< מִשְׁלֵי 20 >

לץ היין המה שכר וכל-שגה בו לא יחכם 1
Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
נהם ככפיר אימת מלך מתעברו חוטא נפשו 2
Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
כבוד לאיש שבת מריב וכל-אויל יתגלע 3
Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
מחרף עצל לא-יחרש ישאל (ושאל) בקציר ואין 4
Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
מים עמקים עצה בלב-איש ואיש תבונה ידלנה 5
Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
רב-אדם--יקרא איש חסדו ואיש אמונים מי ימצא 6
Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
מתהלך בתמו צדיק אשרי בניו אחריו 7
Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
מלך יושב על-כסא-דין-- מזרה בעיניו כל-רע 8
Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
מי-יאמר זכיתי לבי טהרתי מחטאתי 9
Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
אבן ואבן איפה ואיפה-- תועבת יהוה גם-שניהם 10
Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
גם במעלליו יתנכר-נער-- אם-זך ואם-ישר פעלו 11
Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
אזן שמעת ועין ראה-- יהוה עשה גם-שניהם 12
Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
אל-תאהב שנה פן-תורש פקח עיניך שבע-לחם 13
Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
רע רע יאמר הקונה ואזל לו אז יתהלל 14
“Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
יש זהב ורב-פנינים וכלי יקר שפתי-דעת 15
Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
לקח-בגדו כי-ערב זר ובעד נכרים (נכריה) חבלהו 16
Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
ערב לאיש לחם שקר ואחר ימלא-פיהו חצץ 17
Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
מחשבות בעצה תכון ובתחבלות עשה מלחמה 18
Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
גולה-סוד הולך רכיל ולפתה שפתיו לא תתערב 19
Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
מקלל אביו ואמו-- ידעך נרו באישון (באשון) חשך 20
Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
נחלה מבחלת (מבהלת) בראשונה ואחריתה לא תברך 21
Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
אל-תאמר אשלמה-רע קוה ליהוה וישע לך 22
Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
תועבת יהוה אבן ואבן ומאזני מרמה לא-טוב 23
Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
מיהוה מצעדי-גבר ואדם מה-יבין דרכו 24
Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
מוקש אדם ילע קדש ואחר נדרים לבקר 25
Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
מזרה רשעים מלך חכם וישב עליהם אופן 26
Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
נר יהוה נשמת אדם חפש כל-חדרי-בטן 27
Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
חסד ואמת יצרו-מלך וסעד בחסד כסאו 28
Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
תפארת בחורים כחם והדר זקנים שיבה 29
Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
חברות פצע תמריק (תמרוק) ברע ומכות חדרי-בטן 30
Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.

< מִשְׁלֵי 20 >