< Jérémie 34 >

1 La parole qui fut [adressée] par l'Eternel à Jérémie, lorsque Nébucadnetsar Roi de Babylone, et toute son armée, tous les Royaumes de la terre, et tous les peuples qui étaient sous la puissance de sa main combattaient contre Jérusalem, et contre toutes ses villes, disant:
Wakati Nebukadneza mfalme wa Babeli na jeshi lake lote, pamoja na falme zote na mataifa katika himaya aliyotawala walipokuwa wakipigana dhidi ya Yerusalemu pamoja na miji yote inayoizunguka, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
2 Ainsi a dit l'Eternel, le Dieu d'Israël: va, et parle à Sédécias Roi de Juda, et lui dis: ainsi a dit l'Eternel, voici, je m'en vais livrer cette ville en la main du Roi de Babylone, et il la brûlera au feu;
“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli, kusema: Nenda kwa Sedekia mfalme wa Yuda umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto.
3 Et tu n'échapperas point de sa main; car certainement tu seras pris; et tu seras livré entre ses mains, et tes yeux verront les yeux du Roi de Babylone; et il parlera à toi bouche à bouche, et tu viendras dans Babylone.
Hutaweza kuepuka mkono wake, bali hakika utatekwa na kukabidhiwa kwake. Utamwona mfalme wa Babeli kwa macho yako mwenyewe, naye atazungumza nawe ana kwa ana. Nawe utakwenda Babeli.
4 Toutefois, ô Sédécias Roi de Juda, écoute la parole de l'Eternel: l'Eternel a parlé ainsi de toi: tu ne mourras point par l'épée.
“‘Lakini sikia ahadi ya Bwana, ee Sedekia mfalme wa Yuda. Hili ndilo asemalo Bwana kukuhusu: Hutakufa kwa upanga,
5 Mais tu mourras en paix, et on fera brûler sur toi des choses aromatiques, comme on en a brûlé sur tes pères, les Rois précédents qui ont été devant toi; et on te plaindra, [en disant]: hélas, Seigneur! car j'ai prononcé cette parole, dit l'Eternel.
utakufa kwa amani. Kama vile watu walivyowasha moto wa maziko kwa heshima ya baba zako, wafalme waliokutangulia, ndivyo watu watakavyowasha moto kwa heshima yako na kuomboleza, wakisema: “Ole, Ee Bwana!” Mimi mwenyewe ninaweka ahadi hii, asema Bwana.’”
6 Jérémie donc le Prophète prononça toutes ces paroles-là à Sédécias Roi de Juda, dans Jérusalem.
Ndipo nabii Yeremia akamwambia Sedekia mfalme wa Yuda mambo haya yote huko Yerusalemu,
7 Et l'armée du Roi de Babylone combattait contre Jérusalem, et contre toutes les villes de Juda qui étaient demeurées de reste, [savoir] contre Lakis, et contre Hazéka, car c'étaient [les seules] villes fortes qui restaient entre les villes de Juda.
wakati jeshi la mfalme wa Babeli lilipokuwa likipigana dhidi ya Yerusalemu na miji mingine ya Yuda ambayo bado ilikuwa imara, yaani Lakishi na Azeka. Hii ilikuwa miji pekee yenye ngome iliyobaki katika Yuda.
8 La parole qui fut [adressée] par l'Eternel à Jérémie, après que le Roi Sédécias eut traité alliance avec tout le peuple qui était à Jérusalem, pour leur publier la liberté;
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, baada ya Mfalme Sedekia kufanya agano na watu wote huko Yerusalemu ili kutangaza uhuru kwa watumwa.
9 Afin que chacun renvoyât libre son serviteur, et chacun sa servante, Hébreu ou Hébreue, et qu'aucun Juif ne fût l'esclave de son frère.
Kila mmoja alipaswa kuwaacha huru watumwa wake wa Kiebrania, wanawake na wanaume. Hakuna yeyote aliyeruhusiwa kumshikilia Myahudi mwenzake kama mtumwa.
10 Tous les principaux donc, et tout le peuple qui étaient entrés dans cette alliance, entendirent que chacun devait renvoyer libre son serviteur, et chacun sa servante, sans plus les asservir; et ils obéirent, et les renvoyèrent.
Kwa hiyo maafisa wote na watu walioingia katika agano hili wakakubali kwamba watawaacha huru watumwa wao wa kiume na wa kike, na hawatawashikilia tena kama watumwa. Wakakubali na wakawaacha huru.
11 Mais ensuite ils changèrent d'avis, et firent revenir leurs serviteurs et leurs servantes, qu'ils avaient renvoyés libres, et les assujettirent pour leur être serviteurs et servantes.
Lakini baadaye wakabadili mawazo yao, na kuwarudisha wale watumwa waliokuwa wamewaacha huru, wakawafanya tena watumwa.
12 Et la parole de l'Eternel fut [adressée] à Jérémie par l'Eternel, en disant:
Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
13 Ainsi a dit l'Eternel, le Dieu d'Israël: je traitai alliance avec vos pères, le jour que je les tirai hors du pays d'Egypte, de la maison de servitude, en disant:
“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nilifanya agano na baba zenu nilipowatoa Misri, kutoka nchi ya utumwa. Nilisema,
14 Dans la septième année vous renverrez chacun votre frère Hébreu, qui vous aura été vendu; il te servira six ans, puis tu le renverras libre d'avec toi; mais vos pères ne m'ont point écouté, et n'ont point incliné leur oreille.
‘Kila mwaka wa saba, kila mmoja wenu ni lazima amwache huru mtumwa ambaye ni Mwebrania mwenzenu aliyejiuza kwenu. Baada ya kukutumikia kwa miaka sita, ni lazima umwache huru aende zake.’ Hata hivyo baba zenu hawakunisikiliza wala kunijali.
15 Et vous vous étiez convertis aujourd'hui, et vous aviez fait ce qui [était] juste devant moi, en publiant la liberté chacun à son prochain, et vous aviez traité alliance en ma présence, dans la maison sur laquelle mon Nom est réclamé;
Hivi karibuni tu mlitubu na kufanya yaliyo sawa machoni pangu: Kila mmoja wenu aliwatangazia uhuru Waebrania wake. Hata mlifanya agano mbele zangu ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu.
16 Mais vous avez changé d'avis, et avez souillé mon Nom; car vous avez fait revenir chacun son serviteur, et chacun sa servante, que vous aviez renvoyés libres pour être à eux-mêmes, et vous les avez assujettis, afin qu'ils vous soient serviteurs et servantes.
Lakini sasa mmegeuka na kulinajisi jina langu. Kila mmoja wenu amemrudisha mtumwa wa kiume na wa kike ambao mlikuwa mmewaacha huru waende zao walikotaka. Mmewalazimisha kuwa watumwa wenu tena.
17 C'est pourquoi ainsi a dit l'Eternel: vous ne m'avez point écouté pour publier la liberté chacun à son frère, et chacun à son prochain; voici, je m'en vais publier, dit l'Eternel, la liberté contre vous à l'épée, à la peste, et à la famine; et je vous livrerai pour être transportés par tous les Royaumes de la terre.
“Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Hamkunitii mimi. Hamkutangaza uhuru kwa ndugu zenu. Hivyo sasa, ninawatangazia ninyi ‘uhuru,’ asema Bwana: ‘uhuru’ ili kuanguka kwa upanga, tauni na njaa. Nitawafanya mwe chukizo kwa falme zote za dunia.
18 Et je livrerai les hommes qui ont transgressé mon alliance, et qui n'ont point effectué les paroles de l'alliance qu'ils ont traitée devant moi, lorsqu'ils sont passés entre les deux moitiés du veau qu'ils ont coupé en deux;
Watu waliovunja agano langu, na ambao hawakutunza masharti ya agano walilofanya mbele zangu, nitawafanya kama ndama waliyemkata vipande viwili, kisha wakatembea kati ya vile vipande vya huyo ndama.
19 Les principaux de Juda, et les principaux de Jérusalem, les Eunuques, et les Sacrificateurs et tout le peuple du pays, qui ont passé entre les deux moitiés du veau;
Viongozi wa Yuda na Yerusalemu, maafisa wa mahakama, makuhani na watu wote wa nchi waliopita kati ya vile vipande vya ndama,
20 Je les livrerai, dis-je, entre les mains de leurs ennemis, et entre les mains de ceux qui cherchent leur vie; et leurs corps morts seront pour viande aux oiseaux des cieux, et aux bêtes de la terre.
nitawatia mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao. Maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.
21 Je livrerai aussi Sédécias Roi de Juda, et les principaux de sa Cour entre les mains de leurs ennemis, et entre les mains de ceux qui cherchent leur vie; savoir entre les mains de l'armée du Roi de Babylone, qui s'est retiré de devant vous.
“Nitamtia Sedekia mfalme wa Yuda na maafisa wake mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao, kwa jeshi la mfalme wa Babeli, lililokuwa limeondoka kwenu.
22 Voici, je m'en vais leur donner ordre, dit l'Eternel, et je les ferai retourner vers cette ville-ci, et ils combattront contre elle, et la prendront, et la brûleront au feu, et je mettrai les villes de Juda en désolation, tellement qu'il n'y aura personne qui y habite.
Nitatoa amri, asema Bwana, nami nitawarudisha tena katika mji huu. Watapigana dhidi yake, wautwae na kuuteketeza kwa moto. Nami nitaiangamiza miji ya Yuda hivyo pasiwe na yeyote atakayeweza kuishi humo.”

< Jérémie 34 >