< Isaïe 40 >

1 Consolez, consolez mon peuple, dira votre Dieu.
Wafarijini, wafarijini watu wangu, asema Mungu wenu.
2 Parlez à Jérusalem selon son cœur, et lui criez que son temps marqué est accompli, que son iniquité est tenue pour acquittée, qu'elle a reçu de la main de l'Eternel le double pour tous ses péchés.
Sema na Yerusalemu kwa upole, umtangazie kwamba kazi yake ngumu imekamilika, kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia, kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.
3 La voix de celui qui crie au désert [est]; préparez le chemin de l'Eternel, dressez parmi les landes les sentiers à notre Dieu.
Sauti ya mtu aliaye: “Itengenezeni jangwani njia ya Bwana, nyoosheni njia kuu nyikani kwa ajili ya Mungu wetu.
4 Toute vallée sera comblée, et toute montagne et tout coteau seront abaissés, et les lieux tortus seront redressés, et les lieux raboteux seront aplanis.
Kila bonde litainuliwa, kila mlima na kilima kitashushwa; penye mabonde patanyooshwa, napo palipoparuza patasawazishwa.
5 Alors la gloire de l'Eternel se manifestera, et toute chair ensemble la verra; car la bouche de l'Eternel a parlé.
Utukufu wa Bwana utafunuliwa, nao wanadamu wote watauona pamoja. Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”
6 La voix dit; crie; et on a répondu; que crierai-je? Toute chair est [comme] l'herbe, et toute sa grâce est comme la fleur d'un champ.
Sauti husema, “Piga kelele.” Nami nikasema, “Nipige kelele gani?” “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao wote ni kama maua ya kondeni.
7 L'herbe est séchée, et la fleur est tombée, parce que le vent de l'Eternel a soufflé dessus; vraiment le peuple [est comme] l'herbe.
Majani hunyauka na maua huanguka, kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza. Hakika wanadamu ni majani.
8 L'herbe est séchée, et la fleur est tombée; mais la parole de notre Dieu demeure éternellement.
Majani hunyauka na maua huanguka, lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
9 Sion, qui annonces de bonnes nouvelles, monte sur une haute montagne; Jérusalem, qui annonces de bonnes nouvelles, élève ta voix avec force; élève-la, ne crains point; dis aux villes de Juda; voici votre Dieu.
Wewe uletaye habari njema Sayuni, panda juu ya mlima mrefu. Wewe uletaye habari njema Yerusalemu, inua sauti yako kwa kupiga kelele, inua sauti, usiogope; iambie miji ya Yuda, “Yuko hapa Mungu wenu!”
10 Voici, le Seigneur l'Eternel viendra contre le fort, et son bras dominera sur lui; voici son salaire [est] avec lui, et son loyer [marche] devant lui.
Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu, nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake. Tazameni, ujira wake u pamoja naye, nayo malipo yake yanafuatana naye.
11 Il paîtra son troupeau, comme un berger, il assemblera les agneaux entre ses bras, il les placera en son sein; il conduira celles qui allaitent.
Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo: Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake na kuwachukua karibu na moyo wake, huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.
12 Qui est celui qui a mesuré les eaux avec le creux de sa main, et qui a compassé les cieux avec la paume; qui a rassemblé [toute] la poussière de la terre dans un boisseau; et qui a pesé au crochet les montagnes, et les coteaux à la balance?
Ni nani aliyepima maji ya bahari kwenye konzi ya mkono wake, au kuzipima mbingu kwa shibiri yake? Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu, au kupima milima kwenye kipimio na vilima kwenye mizani?
13 Qui a dirigé l'Esprit de l'Eternel, ou qui étant son conseiller, lui a montré [quelque chose]?
Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana, au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?
14 Avec qui a-t-il pris conseil, et qui l'a instruit, et lui a enseigné le sentier de jugement? Qui lui a enseigné la science, et lui a montré le chemin de la prudence?
Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha, naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa? Ni nani aliyemfundisha maarifa au kumwonyesha mapito ya ufahamu?
15 Voilà, les nations sont comme une goutte qui tombe d'un sceau, et elles sont réputées comme la menue poussière d'une balance; voilà, il a jeté çà et là les Iles comme de la poudre.
Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo, ni kama vumbi jembamba juu ya mizani, huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.
16 Et le Liban ne suffirait pas pour faire le feu, et les bêtes qui y sont ne seraient pas suffisantes pour l'holocauste.
Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.
17 Toutes les nations sont devant lui comme un rien, et il ne les considère que comme de la poussière, et comme un néant.
Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu, yanaonekana yasio na thamani na zaidi ya bure kabisa.
18 A qui donc ferez-vous ressembler le [Dieu] Fort, et quelle ressemblance lui approprierez-vous?
Basi, utamlinganisha Mungu na nani? Utamlinganisha na kitu gani?
19 L'ouvrier fond l'image, et l'orfèvre étend de l'or par-dessus, et lui fond des chaînettes d'argent.
Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu, naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu na kuitengenezea mikufu ya fedha.
20 Celui qui est si pauvre qu'il n'a pas de quoi offrir, choisit un bois qui ne pourrisse point, et cherche un ouvrier expert, pour faire une image taillée qui ne bouge point.
Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii huuchagua mti usiooza. Humtafuta fundi stadi wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.
21 N'aurez-vous [jamais] de connaissance? n'écouterez-vous [jamais]? ne vous a-t-il pas été déclaré dès le commencement? ne l'avez-vous pas entendu dès les fondements de la terre?
Je, hujui? Je, hujasikia? Je, hujaambiwa tangu mwanzo? Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?
22 C'est lui qui est assis au-dessus du globe de la terre, et à qui ses habitants sont comme des sauterelles; c'est lui qui étend les cieux comme un voile, il les a même étendus comme une tente pour y habiter.
Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia, nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi. Huzitandaza mbingu kama chandarua, na kuzitandaza kama hema la kuishi.
23 C'est lui qui réduit les Princes à rien, et qui fait être les gouverneurs de la terre comme une chose de néant.
Huwafanya wakuu kuwa si kitu, na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.
24 Même ils ne seront point plantés, même ils ne seront point semés, même leur tronc ne jettera point de racine en terre; même il soufflera sur eux, et ils sécheront, et le tourbillon les emportera comme de la paille.
Mara baada ya kupandwa, mara baada ya kutiwa ardhini, mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini, ndipo huwapulizia nao wakanyauka, nao upepo wa kisulisuli huwapeperusha kama makapi.
25 A qui donc me ferez-vous ressembler, et à qui serais-je égalé? dit le Saint.
“Utanilinganisha mimi na nani? Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.
26 Elevez vos yeux en haut, et regardez; qui a créé ces choses? c'est celui qui fait sortir leur armée par ordre, et qui les appelle toutes par leur nom; il n'y en a pas une qui manque, à cause de la grandeur de ses forces, et parce qu'il excelle en puissance.
Inueni macho yenu mtazame mbinguni: Ni nani aliyeumba hivi vyote? Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine na kuziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu, hakuna hata mojawapo inayokosekana.
27 Pourquoi donc dirais-tu, ô Jacob! et pourquoi dirais-tu, ô Israël! mon état est caché à l'Eternel, et mon droit est inconnu à mon Dieu?
Kwa nini unasema, ee Yakobo, nanyi ee Israeli, kulalamika, “Njia yangu imefichwa Bwana asiione, Mungu wangu hajali shauri langu?”
28 Ne sais-tu pas et n'as-tu pas entendu que le Dieu d'éternité, l'Eternel, a créé les bornes de la terre? il ne se lasse point, et ne se travaille point, et il n'y a pas moyen de sonder son intelligence.
Je wewe, hufahamu? Je wewe, hujasikia? Bwana ni Mungu wa milele, Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala kulegea, wala hakuna hata mmoja awezaye kuupima ufahamu wake.
29 C'est lui qui donne de la force à celui qui est las, et qui multiplie la force de celui qui n'a aucune vigueur.
Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu za wadhaifu.
30 Les jeunes gens se lassent et se travaillent, même les jeunes gens d'élite tombent sans force.
Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,
31 Mais ceux qui s'attendent à l'Eternel prennent de nouvelles forces; les ailes leur reviennent comme aux aigles; ils courront; et ne se fatigueront point; ils marcheront, et ne se lasseront point.
bali wale wamtumainio Bwana atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia.

< Isaïe 40 >