< Jérémie 37 >

1 Or le Roi Sédécias, fils de Josias, régna en la place de Chonja fils de Jéhojakim, et il fut établi pour Roi sur le pays de Juda par Nébucadnetsar Roi de Babylone.
Sedekia mwana wa Yosia akafanywa kuwa mfalme wa Yuda na Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye akatawala mahali pa Yehoyakini mwana wa Yehoyakimu.
2 Mais il n'obéit point, ni lui, ni ses serviteurs, ni le peuple du pays, aux paroles de l'Eternel, qu'il avait prononcées par le moyen de Jérémie le Prophète.
Lakini sio Sedekia, wala watumishi wake, wala watu wa nchi walisikiliza maneno ya Bwana aliyonena kupitia kwa nabii Yeremia.
3 Toutefois le Roi Sédécias envoya Jéhucal fils de Sélemja, et Sophonie fils de Mahaséja Sacrificateur, vers Jérémie le Prophète, pour lui dire: fais, je te prie, requête pour nous à l'Eternel notre Dieu;
Hata hivyo, Mfalme Sedekia akamtuma Yehukali mwana wa Shelemia, pamoja na kuhani Sefania mwana wa Maaseya kwa nabii Yeremia na ujumbe huu: “Tafadhali utuombee kwa Bwana, Mungu wetu.”
4 (Car Jérémie allait et venait parmi le peuple, parce qu'on ne l'avait pas encore mis en prison.)
Wakati huu Yeremia alikuwa huru kuingia na kutoka katikati ya watu, kwa sababu alikuwa bado hajatiwa gerezani.
5 Alors l'armée de Pharaon sortit d'Egypte, et quand les Caldéens, qui assiégeaient Jérusalem, en ouïrent les nouvelles, ils se retirèrent de devant Jérusalem.
Jeshi la Farao lilikuwa limetoka Misri, nao Wakaldayo waliokuwa wameuzunguka Yerusalemu kwa majeshi waliposikia taarifa kuhusu jeshi hilo walijiondoa Yerusalemu.
6 Et la parole de l'Eternel fut [adressée] à Jérémie le Prophète, en disant:
Ndipo neno la Bwana likamjia nabii Yeremia kusema:
7 Ainsi a dit l'Eternel, le Dieu d'Israël: vous direz ainsi au Roi de Juda, qui vous a envoyés pour m'interroger: voici, l'armée de Pharaon, qui est sortie à votre secours, s'en va retourner en son pays d'Egypte.
“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Mwambie mfalme wa Yuda aliyekutuma uniulize mimi, ‘Jeshi la Farao lililotoka kuja kukusaidia litarudi katika nchi yake yenyewe, yaani Misri.
8 Et les Caldéens reviendront, et combattront contre cette ville, et la prendront, et la brûleront au feu.
Kisha Wakaldayo watarudi na kushambulia mji huu, watauteka na kuuchoma moto.’
9 Ainsi a dit l'Eternel: ne vous abusez point vous-mêmes, en disant: les Caldéens se retireront certainement de nous; car ils ne s'en retireront point.
“Hili ndilo Bwana asemalo: Msijidanganye wenyewe mkifikiri, ‘Hakika Wakaldayo watatuacha na kwenda zao.’ Hakika hawatawaacha!
10 Même quand vous auriez battu toute l'armée des Caldéens qui combattent contre vous, et qu'il n'y aurait de reste entre eux que des gens percés de blessures, ils se relèveront pourtant chacun dans sa tente, et brûleront cette ville au feu.
Hata kama mngelishinda jeshi lote la Wakaldayo linalowashambulia ninyi, na wakawa ni watu waliojeruhiwa tu waliobaki kwenye mahema yao, wangetoka na kuuchoma mji huu moto.”
11 Or il arriva que quand l'armée des Caldéens se fut retirée de devant Jérusalem, à cause de l'armée de Pharaon;
Baada ya jeshi la Wakaldayo kujiondoa kutoka Yerusalemu kwa sababu ya jeshi la Farao,
12 Jérémie sortit de Jérusalem pour s'en aller au pays de Benjamin, se glissant hors de là à travers le peuple.
Yeremia akaanza kuondoka mjini ili kwenda nchi ya Benyamini ili akapate sehemu yake ya milki miongoni mwa watu huko.
13 Mais quand il fut à la porte de Benjamin, il y avait là un capitaine de la garde, duquel le nom était Jireija, fils de Sélemja, fils de Hanania, qui saisit Jérémie le Prophète, en [lui] disant: Tu te vas rendre aux Caldéens.
Lakini alipofika kwenye Lango la Benyamini, mkuu wa walinzi, ambaye jina lake lilikuwa Iriya mwana wa Shelemia mwana wa Hanania, akamkamata Yeremia na kusema, “Wewe unakwenda kujiunga na Wakaldayo!”
14 Et Jérémie répondit: cela n'est point; je ne vais point me rendre aux Caldéens; mais il ne l'écouta point, et Jireija prit Jérémie, et l'amena vers les principaux.
Yeremia akasema, “Hiyo si kweli, mimi sijiungi na Wakaldayo.” Lakini Iriya hakumsikiliza; badala yake, akamkamata Yeremia na kumpeleka kwa maafisa.
15 Et les principaux se mirent en colère contre Jérémie, et le battirent, et le mirent en prison dans la maison de Jéhonathan le Secrétaire, car ils en avaient fait un lieu de prison.
Wakamkasirikia Yeremia, wakaamuru apigwe, na akafungwa katika nyumba ya Yonathani mwandishi waliyokuwa wameifanya gereza.
16 Et ainsi Jérémie entra dans la fosse, et dans les cachots; et Jérémie y demeura plusieurs jours.
Yeremia akawekwa kwenye chumba kilichofukuliwa chini, kilichojengwa kwa zege ndani ya gereza chini ya ngome, akakaa huko kwa muda mrefu.
17 Mais le Roi Sédécias y envoya, et l'en tira, et il l'interrogea en secret dans sa maison, et lui dit: y a-t-il quelque parole de par l'Eternel? Et Jérémie répondit: il y en a; et lui dit: tu seras livré entre les mains du Roi de Babylone.
Kisha Mfalme Sedekia akatumana aletwe katika jumba la kifalme, mahali alipomuuliza kwa siri, “Je, kuna neno lolote kutoka kwa Bwana?” Yeremia akajibu, “Ndiyo, utatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli.”
18 Puis Jérémie dit au Roi Sédécias: quelle faute ai-je commise contre toi, et envers tes serviteurs, et envers ce peuple, pour m'avoir mis en prison?
Kisha Yeremia akamwambia Mfalme Sedekia, “Nimefanya kosa gani dhidi yako na maafisa wako au watu hawa, hata ukanitia gerezani?
19 Mais où sont vos Prophètes qui vous prophétisaient, en disant: le Roi de Babylone ne reviendra point contre vous, ni contre ce pays?
Wako wapi manabii wako waliokutabiria wakisema, ‘Mfalme wa Babeli hatakushambulia wewe wala nchi hii?’
20 Or écoute maintenant, je te prie, ô Roi mon Seigneur! et que maintenant ma supplication soit reçue devant ta face, et ne me renvoie point dans la maison de Jéhonathan le Secrétaire, de peur que je n'y meure.
Lakini sasa, bwana wangu mfalme, tafadhali sikiliza. Niruhusu nilete maombi yangu mbele yako, usinirudishe kwenye nyumba ya Yonathani mwandishi, nisije nikafia humo.”
21 C'est pourquoi le Roi Sédécias commanda qu'on gardât Jérémie dans la cour de la prison, et qu'on lui donnât tous les jours un pain de la place des boulangers, jusqu’à ce que tout le pain de la ville fût consumé. Ainsi Jérémie demeura dans la cour de la prison.
Ndipo Mfalme Sedekia akatoa maagizo Yeremia awekwe katika ua wa walinzi, na apewe mkate kutoka mitaa ya waokaji kila siku mpaka mikate yote katika mji itakapokwisha. Kwa hiyo Yeremia akabaki katika ua wa walinzi.

< Jérémie 37 >