< Giosué 13 >

1 ORA, quando Giosuè fu diventato vecchio [ed] attempato, il Signore disse: Tu sei diventato vecchio [ed] attempato, e vi resta ancora molto gran paese a conquistare.
Yoshua alipokuwa mzee na umri wake ukiwa umesogea sana, Bwana akamwambia, “Wewe ni mzee sana, na bado kumesalia sehemu kubwa sana za nchi ambazo ni za kutwaliwa.
2 Quest'[è] il paese che resta: tutte le contrade de' Filistei, e tutto il [paese] de' Ghesuriti;
“Nchi iliyosalia ni hii: maeneo yote ya Wafilisti na Wageshuri:
3 da Sihor, che [è] a fronte all'Egitto, fino a' confini di Ecron, verso Settentrione, [il paese] è riputato de' Cananei; [cioè: ] i cinque principati de' Filistei, quel di Gaza, quel di Asdod, quel di Ascalon, quel di Gat, e quel di Ecron, e gli Avvei;
kutoka Mto Shihori ulioko mashariki mwa Misri, kuelekea kaskazini kwenye eneo la Ekroni, ambayo yote ilihesabika kama ya Wakanaani (maeneo yale matano ya watawala wa Kifilisti, ambayo ni Gaza, Ashdodi, Ashkeloni, Gathi na Ekroni: ndiyo nchi ya Waavi);
4 dal Mezzodì, tutto il paese de' Cananei, e Meara, che [è] de' Sidonii, fino ad Afec, fino a' confini degli Amorrei;
kuanzia kusini, nchi yote ya Wakanaani, kuanzia Ara ambayo ni ya Wasidoni, ikienea hadi Afeki, na eneo la Waamori,
5 e il paese de' Ghiblei, e tutto il Libano, dal Sol levante, da Baal-gad, [che è] sotto il monte di Hermon, fino all'entrata di Hamat;
eneo la Wagebali; Lebanoni yote kuelekea mashariki, kuanzia Baal-Gadi chini ya Mlima Hermoni hadi Lebo-Hamathi.
6 tutti gli abitanti del monte, dal Libano fino alle Acque calde; [e] tutti i Sidonii. Io li caccerò dal cospetto dei figliuoli d'Israele; spartisci pur questo [paese] a sorte ad Israele per eredità, come io t'ho comandato.
“Na kuhusu wakaaji wote katika maeneo ya milima, kuanzia Lebanoni hadi Misrefoth-Maimu, pamoja na eneo lote la Wasidoni, mimi mwenyewe nitawafukuza watoke mbele ya Waisraeli. Hakikisha umegawa nchi hii kwa Israeli kuwa urithi, kama nilivyokuagiza,
7 Ora dunque spartisci questo paese a nove tribù, e alla metà della tribù di Manasse, in eredità.
sasa basi, ligawanye eneo hili kwa yale makabila tisa na ile nusu ya kabila la Manase kuwa urithi.”
8 I Rubeniti, e i Gaditi, con [l'altra metà del]la [tribù di Manasse], hanno ricevuta la loro eredità, la quale Mosè ha data loro, di là dal Giordano, verso Oriente; secondo che Mosè, servitor del Signore, l'ha data loro;
Ile nusu nyingine ya Manase, Wareubeni na Wagadi, walishapokea urithi Mose aliokuwa amewapa mashariki mwa Yordani, sawasawa na mtumishi wa Bwana alivyowagawia.
9 da Aroer, che [è] in sulla riva del torrente di Arnon, e la città che [è] in mezzo del torrente, e tutta la pianura di Medeba, fino a Dibon;
Eneo lao lilienea toka Aroeri, iliyoko ukingoni mwa Bonde la Arnoni kuanzia mji ulio katikati ya bonde, likijumlisha nchi ya uwanda wa juu wote wa Medeba mpaka Diboni,
10 e tutte le città di Sihon, re degli Amorrei, il qual regnò in Hesbon, fino a' confini dei figliuoli di Ammon;
nayo miji yote ya Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala Heshboni, hadi mpakani mwa Waamoni.
11 e Galaad, e le contrade de' Ghesuriti, e de' Maacatiti, e tutto il monte di Hermon, e tutto Basan, fino a Salca;
Vilevile ilijumlisha Gileadi, eneo la Wageshuri na Wamaaka, mlima wote wa Hermoni na Bashani yote ikienea hadi Saleka:
12 tutto il regno d'Og in Basan, il qual regnò in Astarot, e in Edrei, ed era restato del rimanente dei Rafei; Mosè percosse questi [re], e li scacciò.
yaani ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyekuwa ametawala katika Ashtarothi na Edrei, na ndiye pekee alisalia kwa Warefai. Mose alikuwa amewashinda na kuteka nchi yao.
13 (Or i figliuoli d'Israele non cacciarono i Ghesuriti, nè i Maacatiti; anzi i Ghesuriti ed i Maacatiti son dimorati per mezzo Israele fino al dì d'oggi.)
Lakini Waisraeli hawakuwafukuza watu wa Geshuri na wa Maaka, kwa hiyo wanaendelea kuishi miongoni mwa Waisraeli mpaka leo hii.
14 Solo alla tribù di Levi [Mosè] non diede alcuna eredità; i sacrificii da ardere del Signore Iddio d'Israele son la sua eredità, come egli ne ha parlato.
Lakini kwa kabila la Lawi, Mose hakupeana urithi, kwa kuwa sadaka za kuteketezwa kwa moto zilizotolewa kwa Bwana, Mungu wa Israeli, ndizo zilizokuwa urithi wao, kama alivyowaahidi.
15 Mosè adunque diede eredità alla tribù de' figliuoli di Ruben, secondo le lor nazioni.
Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Reubeni ukoo kwa ukoo:
16 E i lor confini furono da Aroer, che [è] in su la riva del torrente di Arnon, e la città che [è] in mezzo del torrente, e tutta la pianura fino a Medeba;
Eneo la Aroeri lililo ukingoni mwa Bonde la Arnoni, na kuanzia mji ulio katikati ya bonde, pia uwanda wote wa juu kupita Medeba
17 Hesbon, e tutte le sue città che [son] nella pianura; Dibon, e Bamot-baal, e Bet-baal-meon;
hadi Heshboni na miji yake yote kwenye uwanda wa juu, ikijumlishwa miji ya Diboni, Bamoth-Baali, Beth-Baal-Meoni,
18 e Iasa, e Chedemot, e Mefaat;
Yahasa, Kedemothi, Mefaathi,
19 e Chiriataim, e Sibma, e Seret-sahar, nel monte della valle;
Kiriathaimu, Sibma, Sereth-Shahari juu ya kilima kilicho katika bonde,
20 e Bet-peor, e Asdot-pisga, e Bet-iesimot;
Beth-Peori, materemko ya Pisga na Beth-Yeshimothi:
21 e tutte le città della pianura, e tutto il regno di Sihon, re degli Amorrei, che avea regnato in Hesbon, il qual Mosè percosse, insieme co' principi di Madian, Evi, e Rechem, e Sur, e Hur, e Reba, [ch'erano] principi [vassalli] di Sihon, e abitavano nel paese.
miji yote ya uwanda wa juu na eneo lote la utawala wa Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala katika Heshboni. Mose alikuwa amemshinda Sihoni, pia watawala wakuu wa Wamidiani, ambao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba, waliokuwa wameungana na Sihoni, ambao waliishi katika nchi ile.
22 I figliuoli d'Israele uccisero ancora con la spada Balaam, figliuolo di Beor, indovino, insieme con gli [altri] uccisi d'infra i Madianiti.
Pamoja na wale waliouawa katika vita, Waisraeli walikuwa wamemuua kwa upanga Balaamu mwana wa Beori aliyekuwa mchawi.
23 E i confini de' figliuoli di Ruben furono il Giordano e i confini. Questa [fu] l'eredità de' figliuoli di Ruben, secondo le lor nazioni, [cioè: ] quelle città e le lor villate.
Mpaka wa Wareubeni ulikuwa ni ukingo wa Mto Yordani. Miji hii na vijiji vyake ndiyo iliyokuwa urithi wa Wareubeni ukoo kwa ukoo.
24 Mosè diede ancora [eredità] alla tribù di Gad, a' figliuoli di Gad, secondo le lor nazioni.
Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo:
25 E la lor contrada fu Iaser, e tutte le città di Galaad, e la metà del paese de' figliuoli di Ammon, fino ad Aroer, che [è] a fronte a Rabba;
Nchi ya Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Amoni iliyoenea hadi Aroeri, karibu na Raba;
26 e da Hesbon fino a Ramatmispe, e Betonim; e da Mahanaim fino a' confini di Debir;
na kuanzia Heshboni mpaka Ramath-Mispa na Betonimu, na kutoka Mahanaimu hadi eneo la Debiri;
27 e nella valle, Bet-haram, e Bet-nimra, e Succot, e Safon, il rimanente del regno di Sihon, re di Hesbon; lungo il Giordano e i confini, infino all'estremità del mare di Chinneret, di là dal Giordano, verso Oriente.
na katika bonde, Beth-Haramu, Beth-Nimra, Sukothi na Safoni na sehemu iliyobaki ya eneo la utawala wa Sihoni mfalme wa Heshboni (upande wa mashariki mwa Mto Yordani, eneo inayoishia kwenye Bahari ya Kinerethi).
28 Questa [fu] l'eredità dei figliuoli di Gad, secondo le lor nazioni, [cioè: ] quelle città e le lor villate.
Miji hii na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Gadi ukoo kwa ukoo.
29 Mosè diede ancora [eredità] alla metà della tribù di Manasse: quella fu per la metà della tribù de' figliuoli di Manasse, secondo le lor nazioni.
Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa hiyo nusu ya kabila la Manase, yaani kwa nusu ya jamaa ya uzao wa Manase, ukoo kwa ukoo:
30 La lor contrada fu da Mahanaim, tutto Basan, tutto il regno d'Og, re di Basan, e tutte le villate di Iair, che [sono] in Basan, [che sono] sessanta terre;
Eneo lililoenea kuanzia Mahanaimu, na kujumlisha Bashani yote, ufalme wote wa Ogu mfalme wa Bashani, makazi yote ya Yairi huko Bashani, miji sitini,
31 e la metà di Galaad, e Astarot, ed Edrei, città del regno d'Og, in Basan. [Tutto ciò] fu [dato] a' figliuoli di Machir, figliuolo di Manasse, [cioè: ] alla metà de' figliuoli di Machir, secondo le lor nazioni.
nusu ya Gileadi, na Ashtarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani). Hii ilikuwa kwa ajili ya wazao wa Makiri mwana wa Manase, kwa ajili ya nusu ya wana wa Makiri, ukoo kwa ukoo.
32 Queste [son le contrade] che Mosè diede per eredità, nelle campagne di Moab, di là dal Giordano di Gerico, verso Oriente.
Huu ndio urithi alioupeana Mose wakati alipokuwa katika tambarare za Moabu, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko.
33 Ma egli non diede alcuna eredità ai figliuoli di Levi; il Signore Iddio d'Israele è la loro eredità, come egli [ne] ha lor parlato.
Lakini kwa kabila la Walawi, Mose hakuwapa urithi; Bwana Mungu, Mungu wa Israeli ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.

< Giosué 13 >