< תהילים 22 >
למנצח על-אילת השחר מזמור לדוד ב אלי אלי למה עזבתני רחוק מישועתי דברי שאגתי | 1 |
Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali na wokovu wangu na mbali na maneno yangu yenye uchungu?
אלהי--אקרא יומם ולא תענה ולילה ולא-דמיה לי | 2 |
Mungu wangu, ninalia mchana kutwa, lakini haunijibu, na wakati wa usiku sinyamazi!
ואתה קדוש-- יושב תהלות ישראל | 3 |
Bado wewe ni mtakatifu; wewe umekaa kama mfalme pamoja na sifa za Israeli.
בך בטחו אבתינו בטחו ותפלטמו | 4 |
Mababu zetu walikuamini wewe, na wewe uliwaokoa wao.
אליך זעקו ונמלטו בך בטחו ולא-בושו | 5 |
Walikulilia wewe nao waka okolewa. Wao walikuamini wewe na hawakuvunjwa moyo.
ואנכי תולעת ולא-איש חרפת אדם ובזוי עם | 6 |
Bali mimi ni funza na sio mtu, nisiye faa kwa ubinadamu na hudharauliwa na watu.
כל-ראי ילעגו לי יפטירו בשפה יניעו ראש | 7 |
Wale wote wanionao hunisuta; hunidhihaki; hunitikisia vichwa vyao.
גל אל-יהוה יפלטהו יצילהו כי חפץ בו | 8 |
Wao husema, “Yeye anamwamini Yahwe; mwache Yahwe amuokoe. Mwache amuokoe yeye, kwa kuwa yeye anampendeza sana Yeye.”
כי-אתה גחי מבטן מבטיחי על-שדי אמי | 9 |
Kwa kuwa wewe ulinileta kutoka tumboni; wewe ulinifanya nikuamini wewe wakati nikiwa nanyonya matiti ya mama yangu.
עליך השלכתי מרחם מבטן אמי אלי אתה | 10 |
Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
אל-תרחק ממני כי-צרה קרובה כי-אין עוזר | 11 |
Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
סבבוני פרים רבים אבירי בשן כתרוני | 12 |
Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
פצו עלי פיהם אריה טרף ושאג | 13 |
Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
כמים נשפכתי-- והתפרדו כל-עצמותי היה לבי כדונג נמס בתוך מעי | 14 |
Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
יבש כחרש כחי ולשוני מדבק מלקוחי ולעפר-מות תשפתני | 15 |
Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
כי סבבוני כלבים עדת מרעים הקיפוני כארי ידי ורגלי | 16 |
Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
אספר כל-עצמותי המה יביטו יראו-בי | 17 |
Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
יחלקו בגדי להם ועל-לבושי יפילו גורל | 18 |
Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
ואתה יהוה אל-תרחק אילותי לעזרתי חושה | 19 |
Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
הצילה מחרב נפשי מיד-כלב יחידתי | 20 |
Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
הושיעני מפי אריה ומקרני רמים עניתני | 21 |
Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
אספרה שמך לאחי בתוך קהל אהללך | 22 |
Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.
יראי יהוה הללוהו-- כל-זרע יעקב כבדוהו וגורו ממנו כל-זרע ישראל | 23 |
Ninyi mnao mwogopa Yahwe, msifuni yeye! Ninyi nyote kizazi cha Yakobo, muheshimuni yeye! Simameni katika hofu yake, ninyi nyote kizazi cha Israeli!
כי לא-בזה ולא שקץ ענות עני-- ולא-הסתיר פניו ממנו ובשועו אליו שמע | 24 |
Kwa kuwa haja dharau au kuchukia mateso ya aliye taabishwa; Yahwe hajamficha uso wake yeye; pindi wale walio taabishwa walipo mlilia yeye, yeye alisikia.
מאתך תהלתי בקהל רב--נדרי אשלם נגד יראיו | 25 |
Yahwe, katika kusanyiko la watu wako nitakusifu kwa yale uliyo tenda; nami nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanao muhofu yeye.
יאכלו ענוים וישבעו-- יהללו יהוה דרשיו יחי לבבכם לעד | 26 |
Walio onewa watakula na kutosheka; wale ambao humtafuta Yahwe watamsifu yeye. Mioyo yenu iishi milele.
יזכרו וישבו אל-יהוה-- כל-אפסי-ארץ וישתחוו לפניך כל-משפחות גוים | 27 |
Watu wote wa duniani watakumbuka na kumrudia Yahwe; familia zote za mataifa watapiga magoti chini mbele yako.
כי ליהוה המלוכה ומשל בגוים | 28 |
Kwa kuwa utawala ni wa Yahwe; yeye ni mtawala wa mataifa.
אכלו וישתחוו כל-דשני-ארץ-- לפניו יכרעו כל-יורדי עפר ונפשו לא חיה | 29 |
Watu wote wa duniani waliofanikiwa wata sherekea na wata abudu; wale wote washukao katika mavumbi watapiga magoti mbele zake, wale ambao hawawezi kulinda maisha yao wenyewe.
זרע יעבדנו יספר לאדני לדור | 30 |
Kizazi kijacho kitamtumikia yeye; wao watakiambia kizazi kinachofuatia kuhusu Bwana.
יבאו ויגידו צדקתו לעם נולד כי עשה | 31 |
Wao watakuja na kuzungumza kuhusu haki yake; wao watawaambia watu ambao bado hawaja zaliwa yale ambayo Yahwe ameyafanya!