< Neemia 11 >

1 OR i principali del popolo abitarono in Gerusalemme; e il rimanente del popolo tirò le sorti, per trarre delle dieci [parti del popolo] una, che abitasse in Gerusalemme, città santa; e le [altre] nove, nelle [altre] città.
Basi viongozi wa watu walikaa Yerusalemu, nao watu wale wengine walipiga kura ili kuleta mtu mmoja kati ya watu kumi aje kuishi Yerusalemu, mji mtakatifu, nao wengine tisa waliobaki wakae katika miji yao wenyewe.
2 E il popolo benedisse tutti coloro che volontariamente si presentarono ad abitare in Gerusalemme.
Watu waliwasifu wale wote waliojitolea kuishi Yerusalemu.
3 Or costoro [sono] i principali della provincia, i quali abitarono in Gerusalemme; [gli altri], Israeliti, sacerdoti, Leviti, Netinei, e figliuoli de' servi di Salomone, essendosi ridotti ad abitar nelle città di Giuda, ciascuno nella sua possessione, per le lor città.
Hawa ndio viongozi wa majimbo waliokuja kuishi Yerusalemu (baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi, watumishi wa Hekalu, na wazao wa watumishi wa Solomoni waliendelea kuishi katika miji ya Yuda, kila mmoja katika milki yake mwenyewe katika miji mbalimbali,
4 In Gerusalemme adunque abitarono de' figliuoli di Giuda, e de' figliuoli di Beniamino. De' figliuoli di Giuda: Ataia, figliuolo di Uzzia, figliuolo di Zaccaria, figliuolo di Amaria, figliuolo di Sefatia, figliuolo di Mahalaleel, d'infra i figliuoli di Fares;
ambapo watu wengine kutoka Yuda na Benyamini waliishi Yerusalemu). Kutoka wazao wa Yuda: Athaya mwana wa Uzia, mwana wa Zekaria, mwana wa Amaria, mwana wa Shefatia, mwana wa Mahalaleli, mzao wa Peresi.
5 e Maaseia, figliuolo di Baruc, figliuolo di Col-hoze, figliuolo di Hazaia, figliuolo di Adaia, figliuolo di Ioiarib, figliuolo di Zaccaria, figliuolo di Siloni;
Naye Maaseya mwana wa Baruku, mwana wa Kolhoze, mwana wa Hazaya, mwana wa Adaya, mwana wa Yoyaribu, mwana wa Zekaria, mzao wa Mshiloni.
6 tutti i figliuoli di Fares che abitarono in Gerusalemme, [furono] quattrocensessantotto uomini di valore.
Wazao wa Peresi walioishi Yerusalemu walikuwa 468, watu wenye uwezo.
7 E d'infra i figliuoli di Beniamino, [costoro: ] Sallu, figliuolo di Mesullam, figliuolo di Ioed, figliuolo di Pedaia, figliuolo di Colaia, figliuolo di Maaseia, figliuolo d'Itiel, figliuolo d'Isaia;
Kutoka wazao wa Benyamini: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Yoedi, mwana wa Pedaya, mwana wa Kolaya, mwana wa Maaseya, mwana wa Ithieli, mwana wa Yeshaya
8 e dopo lui, Gabbai, [e] Sallai; [in tutto] novecenventotto.
na wafuasi wake, Gabai na Salai watu 928.
9 E Ioel, figliuolo di Zicri, [era] costituito sopra loro; e Giuda, figliuolo di Senua, [era] la seconda persona [ordinata] sopra la città.
Yoeli mwana wa Zikri alikuwa afisa wao mkuu, naye Yuda mwana wa Hasenua alikuwa msimamizi juu ya Mtaa wa Pili katika mji.
10 De' sacerdoti: Iedaia, figliuolo di Ioiarib, Iachin,
Kutoka makuhani: Yedaya, mwana wa Yoyaribu, Yakini,
11 Seraia, figliuolo di Hilchia, figliuolo di Mesullam, figliuolo di Sadoc, figliuolo di Meraiot, figliuolo di Ahitub, conduttore della Casa di Dio;
Seraya mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu, msimamizi katika nyumba ya Mungu,
12 co' lor fratelli che facevano l'opera della Casa, [in numero di] ottocenventidue; ed Adaia, figliuolo di Ieroham, figliuolo di Pelalia, figliuolo di Amsi, figliuolo di Zaccaria, figliuolo di Pashur, figliuolo di Malchia;
pamoja na wenzao waliofanya kazi hekaluni: watu 822. Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia, mwana wa Amsi, mwana wa Zekaria, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya,
13 co' suoi fratelli, capi di [famiglie] paterne, [in numero di] dugenquarantadue; ed Amassai, figliuolo di Azareel, figliuolo di Azai, figliuolo di Messillemot, figliuolo d'Immer;
na wenzao, waliokuwa viongozi wa jamaa: watu 242. Amashisai mwana wa Azareli, mwana wa Azai, mwana wa Meshilemothi, mwana wa Imeri,
14 co' lor fratelli, [uomini] di valore, [in numero di] cenventotto; e Zabdiel, figliuolo di Ghedolim, [era] costituito sopra loro.
na wenzao waliokuwa wenye uwezo: watu 128. Afisa wao mkuu alikuwa Zabdieli mwana wa Hagedolimu.
15 E de' Leviti: Semaia, figliuolo di Hassub, figliuolo di Azricam, figliuolo di Hasabia, figliuolo di Buni;
Kutoka Walawi: Shemaya mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, mwana wa Buni;
16 e Sabbetai, e Iozabad, d'infra i capi de' Leviti, [erano ordinati] sopra l'opera di fuori della Casa di Dio.
Shabethai na Yozabadi, viongozi wawili wa Walawi, ambao walisimamia kazi za nje za nyumba ya Mungu;
17 E Mattania, figliuolo di Mica, figliuolo di Zabdi, figliuolo di Asaf, [era] il capo [dei cantori], il quale intonava le laudi nel tempo dell'orazione; e Bacbuchia, il secondo d'infra i fratelli di quello; ed Abda, figliuolo di Sammua, figliuolo di Galal, figliuolo di Iedutun.
Matania mwana wa Mika, mwana wa Zabdi, mwana wa Asafu, kiongozi aliyeongoza kutoa shukrani na maombi; Bakbukia aliyekuwa msaidizi wake kati ya wenzake; na Abda mwana wa Shamua, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni.
18 Tutti i Leviti [che abitarono] nella città santa, [erano] dugentottantaquattro.
Jumla ya Walawi waliokaa katika mji mtakatifu walikuwa watu 284.
19 E de' portinai: Accub, Talmon, co' lor fratelli, che facevano la guardia alle porte; [in numero di] censettantadue.
Mabawabu: Akubu, Talmoni na wenzao, waliolinda malango: watu 172.
20 E il rimanente degl'Israeliti, de' sacerdoti, [e] de' Leviti, [abitò] per tutte le città di Giuda, ciascuno nella sua possessione.
Waisraeli waliosalia, pamoja na makuhani na Walawi, walikuwa katika miji yote ya Yuda, kila mmoja katika urithi wa baba yake.
21 Ma i Netinei abitarono in Ofel; e Siha, e Ghispa, [erano] sopra i Netinei.
Watumishi wa Hekalu waliishi katika kilima cha Ofeli. Siha na Gishpa walikuwa wasimamizi wao.
22 E colui che avea la soprantendenza sopra i Leviti, in Gerusalemme, [era] Uzzi, figliuolo di Bani, figliuolo di Hasabia, figliuolo di Mattania, figliuolo di Mica. [E] i cantori, de' figliuoli di Asaf, [doveano esser del continuo] presenti all'opera della Casa di Dio.
Afisa mkuu wa Walawi huko Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani, mwana wa Hashabia, mwana wa Matania, mwana wa Mika. Uzi alikuwa mmoja wa wazao wa Asafu, waliokuwa waimbaji wenye kuwajibika kwa ajili ya huduma ya nyumba ya Mungu.
23 Perciocchè [v'era] per li cantori ordine del re, e [vi era] una provvisione assegnata per loro, giorno per giorno.
Waimbaji walikuwa chini ya amri za mfalme, ambazo pia ziliratibu shughuli zao za kila siku.
24 E Petahia, figliuolo di Mesezabeel, de' figliuoli di Zera, figliuolo di Giuda, [era] commessario del re, in ogni affare del re col popolo.
Pethahia mwana wa Meshezabeli, mmoja wa wazao wa Zera mwana wa Yuda, alikuwa mwakilishi wa mfalme katika mambo yote kuhusu mahusiano na watu.
25 Ora, quant'è alle villate, co' lor contadi, [quelli ch'erano] de' figliuoli di Giuda abitarono in Chiriat-Arba, e [nel]le terre del suo territorio; e in Dibon, e [nel]le terre del suo territorio; e in Iecabseel, e [nel]le sue villate;
Kuhusu vijiji na mashamba yake, baadhi ya watu wa Yuda waliishi Kiriath-Arba na makazi yaliyokizunguka, katika Diboni na makazi yake, katika Yekabzeeli na vijiji vyake,
26 e in Iesua, e in Molada, e in Bet-pelet,
katika Yeshua, katika Molada, katika Beth-Peleti,
27 e in Hasarsual, e in Beerseba, e ne' luoghi del suo territorio;
katika Hasar-Shuali, katika Beer-Sheba na makazi yake,
28 e in Siclag, e in Mecona, e ne' luoghi del suo territorio;
katika Siklagi, katika Mekona na makazi yake,
29 e in Enrimmon, e in Sorea,
katika En-Rimoni, katika Sora, katika Yarmuthi,
30 e in Iarmut, [in] Zanoa, [in] Adullam, e [nel]le lor villate; in Lachis, e nel suo contado; in Azeca, e ne' luoghi del suo territorio. E presero le loro stanze da Beerseba fino alla valle di Hinnom.
Zanoa, Adulamu na vijiji vyake, katika Lakishi na mashamba yake, na katika Azeka na makazi yake. Hivyo walikuwa wakiishi kuanzia Beer-Sheba mpaka Bonde la Hinomu.
31 E i figliuoli di Beniamino [abitarono] da Gheba, [in] Micmas, [in] Aia, ed [in] Betel, e ne' luoghi del suo territorio;
Wazao wa Wabenyamini kutoka Geba waliishi Mikmashi, Aiya, Betheli na makazi yake,
32 [in] Anatot, [in] Nob, [in] Anania,
katika Anathothi, Nobu na Anania,
33 [in] Hasor, [in] Rama, [in] Ghittaim,
katika Hazori, Rama na Gitaimu,
34 [in] Hadid, [in] Seboim, [in] Neballat,
katika Hadidi, Seboimu na Nebalati,
35 [in] Lod, ed [in] Ono, valle de' fabbri.
katika Lodi na Ono, na katika Bonde la Mafundi.
36 E i Leviti furono spartiti fra Guida e Beniamino.
Baadhi ya makundi ya Walawi wa Yuda waliishi huko Benyamini.

< Neemia 11 >