consacre [de nouveau pour le mettre] dans les vaisseaux.
Daudi akajibu, “Hakika tumejitenga na wanawake kwa siku hizi chache kama kawaida ya ninapotoka kwenda kwenye shughuli. Navyo vyombo vya wale vijana huwa ni vitakatifu hata kwenye safari ya kawaida, si zaidi sana leo vyombo vyao vitakuwa ni vitakatifu?”
6 Le Sacrificateur donc lui donna le pain sacré; car il n'y avait point là d'autre pain que les pains de proposition qui avaient été ôtés de devant l'Eternel, pour remettre du pain chaud le jour qu'on avait levé l'autre.
Hivyo kuhani akampa ile mikate iliyowekwa wakfu, kwa kuwa hapakuwepo mikate mingine isipokuwa hiyo ya Wonyesho iliyokuwa imeondolewa hapo mbele za Bwana na kubadilishwa na mingine yenye moto siku ile ilipoondolewa.
7 Or il y avait là un homme d'entre les serviteurs de Saül, retenu en ce jour-là devant l'Eternel; [cet homme] avait nom Doëg, Iduméen le plus puissant de [tous] les pasteurs de Saül.
Basi siku hiyo palikuwepo na mmoja wa watumishi wa Sauli, aliyezuiliwa mbele za Bwana; alikuwa Doegi Mwedomu, kiongozi wa wachunga wanyama wa Sauli.
8 Et David dit à Ahimélec: Mais n'as-tu point ici en main quelque hallebarde, ou quelque épée? car je n ai point pris mon épée ni mes armes sur moi, parce que l'affaire du Roi était pressée.
Daudi akamuuliza Ahimeleki, “Je, unao mkuki au upanga hapa? Sikuleta upanga wala silaha nyingine yoyote, kwa sababu shughuli ya mfalme ilikuwa ya haraka.”
9 Et le Sacrificateur dit: Voici l'épée de Goliath le Philistin, que tu tuas en la vallée du chêne, elle est enveloppée d'un drap, derrière l'Ephod; si tu la veux prendre pour toi, prends-la; car il n'y en a point ici d'autre que celle-là. Et David dit: Il n'y en a point de pareille; donne-la-moi.
Kuhani akajibu, “Upanga wa Goliathi Mfilisti, ambaye ulimuua katika Bonde la Ela, upo hapa, umefungiwa katika kitambaa nyuma ya kisibau. Kama unauhitaji, uchukue, hakuna upanga mwingine hapa ila huo tu.” Daudi akasema, “Hakuna upanga mwingine kama huo. Nipatie huo.”
10 Alors David se leva, et s'enfuit ce jour-là de devant Saül, et s'en alla vers Akis, Roi de Gath.
Siku ile Daudi akamkimbia Sauli na kwenda kwa Akishi mfalme wa Gathi.
11 Et les serviteurs d'Akis lui dirent: N'est-ce pas ici ce David, [qui est comme le] Roi du pays? n'est-ce pas celui duquel on s'entrerépondait aux danses, en disant: Saül en a tué ses mille, et David ses dix mille?
Lakini watumishi wa Akishi wakamwambia, “Je, huyu si ndiye Daudi mfalme wa nchi? Je, huyu si ndiye yule ambaye wanaimba katika ngoma zao wakisema: “‘Sauli amewaua elfu zake, naye Daudi makumi elfu yake’?”
12 Et David mit ces paroles en son cœur, et eut une fort grande peur à cause d'Akis, Roi de Gath.
Daudi akayaweka maneno haya moyoni naye akamwogopa sana Akishi mfalme wa Gathi.
13 Et il changea sa contenance devant eux, et contrefit le fou entre leurs mains; et il marquait les poteaux des portes, et faisait couler sa salive sur sa barbe.
Basi akajifanya mwendawazimu mbele yao; naye alipokuwa mikononi mwao, alitenda kama kichaa, akikwaruza kwa kutia alama juu ya milango ya lango na kuachia udelele kutiririka kwenye ndevu zake.
14 Et Akis dit à ses serviteurs: Voici, ne voyez-vous pas que c'est un homme insensé? pourquoi me l'avez-vous amené?
Akishi akawaambia watumishi wake, “Tazameni mtu huyu! Ana wazimu! Kwa nini mnamleta kwangu?
15 Manqué-je d'hommes insensés, que vous m'ayez amené celui-ci pour faire l'insensé devant moi? celui-ci entrerait-il en ma maison!
Je, mimi nimepungukiwa na wenda wazimu kiasi kwamba mmeniletea mtu huyo hapa aendelee kufanya hivi mbele yangu? Je, ilikuwa ni lazima mtu huyo aje nyumbani kwangu?”

< 1 Samuel 21 >