< 2 Rois 16 >

1 La dix-septième année de Pékach fils de Rémalia, Achaz fils de Jotham Roi de Juda, commença à régner.
Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
2 Achaz était âgé de vingt ans quand il commença à régner; et il régna seize ans à Jérusalem; et il ne fit point ce qui est droit devant l'Eternel son Dieu comme [avait fait] David son père.
Ahazi alikuwa na miaka ishirini alipoanza kutawala, akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na sita. Tofauti na Daudi baba yake, hakufanya yaliyo mema machoni pa Bwana, Mungu wake.
3 Mais il suivit le train des Rois d'Israël, et même il fit passer son fils par le feu, selon les abominations des nations que l'Eternel avait chassées de devant les enfants d'Israël.
Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, na hata akamtoa mwanawe kafara katika moto, akifuata njia za machukizo za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele ya Waisraeli.
4 Il sacrifiait aussi et faisait des encensements dans les hauts lieux, et sur les coteaux, et sous tout arbre verdoyant.
Akatoa kafara na kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu, juu ya vilima, na chini ya kila mti uliotanda.
5 Alors Retsin Roi de Syrie, et Pékach fils de Rémalia Roi d'Israël, montèrent contre Jérusalem pour lui faire la guerre, et ils assiégèrent Achaz; mais ils n'en purent point venir à bout par les armes.
Kisha Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli wakaondoka kwenda kupigana dhidi ya Yerusalemu na kumzunguka Ahazi kwa jeshi, lakini hawakuweza kumshinda.
6 En ce temps-là Retsin Roi de Syrie, remit Elath en la puissance des Syriens, car il déposséda les Juifs d'Elath, et les Syriens entrèrent à Elath, et ils y ont demeuré jusqu'à ce jour.
Wakati ule, Resini mfalme wa Aramu akaurudisha Elathi kwa Aramu kwa kuwafukuza watu wa Yuda. Kisha Waedomu wakahamia Elathi, nao wanaishi huko mpaka leo.
7 Or Achaz avait envoyé des messagers à Tiglath-piléser Roi des Assyriens, pour lui dire: Je suis ton serviteur, et ton fils; monte et délivre-moi de la main du Roi des Syriens, et de la main du Roi d'Israël, qui s'élèvent contre moi.
Ahazi akatuma wajumbe kumwambia Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru kwamba, “Mimi ni mtumishi na mtumwa wako. Njoo na uniokoe kutoka mkononi mwa mfalme wa Aramu na wa mfalme wa Israeli, ambao wananishambulia.”
8 Et Achaz avait pris l'argent et l'or qui s'était trouvé dans la maison de l'Eternel, et dans les trésors de la maison Royale, et il l'avait envoyé en don au Roi d'Assyrie.
Naye Ahazi akachukua fedha na dhahabu zilizopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme, na kuzituma kama zawadi kwa mfalme wa Ashuru.
9 Et le Roi d'Assyrie y acquiesça, et monta à Damas, et la prit, et en transporta le peuple à Kir, et fit mourir Retsin.
Mfalme wa Ashuru akamwitikia kwa kushambulia Dameski na kuiteka. Akawahamishia wenyeji wake huko Kiri, na kumuua Resini.
10 Alors le Roi Achaz s'en alla au devant de Tiglath-piléser Roi d'Assyrie, à Damas; et le Roi Achaz ayant vu l'autel qui était à Damas, envoya à Urie le Sacrificateur la figure et le modèle de cet autel, selon toute la façon qu'il avait.
Kisha Mfalme Ahazi akaenda Dameski kukutana na Tiglath-Pileseri wa Ashuru. Akaona madhabahu huko Dameski, naye akamtumia Uria kuhani mchoro wa hayo madhabahu, pamoja na maelezo ya mpango kamili wa ujenzi wake.
11 Et Urie le Sacrificateur bâtit un autel, suivant tout ce que le Roi Achaz avait mandé de Damas; Urie le Sacrificateur le fit tout semblable, en attendant que le Roi Achaz fût revenu de Damas.
Kwa hiyo Uria kuhani akajenga madhabahu kulingana na mipango yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ameituma kutoka Dameski, na akamaliza ujenzi kabla ya Mfalme Ahazi kurudi.
12 Et quand le Roi Achaz fut revenu de Damas, et eut vu l'autel, il s'en approcha, et offrit sur cet autel;
Mfalme aliporudi kutoka Dameski na kuona hayo madhabahu, akayasogelea na kutoa sadaka juu yake.
13 Et fit fumer son holocauste et son sacrifice, et versa ses aspersions, et répandit le sang de ses sacrifices de prospérité sur cet autel-là.
Akatoa sadaka yake ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka, akamimina sadaka ya kinywaji na kunyunyizia damu ya sadaka zake za amani juu ya hayo madhabahu.
14 Et quant à l'autel d'airain qui était devant l'Eternel, il le fit reculer de devant la maison, d'entre l'autel et la maison de l'Eternel, et le mit à côté de cet [autre] autel, vers le Septentrion.
Mfalme Ahazi akayaondoa madhabahu ya zamani ya shaba kutoka hapo mbele ya Hekalu la Bwana, yaliyokuwa yamesimama kati ya ingilio la Hekalu na hayo madhabahu mapya, naye akayaweka upande wa kaskazini mwa hayo madhabahu mapya.
15 Et le Roi Achaz commanda à Urie le Sacrificateur, et lui dit: Fais fumer l'holocauste du matin, et l'oblation du soir, et l'holocauste du Roi avec son gâteau, et l'holocauste de tout le peuple du pays avec leurs gâteaux et leurs aspersions sur le grand autel, et répands tout le sang des holocaustes et tout le sang des sacrifices sur cet autel; mais l'autel d'airain sera pour moi, afin de m'y enquérir [du Seigneur].
Ndipo Mfalme Ahazi akatoa amri zifuatazo kwa Uria kuhani: “Juu ya hayo madhabahu kubwa mapya, toa sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa na sadaka ya jioni ya nafaka, sadaka ya mfalme ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa ya watu wote wa nchi, pamoja na sadaka yao ya nafaka na sadaka yao ya kinywaji. Unyunyize juu ya hayo madhabahu damu yote ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu. Lakini mimi nitatumia hayo madhabahu ya zamani ya shaba kwa ajili ya kutafuta uongozi.”
16 Et Urie le Sacrificateur fit comme le Roi Achaz lui avait commandé.
Naye Uria kuhani akafanya kama Mfalme Ahazi alivyoagiza.
17 Le Roi Achaz retrancha aussi les embattements des soubassements, et en ôta les cuviers qui étaient dessus, et fit ôter la mer de dessus les bœufs d'airain, qui étaient dessous, et la mit sur un pavé de pierre.
Mfalme Ahazi akaondoa mbao za pembeni na kuondoa masinia kwenye vile vishikilio vilivyohamishika. Akaondoa ile Bahari kutoka kwenye mafahali wa shaba walioishikilia, na kuiweka kwenye kitako cha jiwe.
18 Il ôta aussi de la maison de l'Eternel le couvert du Sabbat qu'on avait bâti au Temple, et l'entrée du Roi qui était en dehors, à cause du Roi des Assyriens.
Kwa heshima ya mfalme wa Ashuru, akaliondoa pia pazia la Sabato lililokuwa limewekwa ndani ya Hekalu, na akaondoa ile njia ya kifalme ya kuingia kwenye Hekalu la Bwana.
19 Le reste des faits d'Achaz, lesquels il a faits, n'est-il pas écrit au Livre des Chroniques des Rois de Juda?
Matukio mengine ya utawala wa Ahazi na yale aliyoyafanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
20 Puis Achaz s'endormit avec ses pères, et fut enseveli avec eux en la Cité de David; et Ezéchias son fils régna en sa place.
Ahazi akalala na baba zake, naye akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Hezekia mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Rois 16 >