< דברי הימים א 6 >

בני לוי גרשון קהת ומררי 1
Wana wa Levi walikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
ובני קהת--עמרם יצהר וחברון ועזיאל 2
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
ובני עמרם אהרן ומשה ומרים ובני אהרן--נדב ואביהוא אלעזר ואיתמר 3
Wana wa Amramu walikuwa Aruni, Musa, Miriamu. Wana wa Aruni walikuwa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.
אלעזר הוליד את פינחס פינחס הליד את אבישוע 4
Eleazari akawa baba wa Finehasi, na Finehasi akawa baba wa Abishua.
ואבישוע הוליד את בקי ובקי הוליד את עזי 5
Abishua akawa baba wa Buki, na Buki akawa baba wa Uzi.
ועזי הוליד את זרחיה וזרחיה הוליד את מריות 6
Uzi akawa baba wa Zerahia, na Zerahia akawa baba wa Meraioti.
מריות הוליד את אמריה ואמריה הוליד את אחיטוב 7
Meraioti akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
ואחיטוב הוליד את צדוק וצדוק הוליד את אחימעץ 8
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Ahimazi.
ואחימעץ הוליד את עזריה ועזריה הוליד את יוחנן 9
Ahimazi akawa baba wa Azaria, na Azaria akawa baba wa Yohanani.
ויוחנן הוליד את עזריה הוא אשר כהן בבית אשר בנה שלמה בירושלם 10
Yohanani akawa baba wa Azaria, aliye hudumu katika hekalu alilo lijenga Sulemani ndaniya Yerusalemu.
ויולד עזריה את אמריה ואמריה הוליד את אחיטוב 11
Azaria akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
ואחיטוב הוליד את צדוק וצדוק הוליד את שלום 12
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Shalumu.
ושלום הוליד את חלקיה וחלקיה הוליד את עזריה 13
Shalumu akawa baba wa Hilikia, na Hilikia akawa baba wa Azaria.
ועזריה הוליד את שריה ושריה הוליד את יהוצדק 14
Azaria akawa baba Seraia, na Seraia akawa baba wa Yehozadaki.
ויהוצדק הלך--בהגלות יהוה את יהודה וירושלם ביד נבכדנאצר 15
Yehozadaki akaenda matekani Yahweh alipo wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.
בני לוי גרשם קהת ומררי 16
Wana wa Levi walikuwa Gerishomu, Kohathi, na Merari.
ואלה שמות בני גרשום לבני ושמעי 17
Wana wa Gerishomu walikuwa Libini na Shimei.
ובני קהת--עמרם ויצהר וחברון ועזיאל 18
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
בני מררי מחלי ומשי ואלה משפחות הלוי לאבתיהם 19
Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Hawa walikuwa koo za Walawi kwa familia za baba zao.
לגרשום--לבני בנו יחת בנו זמה בנו 20
Uzao wa Gerishomu ulianza na mwanae Libini. Mwana wa Libini alikuwa Jahathi. Mwanae alikuwa Zima.
יואח בנו עדו בנו זרח בנו יאתרי בנו 21
Mwanae alikuwa Yoa. Mwanae alikuwa alikuwa Ido. Mwanae alikuwa Zera. Mwanae alikuwa Yeatherai.
בני קהת--עמינדב בנו קרח בנו אסיר בנו 22
Uzao wa Kohathi ulianza na mwanae Aminadabu. Mwanae alikuwa Kora. Mwanae alikuwa Asiri.
אלקנה בנו ואביסף בנו ואסיר בנו 23
Mwanae alikuwa Elikana. Mwanae alikuwa Ebiasa. Mwanae alikuwa Asiri.
תחת בנו אוריאל בנו עזיה בנו ושאול בנו 24
Mwanae alikuwa Tahathi. Mwanae alikuwa Urieli. Mwanae alikuwa uzia. Mwanae alikuwa Shauli.
ובני אלקנה--עמשי ואחימות 25
Wana wa Elikana walikuwa Amasai, Ahimothi, na Elikana.
אלקנה--בנו (בני) אלקנה צופי בנו ונחת בנו 26
Mwana wa huyu Elikana wa pili alikuwa Zofai. Mwanae alikuwa Nahathi.
אליאב בנו ירחם בנו אלקנה בנו 27
Mwanae alikuwa Eliabu. Mwanae alikuwa Yehoramu. Mwanae alikuwa Elikana.
ובני שמואל הבכר ושני ואביה 28
Wana wa Samwali walikuwa mzaliwa wa kwanza, Yoeli, na Abija, wa pili.
בני מררי מחלי לבני בנו שמעי בנו עזה בנו 29
Mwana wa Merari alikuwa Mahili. Mwanae alikuwa Libini.
שמעא בנו חגיה בנו עשיה בנו 30
Mwanae alikuwa Shimei. Mwanae alikuwa Uza. Mwanae alikuwa Shimea. Mwanae alikuwa Hagia. Mwana alikuwa Asaia.
ואלה אשר העמיד דויד על ידי שיר--בית יהוה ממנוח הארון 31
Haya ndio majina ya wanaume ambao Daudi waliwaeka kusimamia muziki katika nyumba ya Yahweh, baada ya sanduku kuja hapo.
ויהיו משרתים לפני משכן אהל מועד בשיר עד בנות שלמה את בית יהוה בירושלם ויעמדו כמשפטם על עבודתם 32
Walitumika kwa kuimba mbele ya hema, hema la kukutania, mpaka Sulemani alipo jenga nyumba ya Yahweh ndani ya Yerusalemu. Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa.
ואלה העמדים ובניהם מבני הקהתי--הימן המשורר בן יואל בן שמואל 33
Hawa walitumika pamoja na wana wao. Katika makabila ya Wakohathi alitoka Hemani mwana muziki. Babu zake walikuwa hawa, kurudi nyuma ya wakati: Hemani alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Samweli.
בן אלקנה בן ירחם בן אליאל בן תוח 34
Samweli alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Yerohamu. Yerohamu alikuwa mwana wa Elieli. Elieli alikuwa mwana wa Toa.
בן ציף (צוף) בן אלקנה בן מחת בן עמשי 35
Toa alikuwa mwana wa Zufi. Zufi alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Mahathi. Mahathi alikuwa mwana wa Amasai. Amasai alikuwa mwana wa Elikana.
בן אלקנה בן יואל בן עזריה בן צפניה 36
Elikana alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Azaria. Azaria alikuwa mwana wa Zefania.
בן תחת בן אסיר בן אביסף בן קרח 37
Zefania alikuwa mwana wa Tahathi. Tahathi alikuwa mwana wa Asiri. Asiri alikuwa mwana wa Ebiasa. Ebiasa alikuwa mwana wa Kora.
בן יצהר בן קהת בן לוי בן ישראל 38
Kora alikuwa mwana wa Izhari. Izhari alikuwa mwana wa Kohathi. Kohathi alikuwa mwana wa Levi. Levi alikuwa mwana wa Israeli.
ואחיו אסף העמד על ימינו--אסף בן ברכיהו בן שמעא 39
Msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliye simama mkono wake wa kuume. Asafu alikuwa mwana Berekia. Berekia alikuwa mwana wa Shimea.
בן מיכאל בן בעשיה בן מלכיה 40
Shimea alikuwa mwana Mikaeli. Mikaeli alikuwa mwana wa Baaseia. Baaseia alikuwa mwana wa Malikiya.
בן אתני בן זרח בן עדיה 41
Malikiya alikuwa mwana wa Ethini. Ethini alikuwa mwana wa Zera. Zera alikuwa mwana wa Adaia.
בן איתן בן זמה בן שמעי 42
Adaia alikuwa mwana wa Ethani. Ethani alikuwa mwana wa Zima. Zima alikuwa mwana wa Shimei.
בן יחת בן גרשם בן לוי 43
Shimei alikuwa mwana wa Yahathi. Yahathi alikuwa mwana wa Gerishomu. Gerishomu alikuwa mwana wa Levi.
ובני מררי אחיהם על השמאול--איתן בן קישי בן עבדי בן מלוך 44
Upande wa mkono wa koshoto wa Hemani walikuwa wasaidizi wake wana wa Merari. Alikuwa Ethani mwana wa Kishi. Kishi alikuwa mwana wa Abdi. Abdi alikuwa mwana wa Maluki.
בן חשביה בן אמציה בן חלקיה 45
Maluki alikuwa mwana wa Hashabia. Hashabia alikuwa mwana wa Amazia. Amazia alikuwa mwana wa Hilikia.
בן אמצי בן בני בן שמר 46
Hilikia alikuwa mwana wa Amzi. Amzi alikuwa mwana wa Bani. Bani alikuwa mwana wa Shemeri.
בן מחלי בן מושי בן מררי בן לוי 47
Shemeri alikuwa mwana wa Mahili. Mahili alikuwa mwana wa Mushi. Mushi alikuwa mwana wa Merari. Merari alikuwa mwana wa Levi.
ואחיהם הלוים נתונים--לכל עבודת משכן בית האלהים 48
Walawi, alipangiwa kufanya kazi zote za hema, nyumba ya Mungu.
ואהרן ובניו מקטירים על מזבח העולה ועל מזבח הקטרת לכל מלאכת קדש הקדשים ולכפר על ישראל ככל אשר צוה משה עבד האלהים 49
Aruni na wana wake walitoa sadaka katika madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketeza; na sadaka katika madhabahu ya uvumba kwa kazi zote katika pa patakatifu. Hizi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli, kwa kadiri ya yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu aliwaamuru.
ואלה בני אהרן--אלעזר בנו פינחס בנו אבישוע בנו 50
Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo: Mwana wa Aruni alikuwa Eleazari. Mwana Eleazari alikuwa Finehasi. Mwana wa Finehasi alikuwa Abishua.
בקי בנו עזי בנו זרחיה בנו 51
Mwana wa Abishua alikuwa Buki. Mwana wa Buki alikuwa Uzi. Mwana wa Buki alikuwa Zerahia.
מריות בנו אמריה בנו אחיטוב בנו 52
Mwana wa Zerahia alikuwa Meraiothi. Mwana wa Meraiothi alikuwa Amaria. Mwana wa Amaria alikuwa Ahitubi.
צדוק בנו אחימעץ בנו 53
Mwana wa Ahitubi alikuwa Zadoki. Mwana wa Zadoki alikuwa Ahimazi.
ואלה מושבותם לטירותם בגבולם--לבני אהרן למשפחת הקהתי כי להם היה הגורל 54
Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao).
ויתנו להם את חברון בארץ יהודה ואת מגרשיה סביבתיה 55
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda na nchi ya malisho,
ואת שדה העיר ואת חצריה--נתנו לכלב בן יפנה 56
lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
ולבני אהרן נתנו את ערי המקלט--את חברון ואת לבנה ואת מגרשיה ואת יתר ואת אשתמע ואת מגרשיה 57
Kwa wazao wa Aruni waliwapa: Hebroni ( mji wa makimblio), na Libina pamoja na nchi ya malisho, Yatiri, Eshitemoa pamoja na nchi ya malisho,
ואת חילז ואת מגרשיה את דביר ואת מגרשיה 58
Hileni pamoja na nchi ya malisho, na Debiri pamoja na nchi ya malisho.
ואת עשן ואת מגרשיה ואת בית שמש ואת מגרשיה 59
Waliwapa uzao wa Aruni: Ashani pamoja na nchi ya malisho na Bethi Shemeshi pamoja na nchi ya malisho;
וממטה בנימן את גבע ואת מגרשיה ואת עלמת ואת מגרשיה ואת ענתות ואת מגרשיה כל עריהם שלש עשרה עיר במשפחותיהם 60
na kutoka katika kabila la Benjamini walipewa Geba pamoja na nchi ya malisho, Alemethi pamoja na nchi ya malisho, na Anothothi na nchi ya malisho. Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu.
ולבני קהת הנותרים ממשפחת המטה ממחצית מטה חצי מנשה בגורל--ערים עשר 61
Uzao mwengine wa Kohathi waliwapa kwa sehemu miji kumi kutoka kwa kabila la Manase.
ולבני גרשום למשפחותם ממטה יששכר וממטה אשר וממטה נפתלי וממטה מנשה בבשן--ערים שלש עשרה 62
Kwa uzao wa Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri, Naftali, na nusu ya kabila la Manase huko Bashani.
לבני מררי למשפחותם ממטה ראובן וממטה גד וממטה זבלון בגורל--ערים שתים עשרה 63
Kwa uzao wa Merari walipewa miji kumi, kulingana na koo zao, kutoka kwa makabila ya Rubeni, Gadi, na Zebuluni.
ויתנו בני ישראל ללוים את הערים ואת מגרשיהם 64
Hivyo watu wa Israeli walitoa hii miji pamoja na nchi za malisho kwa Walawi.
ויתנו בגורל ממטה בני יהודה וממטה בני שמעון וממטה בני בנימן--את הערים האלה אשר יקראו אתהם בשמות 65
Walitoa kwa sehemu miji iliyo tajwa awali kutoka katika kabila la Yuda, Simeoni, na Benjamini.
וממשפחות בני קהת--ויהי ערי גבולם ממטה אפרים 66
Kwa baadhi ya koo za Wakohathi walitoa miji kutoka kwa kabila la Efraimu.
ויתנו להם את ערי המקלט את שכם ואת מגרשיה--בהר אפרים ואת גזר ואת מגרשיה 67
Waliwapa: Shekemu ( mji wa makimbilio) pamoja na nchi ya malisho katika milima ya Efraimu, Gezeri na nchi ya malisho,
ואת יקמעם ואת מגרשיה ואת בית חורון ואת מגרשיה 68
Jokimeamu pamoja na nchi ya malisho, Bethi Horoni pamoja na nchi ya malisho,
ואת אילון ואת מגרשיה ואת גת רמון ואת מגרשיה 69
Aiyaloni pamoja na nchi ya malisho, na Gathi Rimoni pamoja na nchi ya malisho.
וממחצית מטה מנשה את ענר ואת מגרשיה ואת בלעם ואת מגרשיה--למשפחת לבני קהת הנותרים 70
Nusu ya kabila la Manase waliwapa Wakohathi: Aneri pamoja na nchi ya malisho na Bileamu pamoja na nchi ya malisho. Hizi zikawa mali za koo za Wakohathi.
לבני גרשום--ממשפחת חצי מטה מנשה את גולן בבשן ואת מגרשיה ואת עשתרות ואת מגרשיה 71
Kwa uzao wa Gerishomu kutoka koo za nusu ya kabila la Manase, waliwapa: Golani huko Baashani na nchi ya malisho na Ashitarothi pamoja na nchi ya malisho.
וממטה יששכר את קדש ואת מגרשיה את דברת ואת מגרשיה 72
Kabila la Isakari liliwapa uzao wa Gerishomu: Kedeshi pamoja na nchi ya malisho, Dabera pamoja na nchi ya malisho,
ואת ראמות ואת מגרשיה ואת ענם ואת מגרשיה 73
Ramothi pamoja na nchi ya malisho, na Anemu pamoja na nchi ya malisho.
וממטה אשר את משל ואת מגרשיה ואת עבדון ואת מגרשיה 74
Isakari alipokea kutoka kwa kabila la Asheri: Mashali pamoja na nchi ya malisho, Abdoni pamoja na nchi ya malisho,
ואת חוקק ואת מגרשיה ואת רחב ואת מגרשיה 75
Hukoki pamoja na nchi ya malisho, na Rehobu pamoja na nchi ya malisho.
וממטה נפתלי את קדש בגליל ואת מגרשיה ואת חמון ואת מגרשיה ואת קריתים ואת מגרשיה 76
Walipokea kutoka kabila la Naftali: Kedeshi iliyo Galileya pamoja na nchi ya malisho, Hamoni pamoja na nchi ya malisho, na Kiriathaimu pamoja na nchi ya malisho.
לבני מררי הנותרים--ממטה זבלון את רמונו ואת מגרשיה את תבור ואת מגרשיה 77
Kwa Walawi wengine, uzao wa Merari, walipewa kutoka kabila la Zebuluni: Rimono pamoja na nchi ya malisho na Tabori pamoja na nchi ya malisho.
ומעבר לירדן ירחו למזרח הירדן--ממטה ראובן את בצר במדבר ואת מגרשיה ואת יהצה ואת מגרשיה 78
Kwa wao pia walipewa, upande wa pili wa Yordani huko Yeriko, kwa upande wa mashariki mwa mto: Bezeri katika jangwa pamoja na nchi ya malisho, Yahzahi pamoja na nchi ya malisho,
ואת קדמות ואת מגרשיה ואת מיפעת ואת מגרשיה 79
Kedemothi pamoka na nchi ya malisho, ma Mefathi pamoja na nchi ya malisho. Hizi zilitolewa kutoka kabila la Rubeni.
וממטה גד--את ראמות בגלעד ואת מגרשיה ואת מחנים ואת מגרשיה 80
Walawi walipokea kutoka kabila la Gadi: Ramothi ya Gileadi pamoja na nchi ya malisho, Mahanaimu pamoja na nchi ya malisho,
ואת חשבון ואת מגרשיה ואת יעזיר ואת מגרשיה 81
Heshiboni pamoja na nchi ya malisho, na Yazeri pamoja na nchi ya malisho.

< דברי הימים א 6 >