< תהילים 22 >

למנצח על-אילת השחר מזמור לדוד ב אלי אלי למה עזבתני רחוק מישועתי דברי שאגתי 1
Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali na wokovu wangu na mbali na maneno yangu yenye uchungu?
אלהי--אקרא יומם ולא תענה ולילה ולא-דמיה לי 2
Mungu wangu, ninalia mchana kutwa, lakini haunijibu, na wakati wa usiku sinyamazi!
ואתה קדוש-- יושב תהלות ישראל 3
Bado wewe ni mtakatifu; wewe umekaa kama mfalme pamoja na sifa za Israeli.
בך בטחו אבתינו בטחו ותפלטמו 4
Mababu zetu walikuamini wewe, na wewe uliwaokoa wao.
אליך זעקו ונמלטו בך בטחו ולא-בושו 5
Walikulilia wewe nao waka okolewa. Wao walikuamini wewe na hawakuvunjwa moyo.
ואנכי תולעת ולא-איש חרפת אדם ובזוי עם 6
Bali mimi ni funza na sio mtu, nisiye faa kwa ubinadamu na hudharauliwa na watu.
כל-ראי ילעגו לי יפטירו בשפה יניעו ראש 7
Wale wote wanionao hunisuta; hunidhihaki; hunitikisia vichwa vyao.
גל אל-יהוה יפלטהו יצילהו כי חפץ בו 8
Wao husema, “Yeye anamwamini Yahwe; mwache Yahwe amuokoe. Mwache amuokoe yeye, kwa kuwa yeye anampendeza sana Yeye.”
כי-אתה גחי מבטן מבטיחי על-שדי אמי 9
Kwa kuwa wewe ulinileta kutoka tumboni; wewe ulinifanya nikuamini wewe wakati nikiwa nanyonya matiti ya mama yangu.
עליך השלכתי מרחם מבטן אמי אלי אתה 10
Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
אל-תרחק ממני כי-צרה קרובה כי-אין עוזר 11
Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
סבבוני פרים רבים אבירי בשן כתרוני 12
Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
פצו עלי פיהם אריה טרף ושאג 13
Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
כמים נשפכתי-- והתפרדו כל-עצמותי היה לבי כדונג נמס בתוך מעי 14
Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
יבש כחרש כחי ולשוני מדבק מלקוחי ולעפר-מות תשפתני 15
Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
כי סבבוני כלבים עדת מרעים הקיפוני כארי ידי ורגלי 16
Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
אספר כל-עצמותי המה יביטו יראו-בי 17
Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
יחלקו בגדי להם ועל-לבושי יפילו גורל 18
Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
ואתה יהוה אל-תרחק אילותי לעזרתי חושה 19
Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
הצילה מחרב נפשי מיד-כלב יחידתי 20
Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
הושיעני מפי אריה ומקרני רמים עניתני 21
Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
אספרה שמך לאחי בתוך קהל אהללך 22
Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.
יראי יהוה הללוהו-- כל-זרע יעקב כבדוהו וגורו ממנו כל-זרע ישראל 23
Ninyi mnao mwogopa Yahwe, msifuni yeye! Ninyi nyote kizazi cha Yakobo, muheshimuni yeye! Simameni katika hofu yake, ninyi nyote kizazi cha Israeli!
כי לא-בזה ולא שקץ ענות עני-- ולא-הסתיר פניו ממנו ובשועו אליו שמע 24
Kwa kuwa haja dharau au kuchukia mateso ya aliye taabishwa; Yahwe hajamficha uso wake yeye; pindi wale walio taabishwa walipo mlilia yeye, yeye alisikia.
מאתך תהלתי בקהל רב--נדרי אשלם נגד יראיו 25
Yahwe, katika kusanyiko la watu wako nitakusifu kwa yale uliyo tenda; nami nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanao muhofu yeye.
יאכלו ענוים וישבעו-- יהללו יהוה דרשיו יחי לבבכם לעד 26
Walio onewa watakula na kutosheka; wale ambao humtafuta Yahwe watamsifu yeye. Mioyo yenu iishi milele.
יזכרו וישבו אל-יהוה-- כל-אפסי-ארץ וישתחוו לפניך כל-משפחות גוים 27
Watu wote wa duniani watakumbuka na kumrudia Yahwe; familia zote za mataifa watapiga magoti chini mbele yako.
כי ליהוה המלוכה ומשל בגוים 28
Kwa kuwa utawala ni wa Yahwe; yeye ni mtawala wa mataifa.
אכלו וישתחוו כל-דשני-ארץ-- לפניו יכרעו כל-יורדי עפר ונפשו לא חיה 29
Watu wote wa duniani waliofanikiwa wata sherekea na wata abudu; wale wote washukao katika mavumbi watapiga magoti mbele zake, wale ambao hawawezi kulinda maisha yao wenyewe.
זרע יעבדנו יספר לאדני לדור 30
Kizazi kijacho kitamtumikia yeye; wao watakiambia kizazi kinachofuatia kuhusu Bwana.
יבאו ויגידו צדקתו לעם נולד כי עשה 31
Wao watakuja na kuzungumza kuhusu haki yake; wao watawaambia watu ambao bado hawaja zaliwa yale ambayo Yahwe ameyafanya!

< תהילים 22 >