< Lamentazioni 5 >

1 RICORDATI, Signore, di quello che ci è avvenuto; Riguarda, e vedi li nostro vituperio.
Kumbuka, Ee Bwana, yaliyotupata, tazama, nawe uione aibu yetu.
2 La nostra eredità [è] stata trasportata agli stranieri, [E] le nostre case a' forestieri.
Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni, na nyumba zetu kwa wageni.
3 Noi siam divenuti orfani, senza padre; [E] le nostre madri come donne vedove.
Tumekuwa yatima wasio na baba, mama zetu wamekuwa kama wajane.
4 Noi abbiam bevuta la nostra acqua per danari, Le nostre legne ci sono state vendute a prezzo.
Ni lazima tununue maji tunayokunywa, kuni zetu zapatikana tu kwa kununua.
5 Noi abbiam sofferta persecuzione sopra il nostro collo; Noi ci siamo affannati, e non abbiamo avuto alcun riposo.
Wanaotufuatilia wapo kwenye visigino vyetu, tumechoka na hakuna pumziko.
6 Noi abbiam porta la mano agli Egizi, [Ed] agli Assiri, per saziarci di pane.
Tumejitolea kwa Misri na Ashuru tupate chakula cha kutosha.
7 I nostri padri hanno peccato, e non sono [più]; Noi abbiam portate le loro iniquità.
Baba zetu walitenda dhambi na hawapo tena, na sisi tunachukua adhabu yao.
8 De' servi ci hanno signoreggiati; Non [vi è stato] alcuno che [ci] abbia riscossi di man loro.
Watumwa wanatutawala na hakuna wa kutuokoa mikononi yao.
9 Noi abbiamo addotta la nostra vittuaglia A rischio della nostra vita, per la spada del deserto.
Tunapata chakula chetu kwa kuhatarisha maisha yetu kwa sababu ya upanga jangwani.
10 La nostra pelle è divenuta bruna come un forno, Per l'arsure della fame.
Ngozi yetu ina joto kama tanuru, kwa sababu ya fadhaa itokanayo na njaa.
11 Le donne sono state sforzate in Sion, E le vergini nelle città di Giuda.
Wanawake wametendwa jeuri katika Sayuni, na mabikira katika miji ya Yuda.
12 I principi sono stati impiccati per man di coloro; Non si è avuta riverenza alle facce de' vecchi.
Wakuu wametungikwa juu kwa mikono yao, wazee hawapewi heshima.
13 I giovani hanno portata la macinatura, E i fanciulli son caduti per le legne.
Vijana wanataabika kwenye mawe ya kusagia, wavulana wanayumbayumba chini ya mizigo ya kuni.
14 I vecchi hanno abbandonato le porte, E i giovani i loro suoni.
Wazee wameondoka langoni la mji, vijana wameacha kuimba nyimbo zao.
15 La gioia del nostro cuore è cessata, I nostri balli sono stati cangiati in duolo.
Furaha imeondoka mioyoni mwetu, kucheza kwetu kumegeuka maombolezo.
16 La corona del nostro capo è caduta; Guai ora a noi! perciocchè abbiam peccato.
Taji imeanguka kutoka kichwani petu. Ole wetu, kwa maana tumetenda dhambi!
17 Per questo il cuor nostro è languido; Per queste cose gli occhi nostri sono scurati.
Kwa sababu hiyo, mioyo yetu inazimia, kwa sababu ya hayo, macho yetu yamefifia,
18 Egli è perchè il monte di Sion è deserto, [Sì che] le volpi vi passeggiano.
kwa ajili ya Mlima Sayuni, ambao unakaa ukiwa, nao mbweha wanatembea juu yake.
19 Tu, Signore, dimori in eterno; Il tuo trono [è stabile] per ogni età.
Wewe, Ee Bwana unatawala milele, kiti chako cha enzi chadumu kizazi hadi kizazi.
20 Perchè ci dimenticheresti in perpetuo? [Perchè] ci abbandoneresti per lungo tempo?
Kwa nini watusahau siku zote? Kwa nini umetuacha kwa muda mrefu?
21 O Signore, convertici a te, e noi sarem convertiti: Rinnova i nostri giorni, come [erano] anticamente.
Turudishe kwako mwenyewe, Ee Bwana, ili tupate kurudi. Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale,
22 Perciocchè, ci hai tu del tutto riprovati? Sei tu adirato contro a noi fino all'estremo?
isipokuwa uwe umetukataa kabisa na umetukasirikia pasipo kipimo.

< Lamentazioni 5 >